< Proverbes 19 >

1 Le pauvre qui marche dans son intégrité, vaut mieux que celui qui parle avec perversité et qui est insensé.
Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
2 Une âme sans prudence n'est pas un bien, et celui qui se précipite dans ses démarches, s'égare.
Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
3 C'est la folie de l'homme qui renverse ses voies; et c'est contre l'Éternel que son cœur murmure.
Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
4 Les richesses amènent beaucoup d'amis; mais le pauvre est délaissé, même de son ami.
Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
5 Le faux témoin ne demeurera point impuni, et celui qui profère des mensonges, n'échappera point.
Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6 Plusieurs flattent celui qui est généreux, et chacun est ami de l'homme qui donne.
Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7 Tous les frères du pauvre le haïssent; combien plus ses amis se retireront-ils de lui! Il les presse de ses paroles: ils ne sont plus là!
Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8 Celui qui acquiert du sens, aime son âme, et celui qui conserve la prudence, trouvera le bien.
Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9 Le faux témoin ne demeurera point impuni, et celui qui profère des mensonges, périra.
Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
10 Il ne sied pas à un insensé de vivre dans les délices; combien moins à un esclave de dominer sur les grands!
Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
11 L'homme prudent retient sa colère; et son honneur, c'est d'oublier les offenses.
Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
12 L'indignation du roi est comme le rugissement d'un jeune lion; mais sa faveur est comme la rosée sur l'herbe.
Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
13 Un enfant insensé est un grand malheur pour son père; et les querelles d'une femme sont une gouttière continuelle.
Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
14 Une maison et des richesses sont l'héritage venu des pères; mais une femme prudente est un don de l'Éternel.
Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
15 La paresse produit l'assoupissement, et l'âme paresseuse aura faim.
Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16 Celui qui garde le commandement, garde son âme; mais celui qui ne veille pas sur ses voies, mourra.
Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17 Celui qui a pitié du pauvre, prête à l'Éternel, et il lui rendra son bienfait.
Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18 Châtie ton enfant pendant qu'il y a de l'espérance, mais ne va pas jusques à le faire mourir.
Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19 Celui qui se laisse emporter par la colère, en portera la peine; et si on l'en exempte, il faudra y revenir.
Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20 Écoute le conseil et reçois l'instruction, afin que tu sois sage jusques à la fin de tes jours.
Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21 Il y a des pensées en grand nombre dans le cœur de l'homme; mais le conseil de l'Éternel est immuable.
Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22 Ce qui fait la valeur de l'homme, c'est sa miséricorde; car le pauvre vaut mieux que le menteur.
Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23 La crainte de l'Éternel conduit à la vie; et celui qui l'a sera rassasié, et passera la nuit sans être visité d'aucun mal.
Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24 Le paresseux plonge sa main dans le plat; et il ne la ramène pas à sa bouche.
Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25 Si tu bats le moqueur, le simple en deviendra avisé; et si tu reprends un homme intelligent, il entendra ce qu'il faut savoir.
Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26 L'enfant qui fait honte et dont on rougit, ruine son père et fait fuir sa mère.
Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27 Garde-toi, mon fils, d'écouter les conseils qui pourraient te détourner des paroles de la sagesse.
Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28 Un témoin pervers se moque de la justice, et la bouche des méchants se repaît d'iniquité.
Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29 Les jugements sont préparés pour les moqueurs, et les coups pour le dos des insensés.
Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.

< Proverbes 19 >