< Juges 2 >

1 Or, l'ange de l'Éternel monta de Guilgal à Bokim, et il dit: Je vous ai fait monter hors d'Égypte, et je vous ai amenés dans le pays que j'avais juré à vos pères de vous donner. Et j'ai dit: Je n'enfreindrai jamais l'alliance que j'ai traitée avec vous,
Malaika wa Bwana akatoka Gilgali, akaenda Bokimu, akasema, “Nimekuleta kutoka Misri, na nimekuleta katika nchi niliyoapa kuwapa baba zako.
2 Et vous, vous ne traiterez point d'alliance avec les habitants de ce pays, et vous démolirez leurs autels. Mais vous n'avez point obéi à ma voix. Pourquoi avez-vous fait cela?
Nikasema, 'Sitakuvunja kamwe agano langu na wewe. Usifanye agano na wale wanaoishi katika nchi hii. Ziangushe madhabahu zao. Lakini hukusikiliza sauti yangu. Je! ni nini hiki ulichokifanya?
3 Aussi j'ai dit: Je ne les chasserai point devant vous; mais ils seront à vos côtés, et leurs dieux vous seront un piège.
Basi sasa nasema, “Sitawafukuza Wakanaani mbele yenu, nao watakuwa miiba kwenu, na miungu yao itakuwa mtego kwa ajili yenu.”
4 Et sitôt que l'ange de l'Éternel eut dit ces paroles à tous les enfants d'Israël, le peuple éleva la voix et pleura.
Malaika wa Bwana alipowaambia maneno hayo kwa watu wote wa Israeli, watu wakapiga kelele na kulia.
5 Et ils appelèrent ce lieu-là Bokim (les Pleurs), et ils y sacrifièrent à l'Éternel.
Waliita mahali hapo Bokimu. Hapo wakatoa dhabihu kwa Bwana.
6 Or, Josué ayant renvoyé le peuple, les enfants d'Israël allèrent chacun dans son héritage pour prendre possession du pays.
Yoshua alipowaruhusu watu waende zao, wana wa Israeli kila mmoja akaenda mahali alipopewa, wakiwa na umiliki wa ardhi yao.
7 Et le peuple servit l'Éternel tout le temps de Josué, et tout le temps des anciens qui survécurent à Josué et qui avaient vu les grandes œuvres que l'Éternel avait faites en faveur d'Israël.
Watu walimtumikia Bwana wakati wa maisha ya Yoshua na wazee walioendelea baada yake, ni wale waliokuwa wameona matendo yote makuu ya Bwana aliyoyafanya kwa Israeli.
8 Puis Josué, fils de Nun, serviteur de l'Éternel, mourut, âgé de cent dix ans,
Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, alikufa akiwa na umri wa miaka 110.
9 Et on l'ensevelit dans le territoire de son héritage, à Thimnath-Hérès, sur la montagne d'Éphraïm, au nord de la montagne de Gaash.
Wakamzika ndani ya mpaka wa nchi aliyopewa huko Timnath Heresi, katika mlima wa Efraimu, kaskazini mwa Mlima Gaash.
10 Et toute cette génération fut recueillie avec ses pères; et il s'éleva après elle une autre génération qui ne connaissait point l'Éternel, ni les œuvres qu'il avait faites pour Israël.
Kizazi hicho chote kilikusanyika kwa baba zao. Kizazi kingine kilichofuata baada yao ambao hakikumjua Bwana au kile alichokifanya kwa Israeli.
11 Les enfants d'Israël firent alors ce qui déplaît à l'Éternel, et ils servirent les Baalim.
Watu wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.
12 Et ils abandonnèrent l'Éternel, le Dieu de leurs pères, qui les avait fait sortir du pays d'Égypte; ils allèrent après d'autres dieux, d'entre les dieux des peuples qui les entouraient, et ils se prosternèrent devant eux; ainsi ils irritèrent l'Éternel.
Wakaondoka kwa Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa kutoka Misri. Wakaifuata miungu mingine, miungu ya watu waliokuwa karibu nao, nao wakaisujudia. Wakamkasirisha BWANA kwa sababu
13 Ils abandonnèrent donc l'Éternel, et servirent Baal et les Ashtharoth.
waliondoka kwa Bwana na kumwabudu Baal na Maashtoreti.
14 Et la colère de l'Éternel s'embrasa contre Israël, et il les livra entre les mains de gens qui les pillèrent; et il les vendit à leurs ennemis d'alentour, et ils ne purent plus tenir devant leurs ennemis.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawapa washambuliaji walioiba mali zao kutoka kwao. Aliwauza kama watumwa waliofanyika kwa nguvu za maadui zao waliowazunguka, hivyo hawakuweza kujikinga dhidi ya adui zao.
15 Partout où ils allaient, la main de l'Éternel était contre eux en mal, comme l'Éternel l'avait dit, et comme l'Éternel le leur avait juré. Ainsi ils furent dans une grande détresse.
Israeli walipokwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa dhidi yao kuwashinda, kama alivyowaapia. Na walikuwa katika shida kali.
16 Cependant l'Éternel leur suscitait des juges, qui les délivraient de la main de ceux qui les pillaient.
Ndipo Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa katika mikono ya wale waliokuwa wakiba mali zao.
17 Mais ils n'écoutaient pas même leurs juges, et ils se prostituaient à d'autres dieux; ils se prosternaient devant eux, et ils se détournaient promptement du chemin où leurs pères avaient marché en obéissant aux commandements de l'Éternel; ils ne firent pas de même.
Hata hivyo hawakuwasikiliza waamuzi wao. Hawakuwa waaminifu kwa Bwana na wakajitoa wenyewe kama makahaba kwa miungu mingine na kuabudu. Waligeuka upesi na kuiacha njia waliyoishi baba zao-wale waliotii amri za Bwana-lakini wao wenyewe hawakufanya hivyo.
18 Or, quand l'Éternel leur suscitait des juges, l'Éternel était avec le juge, et les délivrait de la main de leurs ennemis, pendant toute la vie du juge; car l'Éternel se repentait, à cause des gémissements qu'ils poussaient devant ceux qui les opprimaient et qui les accablaient.
Bwana aliinua waamuzi kwa ajili yao, Bwana akawasaidia waamuzi na kuwakomboa kutoka kwa mikono ya adui zao siku zote muamuzi aliishi. Bwana aliwahurumia walipougua kwa sababu ya wale waliowadhulumu na kuwasumbua.
19 Puis, quand le juge mourait, ils se corrompaient de nouveau plus que leurs pères, en allant après d'autres dieux, pour les servir et se prosterner devant eux; ils ne rabattaient rien de leurs actions, ni de leur train obstiné.
Lakini mwamuzi alipokufa, waligeuka na kufanya mambo ambayo yalikuwa mabaya zaidi kuliko baba zao walivyofanya. Wakaenda kuifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao yote mabaya au njia zao za ukaidi.
20 C'est pourquoi la colère de l'Éternel s'embrasa contre Israël, et il dit: Puisque cette nation a transgressé mon alliance que j'avais prescrite à ses pères, et qu'ils n'ont point obéi à ma voix,
Hasira ya Bwana iliwaka juu ya Israeli; akasema, Kwa sababu taifa hili limevunja masharti ya agano langu ambalo nililiweka kwa ajili ya baba zao-kwa sababu hawakuisikiliza sauti yangu.
21 Je ne déposséderai plus devant eux aucune des nations que Josué laissa quand il mourut;
Tangu sasa sitaliondoa mbele yao taifa lolote aliloliacha Yoshua baada ya kufa.
22 Afin de mettre par elles Israël à l'épreuve, pour voir s'ils garderont, ou non, la voie de l'Éternel pour y marcher, comme leurs pères l'ont gardée.
Nitafanya hivi ili kuwajaribu Israeli, ikiwa watafuata njia ya Bwana au sivyo, kama vile baba zao walivyoifuata.
23 Et l'Éternel laissa ces nations-là, sans se hâter de les déposséder, car il ne les avait point livrées entre les mains de Josué.
Ndiyo sababu Bwana aliwaacha mataifa hayo, wala hakuwafukuza haraka na kuwatia mikononi mwa Yoshua.

< Juges 2 >