< Michée 3 >

1 Et je dis: Écoutez, chefs de Jacob, et vous, conducteurs de la maison d'Israël! N'est-ce pas à vous de connaître le droit?
Nimesema'”Sasa sikilizeni, ninyi viongozi wa Yakobo na kutawala nyumba ya Israeli: Je siyo sahihi kwenu kuielewa haki?
2 Vous qui haïssez le bien et qui aimez le mal, qui leur arrachez la peau et la chair de dessus les os!
Ninyi manaochukia mazuri na kupenda uovu, ninyi mnaoambua ngozi yao, miili yao kutoka kwenye mifupa yao-
3 Ils dévorent la chair de mon peuple, lui enlèvent la peau, et lui brisent les os, et les mettent en pièces comme pour la marmite, et comme de la chair dans une chaudière.
ninyi mnaokula pia miili ya watu wangu, na kuambua ngozi yao, kuvunja mifupa yao, na kuwakatakata katika vipande vipande, kama nyama kwenye chungu, kama nyama kwenye sufuria kubwa.
4 Alors ils crieront à l'Éternel, mais il ne leur répondra pas; il leur cachera sa face en ce temps-là, parce que leurs actions ont été mauvaises.
Kisha ninyi watawala mtalia kwa Yahwe, lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwenu kipindi hicho, kwasababu mmefanya matendo maovu.”
5 Ainsi a dit l'Éternel contre les prophètes qui égarent mon peuple, qui publient la paix quand leurs dents ont de quoi mordre, et qui préparent la guerre contre celui qui ne leur met rien dans la bouche.
Yahwe asema hivi kuhusu manabii ambao wawafanyao watu wangu kushindwa, “Kwa wale wawalishao wanatangaza, 'Kutakuwa na ustawi.' Lakini kwa wale wasioweka kitu kwenye vinywa vyao, wanaanzisha vita dhidi yake.
6 C'est pourquoi, au lieu de vision vous aurez la nuit, au lieu de divination les ténèbres; le soleil se couchera sur les prophètes, et le jour s'obscurcira sur eux.
Kwa hiyo, itakuwa usiku kwenu usiokuwa na maono juu yenu; itakuwa giza ili kwamba msiweze kubashiri. Jua litakwenda chini juu ya manabii, na siku itakuwa giza juu yao.
7 Les voyants seront confus, et les devins rougiront de honte; tous se couvriront la barbe, car il n'y aura point de réponse de Dieu.
Waonaji watawekwa kwenye aibu, waaguzi wa watachanganyikiwa. Wote watafunga midomo yao, kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu.”
8 Mais moi, je suis rempli de force, de l'Esprit de l'Éternel, de jugement et de courage, pour déclarer à Jacob son crime et à Israël son péché.
Lakini kwangu, nimejazwa nguvu kutoka kwa Roho wa Yahwe, na nimejaa haki na uweza, kumwambia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 Écoutez ceci, chefs de la maison de Jacob, et vous, conducteurs de la maison d'Israël, qui avez la justice en abomination, et qui pervertissez tout ce qui est droit:
Sasa sikieni hii, ninyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, na watawala wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao mnaochukia haki, na kupotosha kila haki.
10 On bâtit Sion avec le sang, et Jérusalem avec l'iniquité!
Mnaijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Ses chefs jugent pour des présents, ses sacrificateurs enseignent pour un salaire, et ses prophètes prédisent pour de l'argent; et ils s'appuient sur l'Éternel, disant: “L'Éternel n'est-il pas parmi nous? Le mal ne viendra pas sur nous! “
Viongozi wenu huhukumu kwa rushwa, makuhani wenu hufundisha kwa hijara, na manabii wenu hufanya utabiri kwa ajili ya pesa. Hata hivyo bado mtamtegemea Yahwe na kusema, “Je hayupo Yahwe pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.”
12 C'est pourquoi, à cause de vous, Sion sera labourée comme un champ, Jérusalem sera changée en un monceau de ruines, et la montagne du temple en une haute forêt.
Kwa hiyo, kwasababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msituni.

< Michée 3 >