< Ézéchiel 29 >

1 La dixième année, le dixième mois, le douzième jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée en ces mots:
Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Fils de l'homme, tourne ton visage contre Pharaon, roi d'Egypte, et prophétise contre lui et contre toute l'Egypte;
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
3 parle et dis: Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: J'en veux à toi, Pharaon, roi d'Egypte, à toi le grand dragon couché au sein de ses fleuves, qui dis: « Mon fleuve est à moi, et je l'ai fait pour moi. »
Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
4 Je mettrai une boucle à ta mâchoire; et j'attacherai les poissons de tes fleuves à tes écailles, et te tirerai du sein de tes fleuves, avec tous les poissons de tes fleuves attachés à tes écailles.
Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
5 Puis je te jetterai au désert, toi et tous les poissons de tes fleuves, tu tomberas sur la face de la terre, et ne seras ni ramassé ni recueilli: aux bêtes de la terre et aux oiseaux des Cieux je te donne en proie.
Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
6 Et tous les habitants de l'Egypte comprendront que je suis l'Éternel. Parce qu'ils furent un appui de roseau pour la maison d'Israël,
Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
7 quand ils te prirent par ta poignée, tu te brisas y et leur fendis toute l'épaule, et quand ils s'appuyèrent sur toi, tu te cassas et ébranlas leurs reins.
Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
8 Aussi ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Voici je ferai fondre l'épée sur toi, et du milieu de toi j'exterminerai hommes et bêtes,
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
9 et l'Egypte deviendra un désert et une solitude, et ils sauront que je suis l'Éternel. Parce que [Pharaon] dit: « Le fleuve est à moi et je l'ai fait! »
Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
10 pour cela, j'en veux à toi et à tes fleuves, et je ferai du pays d'Egypte une solitude et un vaste désert de Migdol à Siène, et jusques aux confins de l'Ethiopie;
kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
11 le pied de l'homme ne le parcourra point, et le pied de l'animal ne le traversera point, et il ne sera plus habité pendant quarante ans;
Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
12 et je ferai du pays d'Egypte un désert entre les pays déserts, et entre les villes dévastées ses villes seront désertes pendant quarante ans, et je disperserai les Égyptiens parmi les nations et les disséminerai dans les pays divers.
Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
13 Cependant ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Au terme de quarante ans je rassemblerai les Égyptiens du milieu des peuples où ils auront été dispersés,
“‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
14 et je ramènerai les captifs de l'Egypte, et les ferai revenir au pays de Pathros dans leur pays d'origine, et là ils formeront un humble royaume:
Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
15 il sera plus humble que les royaumes, et ne s'élèvera plus au-dessus des peuples, et je les diminuerai, afin qu'ils ne dominent plus les peuples:
Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
16 et ils ne donneront plus à la maison d'Israël une confiance qui la faisait penser au crime, quand elle pouvait s'adresser à eux, et ils sauront que je suis le Seigneur, l'Éternel.
Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
17 Et la vingt-septième année, le premier mois, le premier jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée en ces mots:
Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
18 Fils de l'homme, Nébucadnézar, roi de Babel, a fait faire à son armée un service pénible contre Tyr; toutes les têtes sont chauves, et toutes les épaules pelées, et Tyr ne le paie ni lui, ni son armée, du service qu'il a fait contre elle.
“Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
19 Aussi, ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Voici, je donne à Nébucadnézar, roi de Babel, le pays d'Egypte, pour qu'il emmène son peuple, et emporte sa dépouille, et pille. son butin, et ce sera là le salaire de son armée.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
20 Pour prix du service qu'il a fait, je lui donne le pays d'Egypte, car ils ont travaillé pour moi, dit le Seigneur, l'Éternel.
Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
21 Dans ce même temps je ferai croître une corne à la maison d'Israël, et je t'ouvrirai la bouche au milieu d'eux, et ils sauront que je suis l'Éternel.
“Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

< Ézéchiel 29 >