< Marc 1 >

1 Commencement de l'Évangile de Jésus-Christ, Fils de Dieu.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 Conformément à ce qui avait été écrit dans les prophètes: Voici, j'envoie mon messager devant ta face, qui préparera le chemin devant toi:
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 Voix de celui qui crie dans le désert: Préparez le chemin du Seigneur; aplanissez ses sentiers.
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 Jean baptisait dans le désert, et prêchait le baptême de repentance, pour la rémission des péchés.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 Et toute la Judée et les habitants de Jérusalem allaient à lui, et ils étaient tous baptisés par lui dans le fleuve du Jourdain, en confessant leurs péchés.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 Jean était vêtu de poils de chameau, il avait une ceinture de cuir autour de ses reins, et il se nourrissait de sauterelles et de miel sauvage.
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 Et il prêchait en disant: Il en vient un après moi, qui est plus puissant que moi, et dont je ne suis pas digne, en me baissant, de délier la courroie des souliers.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 Pour moi je vous ai baptisés d'eau, mais lui vous baptisera du Saint-Esprit.
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 Il arriva, en ce temps-là, que Jésus vint de Nazareth de Galilée, et il fut baptisé par Jean dans le Jourdain.
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 Et aussitôt, comme il sortait de l'eau, il vit les cieux s'ouvrir et le Saint-Esprit descendre sur lui comme une colombe.
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 Et une voix vint des cieux, qui dit: Tu es mon Fils bien-aimé, en qui j'ai pris plaisir.
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 Et aussitôt l'Esprit poussa Jésus au désert.
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 Et il fut là au désert quarante jours, étant tenté par Satan; et il était avec les bêtes sauvages, et les anges le servaient.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 Or, après que Jean eut été mis en prison, Jésus s'en alla en Galilée, prêchant l'évangile du royaume de Dieu, et disant:
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 Le temps est accompli, et le royaume de Dieu approche. Repentez-vous et croyez à l'Évangile.
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 Or, comme il marchait le long de la mer de Galilée, il vit Simon et André son frère, qui jetaient leurs filets dans la mer; car ils étaient pêcheurs.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 Alors Jésus leur dit: Suivez-moi, et je vous ferai pêcheurs d'hommes.
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 Et aussitôt, laissant leurs filets, ils le suivirent.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Et de là passant un peu plus avant, il vit dans une barque Jacques, fils de Zébédée, et Jean son frère, qui raccommodaient leurs filets.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Au même instant il les appela; et eux, laissant Zébédée leur père dans la barque avec les ouvriers, le suivirent.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 Ensuite ils entrèrent à Capernaüm; et Jésus, étant d'abord entré dans la synagogue le jour du sabbat, y enseignait.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 Et ils étaient étonnés de sa doctrine; car il les enseignait comme ayant autorité, et non pas comme les scribes.
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 Or, il se trouva dans leur synagogue un homme possédé d'un esprit immonde, qui s'écria, et dit:
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 Ah! qu'y a-t-il entre toi et nous, Jésus Nazarien? Es-tu venu pour nous perdre? Je sais qui tu es; le Saint de Dieu.
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 Mais Jésus le tança en disant: Tais-toi, et sors de lui.
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 Alors l'esprit immonde l'agitant avec violence et jetant un grand cri, sortit de lui.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 Et ils furent tous étonnés, de sorte qu'ils se demandaient entre eux: Qu'est-ce que ceci? Quelle est cette nouvelle doctrine? Car il commande avec autorité même aux esprits immondes, et ils lui obéissent.
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Et sa réputation se répandit aussitôt par toute la contrée des environs de la Galilée.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 Aussitôt après, étant sortis de la synagogue, ils vinrent avec Jacques et Jean dans la maison de Simon et d'André.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Or, la belle-mère de Simon était au lit, malade de la fièvre; et aussitôt ils lui parlèrent d'elle.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 Alors s'approchant, il la fit lever en la prenant par la main; et au même instant la fièvre la quitta, et elle les servit.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 Sur le soir, quand le soleil fut couché, ils lui amenèrent tous les malades, et les démoniaques.
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 Et toute la ville était assemblée à la porte de la maison.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 Et il guérit plusieurs malades de diverses maladies, et il chassa plusieurs démons, ne leur permettant pas de dire qu'ils le connaissaient.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 Le matin, comme il faisait encore fort obscur, s'étant levé, il sortit et s'en alla dans un lieu écarté; et il y priait.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 Et Simon, et ceux qui étaient avec lui allèrent à sa recherche.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 Et l'ayant trouvé, ils lui dirent: Tous te cherchent.
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 Et il leur dit: Allons dans les bourgades voisines, afin que j'y prêche aussi; car c'est pour cela que je suis venu.
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 Et il prêchait dans leurs synagogues, par toute la Galilée, et il chassait les démons.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 Et un lépreux vint à lui, se jeta à genoux, le pria et lui dit: Si tu veux, tu peux me nettoyer.
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Et Jésus, ému de compassion, étendit la main, le toucha, et lui dit: Je le veux, sois nettoyé.
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 Et dès qu'il eut dit cela, la lèpre quitta aussitôt cet homme, et il fut nettoyé.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 Et Jésus le renvoya aussitôt avec de sévères recommandations, et lui dit:
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 Garde-toi d'en rien dire à personne; mais va-t'en et montre-toi au sacrificateur, et offre pour ta purification ce que Moïse a commandé, afin que cela leur serve de témoignage.
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 Mais cet homme étant sorti, se mit à publier hautement la chose et à la divulguer, en sorte que Jésus ne pouvait plus entrer ouvertement dans la ville; mais il se tenait dehors dans des lieux écartés, et de toutes parts on venait à lui.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.

< Marc 1 >