< Psaumes 81 >

1 Chantez avec allégresse à Dieu, notre force; jetez des cris de réjouissance au Dieu de Jacob!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Entonnez le chant; faites résonner le tambourin, la harpe agréable avec la lyre.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Sonnez de la trompette à la nouvelle lune, à la pleine lune, au jour de notre fête.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 Car c'est une loi pour Israël, une ordonnance du Dieu de Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 Il en fit un statut pour Joseph, quand il sortit contre le pays d'Égypte; là j'entendis un langage que je ne connaissais pas.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 J'ai déchargé, dit-il, son épaule du fardeau; ses mains ont lâché la corbeille.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 Tu as crié dans la détresse, et je t'ai délivré; je t'ai répondu, caché dans le tonnerre; je t'ai éprouvé aux eaux de Mériba. (Sélah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Écoute, mon peuple, et je t'exhorterai; Israël, si tu m'écoutais!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 Qu'il n'y ait point chez toi de dieu étranger; ne te prosterne pas devant les dieux des nations!
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 Je suis l'Éternel, ton Dieu, qui t'ai fait remonter du pays d'Égypte. Ouvre ta bouche, et je la remplirai.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 Mais mon peuple n'a pas écouté ma voix; Israël n'a pas voulu m'obéir.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 Et je les ai abandonnés à la dureté de leur cœur, pour marcher selon leurs conseils.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Oh! si mon peuple voulait m'écouter, qu'Israël marchât dans mes voies!
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 J'eusse en un instant fait ployer leurs ennemis, j'aurais tourné ma main contre leurs adversaires.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 Ceux qui haïssent l'Éternel eussent flatté Israël, et son temps heureux eût toujours duré.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 Dieu les eût nourris de la mœlle du froment. Je t'eusse rassasié du miel du rocher.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psaumes 81 >