< 2 Chroniques 15 >

1 Or Azaria, fils de Oded, reçut l'Esprit de Dieu.
Roho ya Mungu ikaja juu ya Azaria mwana wa Odedi.
2 Et il alla au-devant d'Asa et lui dit: Écoutez-moi, Asa, et vous tous de Juda et de Benjamin! L'Éternel a été avec vous, parce que vous ayez été avec Lui; et si vous Le cherchez, Il se laissera trouver par vous; mais si vous L'abandonnez, Il vous abandonnera.
Akaenda nje kukutana na Asa na akamwambia, “Nisikilize, Asa, na Yuda wote na Benyamini: Yahwe yuko pamoja nanyi, pale mnapokuwa naye. Kama mtamtafuta, mtampata; lakini kama mtamsahau, atawasahau ninyi.
3 Il y a eu pour Israël de longs jours sans vrai Dieu et sans Prêtre enseignant, et sans Loi;
Sasa kwa muda mrefu, Israeli hawakuwa na Mungu wa kweli, bila kuhani wa kufundisha, na bila sheria.
4 mais comme dans la détresse ils revinrent à l'Éternel, Dieu d'Israël, et le cherchèrent, Il se laissa trouver par eux.
Lakini katika dhiki yao wakamrudia Yahwe, Mungu wa Israeli, na wakamtafuta, wakamta.
5 Dans ces temps-là il n'y avait point de sûreté pour qui sortait et qui entrait, mais une grande perturbation affectait tous les habitants du pays.
Katika nyakati hizo hapakuwa na amani kwake aliyesafiri kwend mbali, wala kwake aliyesafiri kuja hapa; badala yake shsida kubwa zilikuwa juu ya wenyeji wote wa wanchi.
6 Un peuple se heurtait contre un peuple et une ville contre une ville; car Dieu les inquiétait par toutes sortes de tribulations.
Waligawanyika vikundi vikundi, taifa dhidi ya taifa, na mji dhidi ya mji, kwa maana Mungu aliwapa shsida za kila aina ya kila mateso.
7 Mais vous, restez fermes et n'ayez pas les mains lâches; car il est un salaire pour vos œuvres.
Lakini muwe hodari, na msiuache mkono wenu kuwa dhaifu, kwa maana kazi yen itapewa thawabu.”
8 Et lorsque Asa entendit ces paroles et la prophétie de Oded, le prophète, il s'encouragea et extermina toutes les horreurs de tout le pays de Juda et de Benjamin, et des villes qu'il avait conquises dans la montagne d'Ephraïm, et il restaura l'autel de l'Éternel qui est devant le vestibule de l'Éternel.
Asa aliposikia maneno haya, unabii wa odedi nabii, akajipa ujasiri na kuviondosha mbali vitu vya kuchukiza kutoka nchi yote ya Yuda na Benyamini, na kutoka miji yote aliyokuwa ameiteka kuanzia kilima cha nchi ya Efraimu, na akaijenga tena madhabahu ya Yahwe, ambayo ilikuwa mbele ya ukumbi wa nyumba ya Yahwe.
9 Et il assembla tout Juda et Benjamin et avec eux les étrangers d'Ephraïm et de Manassé et de Siméon; car une multitude de gens étaient passés chez lui d'Israël, lorsqu'ils virent que l'Éternel, son Dieu, était avec lui.
Akawakusanya Yuda wote na Benyamini, na wae waliokaa pamoja nao—watu wa kutoka Efraimu na Manase, na kutoka Simeoni. Kwa maana walikuja kwake katika hesabu kubwa kutoka Israeli, walipoona kwamba Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye.
10 Et ils s'assemblèrent à Jérusalem au troisième mois, la quinzième année du règne d'Asa,
Kwa hiyo wakakusanyika katika Yerusalemu katika mwezzi wa tatu, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11 et dans cette journée ils sacrifièrent à l'Éternel, sur le butin qu'ils avaient remporté, sept cents taureaux et sept mille moutons,
Katika siku hiyo walimtolea Yahwe dhabihu baadhi ya nyara ambazo walikuwa wameleta; ng'mbe wa kulima mia saba na kondoo na mbuzi elfu saba.
12 et conclurent l'engagement de chercher l'Éternel, Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme;
Wakaingia kataika agano kwa ajili ya kumtafuta Yahwe, Mungu wa babau zao, kwa moyo wao wote na roho yao yote.
13 et quiconque ne chercherait pas l'Éternel, Dieu d'Israël, subirait la mort, petit et grand, homme et femme.
Wakakubaliana kwamba yeyote atakepuuzia kumtafuta Yahwe, Mungu wa Israeli, atapaswa kuuawa, iwe mdogo ama mkubwa, iwe mwanaume ama mwanamke.
14 Et ils prêtèrent serment à l'Éternel d'une voix forte et par acclamation et au son des trompettes et des clairons:
Wakaapa kwa Yahwe kwa sauti kubwa, kwa kelele, na kwa sauti za tarumbeta na baragumu.
15 et tout Juda se réjouit du serment, car ils l'avaient prêté de tout leur cœur, et c'était de leur plein gré qu'ils le cherchaient, et Il se laissa trouver par eux, et l'Éternel leur donna paix de toutes parts.
Yuda wote wakakifurahia kile kiaapo. kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote, na walimtafuta Mungu kwa nia yao yote, na walimuona. Yahwe akawapa amani pande zote.
16 Et même il destitua Maacha, mère du roi Asa, de sa qualité de reine, pour avoir fait une idole Astarté; et Asa mit son idole en pièces, et la broya et la brûla dans la vallée du Cédron.
Pia akamwondoa Maaka, asiwe malikia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza ya Maashera. Asa akaivunja vunja sanamu ya kuchukiza, akaiweka kwenye mavumbi akaichoma moto huko kijitoni Kidroni.
17 Mais les tertres ne disparurent pas d'Israël, néanmoins le cœur d'Asa resta intact toute sa vie.
Lakini sehemu za juu hazikuwa zimeondolewa nje ya Israeli. Vile vile, Moyo wa Asa ulijitoa kikamilifu siku zake zote.
18 Et il introduisit ce que son père avait consacré et ce que lui-même avait consacré, dans le temple de Dieu, argent, or et meubles.
Akaleta kwenye nyumba ya Mungu vitu vya baba yake na vitu vyake mwenyewe vilivyokuwa vya Yahwe: vitu vya fedha na dhahabu.
19 Et il n'y eut pas guerre jusqu'à la trente-cinquième année du règne d'Asa.
Hapakuwa na vita zaidi hadi miaka thelathini na mitano ya utawala wa Asa.

< 2 Chroniques 15 >