< Psaumes 80 >

1 Pasteur d'Israël, prête l'oreille; toi qui mènes Joseph comme un troupeau, toi qui sièges entre les chérubins, fais briller ta splendeur!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Devant Éphraïm, Benjamin et Manassé, réveille ta puissance et viens nous sauver.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 O Dieu! rétablis-nous; fais luire ta face, et nous serons sauvés!
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Éternel, Dieu des armées, jusques à quand ta colère fumera-t-elle contre la prière de ton peuple?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Tu leur fais manger un pain de larmes, et tu leur fais boire des larmes à pleine mesure.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Tu fais de nous un sujet de contestations pour nos voisins, et nos ennemis se raillent de nous entre eux.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Dieu des armées! rétablis-nous; fais luire ta face, et nous serons sauvés!
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Tu enlevas de l'Égypte une vigne; tu chassas des nations et tu la plantas.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Tu préparas le sol devant elle; elle poussa ses racines et remplit la terre.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Les montagnes se couvraient de son ombre, et les cèdres de Dieu de ses sarments.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Elle étendait ses pampres jusqu'à la mer, et ses rejetons jusqu'au fleuve.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Pourquoi as-tu rompu ses clôtures, en sorte que tous les passants la pillent?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Que le sanglier des forêts la dévaste, et que les bêtes des champs la broutent?
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Dieu des armées, reviens! Regarde des cieux, et vois, et visite cette vigne.
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 Protège ce que ta droite a planté, et le fils que tu t'es choisi.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Elle est brûlée, elle est coupée. Ils périssent devant le courroux de ta face.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Que ta main soit sur l'homme de ta droite, sur le fils de l'homme que tu t'es choisi;
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Et nous ne nous détournerons plus de toi; rends-nous la vie, et nous invoquerons ton nom.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Éternel, Dieu des armées, rétablis-nous; fais luire ta face, et nous serons sauvés!
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psaumes 80 >