< Psaumes 77 >

1 Ma voix s'adresse à Dieu, et je crie, ma voix s'adresse à Dieu, et il m'écoutera.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 Au jour de ma détresse, j'ai cherché le Seigneur; la nuit, ma main était étendue vers lui et ne se lassait point; mon âme refusait d'être consolée.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 Je me souvenais de Dieu, et je gémissais; je méditais, et mon esprit était abattu. (Sélah, pause)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Tu avais retenu mes yeux dans les veilles; j'étais troublé, je ne pouvais parler.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 Je pensais aux jours d'autrefois, aux années des temps passés.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 Je me rappelais mes mélodies de la nuit; je méditais en mon cœur, et mon esprit examinait.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 Le Seigneur rejettera-t-il pour toujours, ne sera-t-il plus désormais propice?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Sa bonté a-t-elle cessé pour toujours? Sa parole a-t-elle pris fin pour tous les âges?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Dieu a-t-il oublié d'avoir pitié? A-t-il dans sa colère fermé ses compassions?
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 Et j'ai dit: Voilà ce qui fait ma souffrance: C'est que la droite du Très-Haut a changé.
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 Je me rappellerai les exploits de l'Éternel, me souvenant de tes merveilles d'autrefois;
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 Je méditerai sur toutes tes œuvres, et je considérerai tes hauts faits.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 O Dieu, tes voies sont saintes! Quel autre Dieu est grand comme Dieu?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 Tu es le Dieu qui fait des merveilles; tu as fait connaître ta force parmi les peuples.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 Par ton bras, tu rachetas ton peuple, les enfants de Jacob et de Joseph. (Sélah)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 Les eaux te virent, ô Dieu! Les eaux te virent; elles tremblèrent; même les abîmes s'émurent.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 Les nues se répandirent en eaux; les nuages tonnèrent; tes traits aussi volèrent çà et là.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 Ton tonnerre gronda dans le tourbillon; les éclairs brillèrent sur le monde; la terre s'émut et trembla.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Tu as fait ton chemin dans la mer, tes sentiers dans les grandes eaux; et tes traces n'ont point été connues.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Tu as conduit ton peuple comme un troupeau, par la main de Moïse et d'Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< Psaumes 77 >