< Psaumes 85 >

1 Éternel, tu as été propice envers ta terre; tu as ramené les captifs de Jacob.
Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2 Tu as pardonné l'iniquité de ton peuple; tu as couvert tous leurs péchés. (Sélah)
Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
3 Tu as retiré tout ton courroux; tu es revenu de l'ardeur de ta colère.
Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4 Rétablis-nous, ô Dieu de notre salut, et fais cesser ton indignation contre nous!
Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5 Seras-tu toujours courroucé contre nous? Feras-tu durer ta colère d'âge en âge?
Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6 Ne reviendras-tu pas nous rendre la vie, afin que ton peuple se réjouisse en toi?
Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
7 Fais-nous voir ta bonté, ô Éternel, et accorde-nous ta délivrance!
Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
8 J'écouterai ce que dit Dieu, l'Éternel, car il parlera de paix à son peuple et à ses bien-aimés, afin qu'ils ne retournent plus à la folie.
Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
9 Oui, son salut est près de ceux qui le craignent, afin que la gloire habite dans notre terre.
Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
10 La bonté et la vérité se sont rencontrées; la justice et la paix se sont entrebaisées.
Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
11 La vérité germera de la terre, et la justice regardera des cieux.
Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
12 L'Éternel aussi donnera ses biens, et notre terre donnera ses fruits.
Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
13 La justice marchera devant lui, et il la mettra partout où il passera.
Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.

< Psaumes 85 >