< Proverbes 13 >

1 L'enfant sage écoute l'instruction de son père; mais le moqueur n'écoute point la réprimande.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 L'homme sera rassasié de bien par le fruit de sa bouche; mais l'âme des perfides vit d'injustice.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Celui qui garde sa bouche, garde son âme; mais celui qui ouvre trop ses lèvres, y trouvera sa perte.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 L'âme du paresseux ne fait que souhaiter, et il n'a rien; mais l'âme des diligents sera rassasiée.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Le juste hait la parole de mensonge; mais le méchant se rend odieux, et tombe dans la confusion.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 La justice garde celui qui marche dans l'intégrité; mais la méchanceté renversera celui qui s'égare.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Tel se fait riche qui n'a rien du tout; et tel se fait pauvre qui a de grands biens.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 Les richesses font qu'un homme peut racheter sa vie; mais le pauvre n'entend point de menaces.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 La lumière des justes réjouira; mais la lampe des méchants s'éteindra.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 L'orgueil ne produit que des querelles; mais la sagesse est avec ceux qui prennent conseil.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Les richesses mal acquises, seront diminuées; mais celui qui amasse par son travail, les multipliera.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 L'espérance différée fait languir le cœur; mais le souhait accompli est comme l'arbre de vie.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Celui qui méprise la parole, se perd; mais celui qui respecte le commandement, en aura la récompense.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 L'enseignement du sage est une source de vie, pour détourner des pièges de la mort.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Une raison saine donne de la grâce; mais la voie de ceux qui agissent perfidement, est rude.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Tout homme bien avisé agit avec intelligence; mais l'insensé fait voir sa folie.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Le méchant messager tombera dans le mal; mais le messager fidèle apporte la guérison.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 La pauvreté et l'ignominie arriveront à celui qui rejette l'instruction; mais celui qui profite de la réprimande, sera honoré.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Le souhait accompli est une chose douce à l'âme; mais se détourner du mal fait horreur aux insensés.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 Celui qui fréquente les sages, deviendra sage; mais le compagnon des fous se perdra.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Le mal poursuit les pécheurs; mais le bonheur est la récompense des justes.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 L'homme de bien transmettra son héritage aux enfants de ses enfants; mais les richesses du pécheur sont réservées pour le juste.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Il y a beaucoup à manger dans le champ défriché par le pauvre; mais il y a des hommes qui périssent faute de jugement.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Celui qui épargne la verge, hait son fils; mais celui qui l'aime se hâte de le châtier.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Le juste mangera et sera rassasié à souhait; mais le ventre des méchants aura disette.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

< Proverbes 13 >