< Juges 6 >

1 Or, les enfants d'Israël firent ce qui est mauvais devant l'Éternel, et l'Éternel les livra entre les mains des Madianites pendant sept ans.
Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
2 Et la main des Madianites fut puissante contre Israël. Et à cause des Madianites, les enfants d'Israël se firent des retraites dans les montagnes, des cavernes et des forts.
Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
3 Quand Israël avait semé, il arrivait que les Madianites montaient avec les Amalécites et les fils de l'Orient, et ils montaient contre lui.
Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
4 Ils faisaient un camp contre lui; ils détruisaient les récoltes du pays jusqu'à Gaza, et ne laissaient point de vivres en Israël, ni brebis, ni bœufs, ni ânes.
Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
5 Car ils montaient, eux et leurs troupeaux, et leurs tentes, comme une multitude de sauterelles; et eux et leurs chameaux étaient innombrables; et ils venaient dans le pays pour le ravager.
Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
6 Israël fut donc très appauvri par les Madianites, et les enfants d'Israël crièrent à l'Éternel.
Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
7 Alors, les enfants d'Israël ayant crié à l'Éternel au sujet des Madianites,
Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
8 L'Éternel envoya un prophète vers les enfants d'Israël. Et il leur dit: Ainsi parle l'Éternel, le Dieu d'Israël: Je vous ai fait monter hors d'Égypte, et je vous ai retirés de la maison de servitude;
Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
9 Je vous ai délivrés de la main des Égyptiens, et de la main de tous ceux qui vous opprimaient; je les ai chassés devant vous; je vous ai donné leur pays, et vous ai dit:
Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
10 Je suis l'Éternel votre Dieu, vous ne craindrez point les dieux des Amoréens, dans le pays desquels vous habitez. Mais vous n'avez point écouté ma voix.
Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
11 Puis l'ange de l'Éternel vint, et s'assit sous le térébinthe d'Ophra, qui appartenait à Joas, l'Abiézérite. Et Gédéon, son fils, battait du froment dans le pressoir, pour le soustraire aux Madianites.
Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
12 Et l'ange de l'Éternel lui apparut, et lui dit: Vaillant guerrier, l'Éternel est avec toi!
Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
13 Et Gédéon lui répondit: Hélas! Mon Seigneur, si l'Éternel est avec nous, pourquoi donc toutes ces choses nous sont-elles arrivées? Et où sont toutes ces merveilles que nos pères nous ont racontées, en disant: L'Éternel ne nous a-t-il pas fait monter hors d'Égypte? Car maintenant l'Éternel nous a abandonnés et nous a livrés entre les mains des Madianites.
Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
14 Et l'Éternel tourna sa face vers lui et lui dit: Va avec cette force que tu as, et délivre Israël de la main des Madianites. N'est-ce pas moi qui t'envoie?
Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
15 Et il lui répondit: Hélas! Mon Seigneur, avec quoi délivrerai-je Israël? Voici, mon millier est le plus pauvre en Manassé; et je suis le plus petit dans la maison de mon père.
Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
16 Et l'Éternel lui dit: Parce que je serai avec toi, tu battras les Madianites comme un seul homme.
Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
17 Et Gédéon lui dit: Si j'ai trouvé grâce à tes yeux, donne-moi un signe que c'est toi qui me parles.
Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
18 Ne t'éloigne point d'ici, jusqu'à ce que je revienne auprès de toi, et que j'apporte mon offrande, et que je la dépose devant toi. Et il dit: Je resterai jusqu'à ce que tu reviennes.
Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
19 Alors Gédéon rentra, et apprêta un chevreau de lait, et fit avec un épha de farine, des gâteaux sans levain. Il mit la viande dans un panier, et le bouillon dans un pot, et les lui apporta sous le térébinthe, et les lui présenta.
Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
20 Et l'ange de Dieu lui dit: Prends la viande et les gâteaux sans levain, et dépose-les sur ce rocher, et répands le bouillon. Et il fit ainsi.
Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
21 Alors l'ange de l'Éternel avança le bout du bâton qu'il avait en sa main, et toucha la chair et les gâteaux sans levain; et le feu monta du rocher, et consuma la chair et les gâteaux sans levain; et l'ange de l'Éternel disparut à ses y eux.
Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
22 Et Gédéon vit que c'était l'ange de l'Éternel, et il dit: Hélas, Seigneur Éternel! Car j'ai vu l'ange de l'Éternel face à face.
Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
23 Mais l'Éternel lui dit: Sois en paix, ne crains point, tu ne mourras pas.
Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
24 Et Gédéon bâtit là un autel à l'Éternel, et l'appela JÉHOVA-SHALOM (L'Éternel-Paix). Il existe encore aujourd'hui à Ophra des Abiézérites.
Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
25 Or, dans cette même nuit, l'Éternel lui dit: Prends le jeune taureau de ton père, et un second taureau de sept ans, et démolis l'autel de Baal qui est à ton père, et coupe l'emblème d'Ashéra qui est au-dessus.
Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
26 Et bâtis un autel à l'Éternel ton Dieu, sur le haut de ce lieu fort, dans l'enceinte; tu prendras le second taureau, et tu l'offriras en holocauste, avec le bois de l'emblème d'Ashéra que tu auras coupé.
Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
27 Et Gédéon prit dix hommes parmi ses serviteurs et fit comme l'Éternel lui avait dit; et comme il craignait la maison de son père et les gens de la ville, il le fit de nuit et non de jour.
Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
28 Et au matin les gens de la ville se levèrent de bonne heure, et voici, l'autel de Baal avait été démoli, et l'emblème d'Ashéra, qui était au-dessus, était coupé, et le second taureau était offert en holocauste sur l'autel qui avait été bâti.
Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
29 Et ils se dirent les uns aux autres: Qui a fait cela? Et ils s'en informèrent et firent des recherches, et on dit: C'est Gédéon, fils de Joas, qui l'a fait.
Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
30 Les gens de la ville dirent à Joas: Fais sortir ton fils, et qu'il meure; car il a démoli l'autel de Baal, et il a coupé l'emblème d'Ashéra qui était au-dessus.
Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
31 Et Joas répondit à tous ceux qui s'adressèrent à lui: Est-ce à vous de prendre parti pour Baal? Est-ce à vous de le sauver? Quiconque prendra parti pour Baal sera mis à mort avant que le matin vienne. S'il est dieu, qu'il plaide pour lui-même, puisqu'on a démoli son autel.
Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
32 Et en ce jour-là, on appela Gédéon Jérubbaal (que Baal plaide), disant: Que Baal plaide contre lui, puisque Gédéon a démoli son autel.
Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
33 Or, tous les Madianites, les Amalécites et les fils de l'Orient se rassemblèrent; ils passèrent le Jourdain, et campèrent dans la vallée de Jizréel.
Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
34 Et l'Esprit de l'Éternel revêtit Gédéon; il sonna de la trompette, et les Abiézérites s'assemblèrent pour le suivre.
Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
35 Il envoya aussi des messagers par toute la tribu de Manassé, qui s'assembla pour marcher après lui. Puis il envoya des messagers à Asser, à Zabulon, et à Nephthali, qui montèrent à leur rencontre.
Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
36 Et Gédéon dit à Dieu: Si tu veux délivrer Israël par mon moyen, comme tu l'as dit,
Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
37 Voici, je vais mettre une toison dans l'aire; si la rosée est sur la toison seule et que la terre reste sèche, je connaîtrai que tu délivreras Israël par ma main, comme tu me l'as dit.
tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
38 Et c'est ce qui arriva; car le lendemain il se leva de bonne heure, et, ayant pressé la toison, il en fit sortir une pleine coupe d'eau de rosée.
Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
39 Gédéon dit encore à Dieu: Que ta colère ne s'embrase point contre moi, et je ne parlerai plus que cette fois. Je te prie, que je fasse une épreuve avec la toison, pour cette fois seulement; que la toison seule reste sèche, et que la rosée soit sur tout le sol.
Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
40 Et Dieu fit ainsi cette nuit-là; la toison seule resta sèche, et la rosée fut sur tout le sol.
Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.

< Juges 6 >