< 2 Samuel 8 >
1 Et dans les temps qui suivirent, David battit les Philistins et les humilia, et ôta des mains des Philistins les rênes de leur métropole.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 Et il battit les Moabites, et il les mesura au cordeau, en les faisant coucher par terre, et il en mesura deux cordeaux pour les livrer à la mort et un cordeau entier pour leur laisser la vie. Ainsi, les Moabites furent asservis à David, et payèrent le tribut.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 Et David battit Hadadézer, fils de Rehob, roi de Tsoba, en allant reprendre la haute main sur l'Euphrate.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 Et David lui prit mille sept cents cavaliers, et vingt mille fantassins. David énerva tous les chevaux de trait, dont pourtant il garda cent pour lui.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 Et les Syriens de Damas vinrent au secours de Hadadézer, roi de Tsoba, et David tua aux Syriens vingt-deux mille hommes.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Et David mit des garnisons dans la Syrie de Damas, et les Syriens furent asservis à David et payèrent le tribut. Ainsi l'Éternel rendait David victorieux dans toutes ses expéditions.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 Et David prit les boucliers d'or que portaient les serviteurs d'Hadadézer et les apporta à Jérusalem.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 Et de Bétah et de Bérothaï, villes de Hadadézer, David enleva une très grande quantité d'airain.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 Et Thoï, roi de Hamath, apprit que David avait abattu toute la puissance de Hadadézer;
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 alors Thoï députa Joram, son fils, au Roi David pour le saluer, et pour le féliciter d'avoir fait la guerre à Hadadézer, et de l'avoir défait (car Thoï était en hostilité avec Hadadézer); et Joram apportait de la vaisselle d'argent, de la vaisselle d'or et de la vaisselle d'airain.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 Et le Roi David la consacra aussi à l'Éternel, de même que l'argent et l'or qu'il avait consacré sur les dépouilles de tous les peuples domptés par lui,
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 Syriens, Moabites, Ammonites, Philistins, Amalécites, et sur le butin de Hadadézer, fils de Rehob, roi de Tsoba.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 David acquit aussi un nom par la défaite des Syriens dans la vallée du sel, au nombre de dix-huit mille.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 Et il mit des garnisons dans l'Idumée, dans toute l'Idumée il mit des garnisons et toute l'Idumée fut asservie à David. Ainsi l'Éternel rendait David victorieux dans toutes ses campagnes.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 Et David régna sur la totalité d'Israël et exerça le droit et la justice sur la totalité de son peuple.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 Or Joab, fils de Tseruïa, était préposé sur l'armée, et Josaphat, fils d'Ahilud, était chancelier,
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 et Tsadoc, fils d'Ahitub, et Ahimélech, fils d'Abiathar, étaient Prêtres, et Seraïa, secrétaire,
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 et Benaïa, fils de Joïada, était préposé sur les satellites et les coureurs, et les fils de David étaient ministres.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.