< Osée 6 >
1 « Venez, retournons à l'Éternel, car Il a déchiré et Il nous guérira, Il a frappé et Il bandera nos plaies.
“Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
2 Il nous rendra la vie dans deux jours, et le troisième Il nous mettra debout, afin que nous vivions devant lui.
Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
3 Apprenons donc à connaître, appliquons-nous à connaître l'Éternel! Tel que celui de l'aurore, son lever est certain; Il viendra à nous comme la rosée, comme la seconde pluie qui arrose la terre. »
Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
4 Que te ferai-je, Éphraïm, que te ferai-je, Juda? Car votre piété est comme les vapeurs du matin, et comme la rosée qui bientôt s'évanouit.
“Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
5 Pour cela je les frappe par mes prophètes, je les tue par les paroles de ma bouche, et tes châtiments apparaîtront comme la lumière.
Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
6 Car j'aime la piété et non les sacrifices, et la connaissance de Dieu plus que les victimes.
Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 Mais eux, comme Adam, violent l'alliance; ici même ils me sont infidèles.
Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
8 Galaad est une ville de malfaiteurs, elle porte des traces de sang.
Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9 Telle une bande de brigands aux aguets, telle est la confrérie des sacrificateurs; ils tuent sur le chemin de Sichem, oui, ils commettent des crimes.
Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
10 Dans la maison d'Israël je vois des horreurs; c'est la prostitution d'Éphraïm; Israël est souillé.
Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
11 A toi aussi, Juda, est préparée une moisson, quand je ramènerai les captifs de mon peuple.
“Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,