< Psaumes 27 >

1 Psaume de David. L'Éternel est ma lumière et ma délivrance; de qui aurais-je peur? L'Éternel est le rempart de ma vie; de qui aurais-je de la crainte?
Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
2 Quand les méchants, mes adversaires et mes ennemis, sont venus contre moi pour me dévorer, eux-mêmes ont bronché et sont tombés.
Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
3 Quand une armée camperait contre moi, mon cœur ne craindrait point; quand la guerre s'élèverait contre moi, ce sera là ma confiance.
Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
4 J'ai demandé une seule chose à l'Éternel, et je la rechercherai: c'est d'habiter dans la maison de l'Éternel tous les jours de ma vie, pour contempler la beauté de l'Éternel, et pour visiter son palais.
Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
5 Car il m'abritera dans sa tente au mauvais jour; il me cachera dans le lieu secret de son tabernacle; il m'élèvera comme sur un rocher.
Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
6 Et maintenant ma tête s'élèvera au-dessus de mes ennemis qui sont autour de moi; j'offrirai dans son tabernacle des sacrifices de cris de joie; je chanterai et je psalmodierai à l'Éternel.
Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
7 Éternel, écoute ma voix, je t'invoque; aie pitié de moi et m'exauce!
Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
8 Mon cœur me dit de ta part: Cherchez ma face. Je cherche ta face, ô Éternel!
Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
9 Ne me cache pas ta face! Ne rejette pas ton serviteur dans ton courroux! Tu as été mon aide; ne me délaisse pas, ne m'abandonne pas, Dieu de mon salut!
Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
10 Quand mon père et ma mère m'auraient abandonné, l'Éternel me recueillera.
Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
11 Éternel, enseigne-moi ta voie, et me conduis dans le droit chemin, à cause de mes ennemis.
Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
12 Ne me livre pas au désir de mes adversaires; car de faux témoins et qui ne respirent que violence, se sont élevés contre moi.
Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
13 Ah! si je n'avais cru que je verrais les biens de l'Éternel dans la terre des vivants!
Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
14 Attends-toi à l'Éternel, demeure ferme, que ton cœur se fortifie; oui, attends-toi à l'Éternel!
Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!

< Psaumes 27 >