< Marc 10 >

1 Jésus étant parti de là, vint aux confins de la Judée, le long du Jourdain; et le peuple s'assembla encore vers lui, et il continua à les instruire, comme il avait accoutumé.
Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
2 Alors les pharisiens vinrent et lui demandèrent, pour l'éprouver: Est-il permis à un homme de répudier sa femme
Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 Il répondit et leur dit: Qu'est-ce que Moïse vous a commandé?
Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
4 Ils lui dirent: Moïse a permis d'écrire une lettre de divorce, et de répudier.
Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 Et Jésus, répondant, leur dit: Il vous a écrit cette loi à cause de la dureté de votre cœur.
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 Mais au commencement de la création, Dieu ne fit qu'un homme et qu'une femme.
Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
7 C'est pourquoi l'homme quittera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme;
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
8 Et les deux seront une seule chair; ainsi ils ne sont plus deux, mais une seule chair.
Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9 Que l'homme ne sépare donc point ce que Dieu a joint.
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 Et les disciples l'interrogèrent encore sur ce sujet dans la maison;
Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
11 Et il leur dit: Quiconque répudiera sa femme et en épousera une autre, commettra un adultère à son égard;
Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
12 Et si la femme quitte son mari et en épouse un autre, elle commet un adultère.
Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
13 Alors on lui présenta de petits enfants, afin qu'il les touchât; mais les disciples reprenaient ceux qui les présentaient.
Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
14 Et Jésus ayant vu cela, en fut indigné, et il leur dit: Laissez venir à moi les petits enfants, et ne les en empêchez point; car le royaume de Dieu est pour ceux qui leur ressemblent.
Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
15 Je vous dis en vérité, que quiconque ne recevra pas le royaume de Dieu comme un petit enfant, n'y entrera point.
Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
16 Et les ayant pris entre ses bras, il leur imposa les mains et les bénit.
Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
17 Et comme ils sortaient pour se mettre en chemin, un homme accourut, et, s'étant mis à genoux devant lui, lui demanda: Bon Maître, que dois-je faire pour hériter de la vie éternelle? (aiōnios g166)
Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
18 Jésus lui dit: Pourquoi m'appelles-tu bon? Personne n'est bon, sauf Dieu seul.
Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 Tu connais les commandements: Ne commets point d'adultère; ne tue point; ne dérobe point; ne dis point de faux témoignage; ne commets point de fraude; honore ton père et ta mère.
Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
20 Il répondit: Maître, j'ai observé toutes ces choses dès ma jeunesse.
Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 Et Jésus, jetant les yeux sur lui, l'aima et lui dit: Il te manque une chose: Va, vends tout ce que tu as, et le donne aux pauvres, et tu auras un trésor dans le ciel; après cela viens, suis-moi, en te chargeant de la croix.
Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 Mais affligé de cette parole, il s'en alla tout triste, car il avait de grands biens.
Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Alors Jésus, regardant autour de lui, dit à ses disciples: Qu'il est difficile que ceux qui ont des richesses entrent dans le royaume de Dieu!
Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
24 Et ses disciples furent étonnés de ce discours. Mais Jésus, reprenant la parole, leur dit: Mes enfants, qu'il est difficile à ceux qui se confient dans les richesses d'entrer dans le royaume de Dieu!
Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
25 Il est plus aisé qu'un chameau passe par le trou d'une aiguille, qu'il ne l'est qu'un riche entre dans le royaume de Dieu.
Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 Et ils furent encore plus étonnés, et ils se disaient l'un à l'autre: Et qui peut donc être sauvé?
Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
27 Mais Jésus, les regardant, leur dit: Cela est impossible aux hommes, mais non à Dieu; car toutes choses sont possibles à Dieu.
Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
28 Alors Pierre se mit à lui dire: Voici, nous avons tout quitté, et nous t'avons suivi.
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
29 Et Jésus répondit: Je vous le dis en vérité: Il n'y a personne qui ait quitté maison, ou frères, ou sœurs, ou père, ou mère, ou femme, ou enfants, ou champs, à cause de moi et de l'Évangile,
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
30 Qui n'en reçoive dès à présent en ce siècle, cent fois autant, des maisons, des frères, des sœurs, des mères, des enfants, et des terres, avec des persécutions; et, dans le siècle à venir, la vie éternelle. (aiōn g165, aiōnios g166)
ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Mais plusieurs qui sont les premiers seront les derniers, et ceux qui sont les derniers seront les premiers.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 Or, ils étaient en chemin, montant à Jérusalem, Jésus marchait devant eux; et ils étaient effrayés et craignaient en le suivant. Et Jésus, prenant encore à part les douze, commença à leur dire ce qui lui devait arriver:
Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
33 Voici, nous montons à Jérusalem, et le Fils de l'homme sera livré aux principaux sacrificateurs et aux scribes, et ils le condamneront à la mort, et le livreront aux Gentils.
Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
34 Ils se moqueront de lui, ils le fouetteront, ils lui cracheront au visage, et le feront mourir; mais il ressuscitera le troisième jour.
ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
35 Alors Jacques et Jean, fils de Zébédée, vinrent à lui et dirent: Maître, nous voudrions que tu nous fisses ce que nous te demanderons.
Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
36 Et il leur dit: Que voulez-vous que je vous fasse?
Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
37 Ils lui dirent: Accorde-nous d'être assis dans ta gloire, l'un à ta droite et l'autre à ta gauche.
Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
38 Et Jésus leur dit: Vous ne savez ce que vous demandez. Pouvez-vous boire la coupe que je dois boire, et être baptisés du baptême dont je dois être baptisé?
Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
39 Ils lui dirent: Nous le pouvons. Et Jésus leur dit: Il est vrai que vous boirez la coupe que je dois boire, et que vous serez baptisés du baptême dont je dois être baptisé;
Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
40 Mais quant à être assis à ma droite ou à ma gauche, ce n'est pas à moi de l'accorder, si ce n'est à ceux à qui cela est destiné.
lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
41 Ce que les dix autres ayant entendu, ils commencèrent à s'indigner contre Jacques et Jean.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 Mais Jésus, les ayant appelés, leur dit: Vous savez que ceux qu'on regarde comme les chefs des nations les maîtrisent; et que les grands exercent leur autorité sur elles.
Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
43 Mais il n'en sera pas de même parmi vous; au contraire, quiconque voudra être grand parmi vous, sera votre serviteur.
Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
44 Et quiconque voudra être le premier d'entre vous, sera l'esclave de tous.
na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
45 Car le Fils de l'homme est venu, non pour être servi, mais pour servir et pour donner sa vie en rançon pour plusieurs.
Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
46 Ensuite ils arrivèrent à Jérico; et comme il en repartait avec ses disciples et une grande troupe, le fils de Timée, Bartimée, l'aveugle, était assis auprès du chemin, demandant l'aumône.
Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
47 Et ayant entendu que c'était Jésus de Nazareth qui passait, il se mit à crier et à dire: Jésus, fils de David, aie pitié de moi!
Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Et plusieurs le reprenaient, pour le faire taire; mais il criait encore plus fort: Fils de David, aie pitié de moi!
Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Et Jésus s'étant arrêté, dit qu'on l'appelât. Ils appelèrent donc l'aveugle, et lui dirent: Prends courage, lève-toi, il t'appelle.
Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
50 Et jetant son manteau, il se leva et vint vers Jésus.
Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
51 Alors Jésus, prenant la parole, lui dit: Que veux-tu que je te fasse? Et l'aveugle lui répondit: Maître, que je recouvre la vue.
Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
52 Et Jésus lui dit: Va, ta foi t'a guéri. Et aussitôt il recouvra la vue, et il suivait Jésus dans le chemin.
Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.

< Marc 10 >