< Zacharie 13 >

1 En ce jour-là, il y a aura une source ouverte à la maison de David et aux habitants de Jérusalem, pour le péché et pour la souillure.
Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
2 Il arrivera aussi, en ce jour-là, dit l'Éternel des armées, que je retrancherai du pays les noms des idoles, et il n'en sera plus fait mention; et j'ôterai aussi du pays les prophètes et l'esprit impur.
Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
3 Et il arrivera que si quelqu'un prophétise encore, son père et sa mère qui l'auront engendré lui diront: Tu ne vivras plus, car tu dis des mensonges au nom de l'Éternel! Et son père et sa mère qui l'auront engendré, le transperceront quand il prophétisera.
Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
4 En ce jour-là, les prophètes seront confus, chacun de sa vision, quand ils prophétiseront; et ils ne se revêtiront plus du manteau de poil pour mentir.
Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
5 Et chacun d'eux dira: Je ne suis pas prophète; je suis un laboureur, car on m'a acheté dès ma jeunesse.
Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
6 Et quand on lui dira: Qu'est-ce que ces blessures à tes mains? il répondra: C'est dans la maison de mes amis qu'on me les a faites.
Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
7 Épée, réveille-toi contre mon pasteur, contre l'homme qui est mon compagnon, dit l'Éternel des armées! Frappe le pasteur, et les brebis seront dispersées; et je tournerai ma main contre les petits.
Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
8 Et il arrivera dans tout le pays, dit l'Éternel, que deux parties seront retranchées et périront, mais la troisième y demeurera de reste.
Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
9 Et je ferai passer cette troisième partie au feu; je les affinerai comme on affine l'argent, et je les éprouverai comme on éprouve l'or. Ceux-là invoqueront mon nom, et je les exaucerai. Je dirai: C'est mon peuple! et ils diront: L'Éternel est mon Dieu!
Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”

< Zacharie 13 >