< 2 Samuel 2 >
1 Et après ces événements, David interrogea l'Éternel en ces termes: Dois-je gagner l'une des villes de Juda? Et l'Éternel lui dit:
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 Oui. Et David dit: Laquelle? Et Il répondit: Hébron. Et David s'y transporta avec ses deux femmes, Ahinoam de Jizréel, et Abigaïl, femme de Nabal, le Carmélite.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 Il y emmena de même avec lui les hommes qui l'accompagnaient, chacun d'eux avec sa maison, et ils demeurèrent dans les villes attenantes à Hébron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Alors arrivèrent des hommes de Juda, et là ils oignirent David comme roi de la maison de Juda.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 Et l'on apporta cet avis à David: Ce sont les hommes de Jabès en Galaad, qui ont donné la sépulture à Saül. Aussitôt David dépêcha des envoyés aux hommes de Jabès en Galaad avec ce message: Soyez les bénis de l'Éternel pour votre acte de piété envers votre Seigneur, envers Saül à qui vous avez donné la sépulture.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Qu'en retour l'Éternel vous témoigne Son amour et Sa fidélité! de mon côté je vous donne ce témoignage de bonté, en suite de ce que vous avez fait.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Maintenant ayez toujours la main ferme, et soyez des braves! car si votre Seigneur Saül est mort, moi, j'ai été oint par la maison de Juda pour être son Roi.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Cependant Abner, fils de Ner, général d'armée de Saül, prit Isboseth, fils de Saül, et le fit passer à Mahanaïm
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 et l'établit roi de Galaad, et des Assurites et de Jizréel, et d'Ephraïm et de Benjamin, ainsi de tout Israël.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Isboseth, fils de Saül, avait quarante ans, lorsqu'il devint roi d'Israël, et il régna deux ans; la maison de Juda seule s'attachait à David.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 Et la durée du temps que David passa à Hébron, comme roi de la maison de Juda, fut de sept ans et six mois.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Et Abner, fils de Ner, avec les serviteurs d'Isboseth, fils de Saül, sortit de Mahanaïm pour marcher sur Gabaon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Et Joab, fils de Tseruïa, et les serviteurs de David se mirent en campagne, et ils se rencontrèrent de part et d'autre à l'étang de Gabaon, et ils prirent position ceux-ci d'un côté de l'étang, ceux-là de l'autre.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Alors Abner dit à Joab: Prenons pour champions des jeunes gens soldats, et qu'ils s'escarmouchent devant nous! Et Joab dit: Prenons ces champions.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Et ils se mirent sur pied et ils s'avancèrent au nombre de douze pour Benjamin et Isboseth, fils de Saül, et douze des serviteurs de David.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Et chacun d'eux saisit la tête de son adversaire, et chacun d'eux enfonça son épée dans le flanc de son adversaire, et ils tombèrent tous à la fois. Et l'on donna à cet emplacement le nom de Helkath-Hatsourim (champ des lames): il est près de Gabaon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 En cette journée le combat fut très rude et Abner et les hommes d'Israël furent défaits par les serviteurs de David.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Et il y avait là trois fils de Tseruïa: Joab et Abisaï et Hasahel. Et Hasahel avait dans ses pieds l'agilité d'une gazelle qui court dans les champs.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Et Hasahel poursuivait Abner sans s'écarter ni à droite ni à gauche des traces d'Abner.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Et Abner se tournant en arrière dit: Est-ce toi qui es Hasahel? Et il répondit: C'est moi-même.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Et Abner lui dit: Tire-toi de côté à ta droite ou à ta gauche, et attaque-toi à l'un de ces jeunes hommes, et t'empare de son armure. Mais Hasahel ne voulut pas se désister de sa poursuite.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Et Abner répéta à Hasahel: Renonce à me poursuivre! pourquoi devrais-je t'étendre sur le carreau? Comment alors pourrais-je me présenter à ton frère Joab?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 Mais il refusa de céder. Alors Abner lui porta au ventre un coup du talon de sa lance qui ressortit par derrière, et Hasahel tomba et mourut sur la place. Et tous ceux qui arrivaient à l'endroit où Hasahel était tombé et mort, s'arrêtaient.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Et Joab et Abisaï poursuivirent Abner, et au coucher du soleil ils atteignirent le monticule d'Amma, situé devant Giah sur la route du désert de Gabaon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 Et les Benjaminites vinrent se grouper à la suite d'Abner et se formèrent en légion et prirent position au sommet d'un coteau.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Alors Abner s'adressant à Joab lui dit: L'épée sera-t-elle donc toujours dévorante? Ne sais-tu pas qu'il ne résultera que misère? Combien de temps encore veux-tu ne pas dire au peuple de renoncer à poursuivre des frères?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Et Joab dit: Par la vie de Dieu! si tu n'avais pas parlé, c'est demain seulement que le peuple aurait été ramené de la poursuite de ses frères.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Puis Joab sonna de la trompette, et tout le peuple fit halte, et cessa de harceler Israël et ne continua pas la guerre.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Cependant Abner et ses hommes employèrent toute cette même nuit à traverser la plaine, et ils passèrent le Jourdain et traversèrent tout le Bithron et gagnèrent Mahanaïm.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Et Joab renonçant à la poursuite d'Abner, rassembla tout le peuple; et des serviteurs de David il manquait dix-neuf hommes et Hasahel.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 D'un autre côté les serviteurs de David avaient frappé dans Benjamin et la troupe d'Abner, trois cent soixante hommes, à mort.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Et ils emportèrent Hasahel et lui donnèrent la sépulture dans le tombeau de son père à Bethléhem. Et Joab et ses hommes marchèrent toute la nuit et avec le jour ils arrivaient à Hébron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.