< Zacharie 1 >

1 La seconde année du règne de Darius, au huitième mois, la parole de l'Éternel fut adressée au prophète Zacharie, fils de Barachie, fils d'Iddo, en ces mots:
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 L'Éternel a été fort indigné contre vos pères.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Tu leur diras donc: Ainsi a dit l'Éternel des armées: Revenez à moi, dit l'Éternel des armées, et je reviendrai à vous, dit l'Éternel des armées.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Ne soyez pas comme vos pères, que les premiers prophètes ont appelés, en disant: Ainsi a dit l'Éternel des armées: Détournez-vous de vos voies mauvaises et de vos mauvaises actions; mais ils n'ont pas écouté, ils n'ont point fait attention à ma parole, dit l'Éternel.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Vos pères, où sont-ils? Et ces prophètes devaient-ils toujours vivre?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 Cependant mes paroles et mes ordres, que j'avais donnés aux prophètes mes serviteurs, ne se sont-ils pas accomplis sur vos pères? Ils sont revenus, et ils ont dit: Tout ce que l'Éternel des armées avait résolu de nous faire, selon nos voies et selon nos actions, il l'a exécuté sur nous.
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 Le vingt-quatrième jour du onzième mois, qui est le mois de Shébat, la seconde année de Darius, la parole de l'Éternel fut adressée au prophète Zacharie, fils de Barachie, fils d'Iddo, en ces mots:
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 J'eus la nuit une vision; et voici, un homme monté sur un cheval roux; il se tenait parmi les myrtes qui étaient dans le fond; et, après lui, des chevaux roux, bais et blancs.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 Et je dis: Mon Seigneur, qui sont-ils? Et l'ange qui me parlait me dit: Je vais te faire voir ce que sont ces chevaux.
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 Et l'homme qui se tenait parmi les myrtes, répondit et dit: Ce sont ceux que l'Éternel a envoyés pour parcourir la terre.
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 Et ils répondirent à l'ange de l'Éternel, qui se tenait parmi les myrtes, et dirent: Nous avons parcouru la terre; et voici, toute la terre est tranquille et en repos.
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Alors l'ange de l'Éternel répondit et dit: Éternel des armées! jusqu'à quand n'auras-tu pas compassion de Jérusalem et des villes de Juda, contre lesquelles tu es indigné depuis soixante et dix ans?
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 Et l'Éternel répondit à l'ange qui me parlait, de bonnes paroles, des paroles de consolation.
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 Et l'ange qui me parlait me dit: Crie, et dis: Ainsi a dit l'Éternel des armées: Je suis jaloux pour Jérusalem, pour Sion, d'une grande jalousie;
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 Et je suis courroucé d'un grand courroux contre ces nations tranquilles; car, lorsque j'étais un peu courroucé, elles ont aidé au mal.
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 C'est pourquoi, ainsi a dit l'Éternel: Je reviens vers Jérusalem avec compassion; ma maison y sera rebâtie, dit l'Éternel des armées, et le cordeau sera étendu sur Jérusalem.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 Crie encore, et dis: Ainsi a dit l'Éternel des armées: Mes villes regorgeront encore de biens, et l'Éternel consolera encore Sion, et il élèvera encore Jérusalem.
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 Puis je levai les yeux et regardai; et je vis quatre cornes.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 Et je dis à l'ange qui me parlait: Qu'est-ce que ces cornes? Et il me dit: Ce sont les cornes qui ont dispersé Juda, Israël et Jérusalem.
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 Puis l'Éternel me fit voir quatre forgerons.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 Et je dis: Qu'est-ce que ceux-ci viennent faire? Et il répondit: Ce sont là les cornes qui ont dispersé Juda, tellement que personne n'osait lever la tête; mais ceux-ci sont venus pour les effrayer, pour abattre les cornes des nations, qui ont levé la corne contre le pays de Juda pour le disperser.
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zacharie 1 >