< Proverbes 20 >

1 Le vin est moqueur, et la boisson forte est tumultueuse, et quiconque en fait excès, n'est pas sage.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 La menace du roi est comme le rugissement d'un jeune lion; celui qui l'irrite pèche contre soi-même.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 C'est une gloire pour l'homme de s'abstenir des disputes; mais tout insensé s'y engage.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Le paresseux ne labourera point à cause du mauvais temps; lors de la moisson il mendiera; mais il n'aura rien.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Le conseil dans le cœur de l'homme est une eau profonde; et l'homme intelligent y puisera.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 La plupart des hommes vantent leur bonté; mais qui trouvera un homme véritable?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 Le juste marche dans son intégrité; heureux ses enfants après lui!
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Le roi assis sur le trône de la justice, dissipe tout mal par son regard.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Qui est-ce qui peut dire: J'ai purifié mon cœur; je suis net de mon péché?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Le double poids et la double mesure sont tous deux en abomination à l'Éternel.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 L'enfant fait déjà connaître par ses actions, si sa conduite sera pure et droite.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 L'oreille qui entend, et l'œil qui voit, sont deux choses que l'Éternel a faites.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 N'aime point le sommeil, de peur que tu ne deviennes pauvre; ouvre tes yeux, et tu seras rassasié de pain.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 Celui qui achète, dit: Cela ne vaut rien, cela ne vaut rien; puis il s'en va, et se vante.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Il y a de l'or, et beaucoup de perles; mais les lèvres sages sont un vase précieux.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Quand quelqu'un aura cautionné un étranger, prends son vêtement et exige de lui un gage, à cause des étrangers.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Le pain acquis par la tromperie est agréable à l'homme; mais ensuite sa bouche sera remplie de gravier.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Les résolutions s'affermissent par le conseil; fais donc la guerre avec prudence.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Le médisant révèle les secrets; évite donc celui qui aime ouvrir ses lèvres.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 La lampe de celui qui maudit son père ou sa mère, sera éteinte dans les plus profondes ténèbres.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 L'héritage trop vite acquis à l'origine, ne sera point béni à la fin.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Ne dis point: Je rendrai le mal; mais attends l'Éternel, et il te délivrera.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Le double poids est en abomination à l'Éternel, et la balance fausse n'est pas chose bonne.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 Cest l'Éternel qui dirige les pas de l'homme; comment donc l'homme comprendrait-il sa voie?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 C'est un piège pour l'homme que de prononcer légèrement une promesse sacrée, et, après ses vœux, d'examiner encore.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 Le roi sage dissipe les méchants, et fait tourner la roue sur eux.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 L'esprit de l'homme est une lampe de l'Éternel; il sonde les profondeurs de l'âme.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 La bonté et la vérité garderont le roi; il soutient son trône par la bonté.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 La force des jeunes gens est leur gloire, et les cheveux blancs sont l'honneur des vieillards.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Les meurtrissures des plaies sont la correction du méchant, ainsi que les coups qui atteignent les profondeurs des entrailles.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.

< Proverbes 20 >