< Proverbes 24 >

1 Ne porte point envie aux hommes méchants, et ne désire point être avec eux.
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 Car leur cœur médite la ruine et leurs lèvres parlent de nuire.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 C'est par la sagesse que la maison sera bâtie, et c'est par l'intelligence qu'elle sera affermie.
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 Et c'est par la science que les chambres seront remplies de tous les biens précieux et agréables.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 L'homme sage est plein de force, et l'homme intelligent devient puissant.
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Car c'est avec la prudence qu'on fait la guerre, et la victoire dépend du nombre des conseillers.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 La sagesse est trop élevée pour un insensé; il n'ouvrira pas la bouche aux portes.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 Celui qui pense à faire mal, on l'appellera maître en méchanceté.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 Un mauvais dessein est une folie, et le moqueur est en abomination aux hommes.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Si tu perds courage au jour de la détresse, ta force sera petite.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Délivre ceux qui sont traînés à la mort, et qui sont sur le point d'être tués.
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 Si tu dis: Voici, nous n'en avons rien su; celui qui pèse les cœurs ne l'entendra-t-il point? Et celui qui garde ton âme ne le saura-t-il point? Et ne rendra-t-il pas à chacun selon son œuvre?
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Mon fils, mange le miel, car il est bon, et le rayon de miel, qui est doux à ton palais.
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Telle sera la connaissance de la sagesse à ton âme; quand tu l'auras trouvée, il y aura une bonne issue, et ton attente ne sera point trompée.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 Méchant, ne tends pas d'embûches contre la demeure du juste, et ne dévaste pas son habitation.
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Car le juste tombera sept fois, et il sera relevé; mais les méchants sont précipités dans le malheur.
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 Quand ton ennemi sera tombé, ne t'en réjouis point; et quand il sera renversé, que ton cœur ne s'en égaie point;
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 De peur que l'Éternel ne le voie, et que cela ne lui déplaise, et qu'il ne détourne de lui sa colère.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 Ne t'irrite point à cause de ceux qui font le mal; ne porte point envie aux méchants;
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 Car il n'y a pas d'issue pour celui qui fait le mal, et la lampe des méchants sera éteinte.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Mon fils, crains l'Éternel et le roi, et ne te mêle point avec des gens remuants.
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 Car leur ruine surviendra tout d'un coup, et qui sait le malheur qui arrivera aux uns et aux autres?
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 Voici encore ce qui vient des sages: Il n'est pas bon d'avoir égard à l'apparence des personnes dans le jugement.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 Celui qui dit au méchant: Tu es juste, les peuples le maudiront, et les nations le détesteront.
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 Mais ceux qui le reprennent s'en trouveront bien; sur eux viendront la bénédiction et le bonheur.
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Celui qui répond avec droiture à quelqu'un, lui donne un baiser sur les lèvres.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 Règle ton ouvrage au-dehors, et mets ordre à ton champ; et puis tu bâtiras ta maison.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 Ne sois point témoin contre ton prochain sans qu'il soit nécessaire: voudrais-tu séduire par tes lèvres?
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 Ne dis point: Je lui ferai comme il m'a fait; je rendrai à cet homme selon son œuvre.
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 J'ai passé près du champ d'un paresseux, et près de la vigne d'un homme dépourvu de sens;
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 Et voici, les chardons y croissaient partout; les ronces en couvraient la surface, et son mur de pierre était écroulé.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Quand je vis cela, j'y appliquai mes pensées; je le regardai, j'en tirai instruction.
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 Un peu dormir, un peu sommeiller, un peu croiser les mains pour se reposer,
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 Et ta pauvreté viendra comme un passant, et ta disette comme un homme armé.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< Proverbes 24 >