< Juges 11 >

1 Jephthé, le Galaadite, était un vaillant guerrier, mais fils d'une femme prostituée; et c'était Galaad qui avait engendré Jephthé.
Yeftha Mgileadi alikuwa shujaa mwenye nguvu, lakini alikuwa mwana wa kahaba. Gileadi alikuwa baba yake.
2 Or la femme de Galaad lui avait enfanté des fils; et quand les fils de cette femme furent grands, ils chassèrent Jephthé, en lui disant: Tu n'auras point d'héritage dans la maison de notre père; car tu es fils d'une femme étrangère.
Mke wa Gileadi pia alizaa wanawe wengine. Wana wa mkewe walipokua, walimlazimisha Yeftha aondoke nyumbani na kumwambia, “Huwezi kurithi chochote kutoka katika familia yetu. Wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.”
3 Jephthé s'enfuit donc loin de ses frères, et habita dans le pays de Tob. Alors des gens de rien s'amassèrent auprès de Jephthé, et ils faisaient des incursions avec lui.
Basi Yeftha akaondoka toka kwa ndugu zake, akaishi katika nchi ya Tobu. Watu wasiokuwa na sheria waliungana na Yeftha na wakaja na kwenda pamoja naye.
4 Or, quelque temps après, les enfants d'Ammon firent la guerre à Israël.
Siku kadhaa baadaye, wana wa Amoni walipigana na Israeli.
5 Et comme les enfants d'Ammon faisaient la guerre à Israël, les anciens de Galaad allèrent chercher Jephthé au pays de Tob.
Wana wa Amoni walipopigana na Israeli, wazee wa Gileadi wakaenda kumleta Yeftha kutoka nchi ya Tobu.
6 Et ils dirent à Jephthé: Viens, et sois notre capitaine, et nous combattrons les enfants d'Ammon.
Wakamwambia Yeftha, “Njoo uwe kiongozi wetu ili tupigane na wana wa Amoni.”
7 Mais Jephthé répondit aux anciens de Galaad: N'est-ce pas vous qui m'avez haï? Et ne m'avez-vous pas chassé de la maison de mon père? Pourquoi venez-vous vers moi, maintenant que vous êtes en peine?
YEphtha akawaambia viongozi wa Gileadi, “mlinichukia na kunilazimisha kuondoka nyumbani kwa baba yangu. Kwa nini mnakuja kwangu sasa munapokuwa na shida?”
8 Alors les anciens de Galaad dirent à Jephthé: Nous revenons à toi maintenant, afin que tu marches avec nous, et que tu combattes les enfants d'Ammon, et que tu sois notre chef, celui de tous les habitants de Galaad.
Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Ndiyo sababu tunakugeukia sasa; njoo pamoja nasi pigana na watu wa Amoni, na wewe utakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.
9 Et Jephthé répondit aux anciens de Galaad: Si vous me ramenez pour combattre contre les enfants d'Ammon, et que l'Éternel les livre entre mes mains, je serai votre chef.
Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, “Ikiwa mnanirejesha nyumbani tena ili kupigana na wana wa Amoni, na kama Bwana atatupa ushindi juu yao, nitakuwa kiongozi wenu.”
10 Et les anciens de Galaad dirent à Jephthé: Que l'Éternel nous entende et nous juge, si nous ne faisons pas ce que tu as dit.
wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, “Bwana awe shahidi kati yetu ikiwa hatutafanya kama tunavyosema!”
11 Jephthé s'en alla donc avec les anciens de Galaad; et le peuple l'établit chef et capitaine, et Jephthé répéta devant l'Éternel, à Mitspa, toutes les paroles qu'il avait prononcées.
Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, nao watu wakamfanya awe msimamizi na mkuu juu yao. Alipokuwa mbele ya Bwana huko Mizpa, Yeftha akarudia ahadi zote alizozifanya.
12 Puis Jephthé envoya des messagers au roi des enfants d'Ammon, pour lui dire: Qu'y a-t-il entre moi et toi, que tu sois venu contre moi pour faire la guerre dans mon pays?
Ndipo Yeftha akatuma wajumbe kwa mfalme wa wana wa Amoni, akisema, “Ni nini mgogoro huu kati yetu? Kwa nini umekuja kwa nguvu kuchukua ardhi yetu?”
13 Et le roi des enfants d'Ammon répondit aux messagers de Jephthé: C'est parce qu'Israël, quand il montait d'Égypte, a pris mon pays depuis l'Arnon jusqu'au Jabbok et au Jourdain. Rends-le maintenant de bon gré.
Mfalme wa wana wa Amoni akawajibu wajumbe wa Yeftha, “Kwa sababu Israeli walipopanda kutoka Misri, walichukua nchi yangu toka Arnoni hata Yaboki, mpaka Yordani. Sasa rudisha ardhi hizo kwa amani.”
14 Mais Jephthé envoya de nouveau au roi des enfants d'Ammon,
Yefta akatuma tena wajumbe kwa mfalme wa wana wa Amoni,
15 Des messagers qui lui dirent: Ainsi a dit Jephthé: Israël n'a rien pris du pays de Moab, ni du pays des enfants d'Ammon.
akasema, “Yefita asema hivi, Israeli hawakuchukua nchi ya Moabu na nchi ya wana wa Amoni;
16 Mais lorsque Israël monta d'Égypte, il marcha par le désert jusqu'à la mer Rouge, et arriva à Kadès,
lakini walitoka Misri, na Israeli wakaenda kupitia jangwa hadi Bahari ya Shamu na Kadeshi.
17 Et envoya des députés au roi d'Édom, pour lui dire: Laisse-moi passer par ton pays. Mais le roi d'Édom n'y consentit pas. Et il en envoya de même au roi de Moab, qui refusa, et Israël resta à Kadès.
Israeli walipomtuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu, wakisema, 'Tafadhali tunaomba ruhusa tupite katika nchi yako,' mfalme wa Edomu hakuwasikiliza. Wakawatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu, lakini akakataa. Basi Israeli wakakaa Kadeshi.
18 Puis il marcha par le désert, et fit le tour du pays d'Édom et du pays de Moab, et arriva au pays de Moab, du côté de l'orient. Il campa au delà de l'Arnon, sans entrer sur le territoire de Moab; car l'Arnon était la frontière de Moab.
Kisha wakapitia jangwani, wakaondoka katika nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu; wakavuka upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga ng'ambo ya Arnoni. Lakini hawakuingia mpaka wa Moabu, maana Arnoni ilikuwa mpaka wa Moabu.
19 Mais Israël envoya des messagers à Sihon, roi des Amoréens, roi de Hesbon, et Israël lui fit dire: Laisse-nous passer par ton pays, jusqu'à notre destination.
Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni; Israeli akamwambia, 'Tafadhali, tunaomba tupite katika nchi yako hata mahali petu.'
20 Mais Sihon, ne se fiant point à Israël, pour le laisser passer par son pays, rassembla tout son peuple; ils campèrent vers Jahats, et combattirent contre Israël.
Lakini Sihoni hakumwamini Israeli apite katika eneo lake. Basi Sihoni akakusanya jeshi lake lote, akalipeleka Yahasa, na huko akapigana na Israeli
21 Et l'Éternel, le Dieu d'Israël, livra Sihon et tout son peuple entre les mains d'Israël; et Israël le défit, et conquit tout le pays des Amoréens, qui habitaient ce pays-là.
Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mkononi mwa Israeli, nao wakawashinda. Basi Israeli wakachukua nchi yote ya Waamori waliokaa katika nchi hiyo.
22 Ils conquirent donc tout le pays des Amoréens, depuis l'Arnon jusqu'au Jabbok, et depuis le désert jusqu'au Jourdain.
Wachukua kila kitu ndani ya wilaya ya Waamori, kutoka Arnoni hadi Yaboki, na kutoka jangwani hadi Yordani.
23 Et maintenant que l'Éternel, le Dieu d'Israël, a chassé les Amoréens devant son peuple d'Israël, est-ce toi qui aurais la possession de leur pays?
Basi, Bwana, Mungu wa Israeli, amewafukuza Waamori mbele ya watu wake Israeli, na sasa mnataka kuimiliki nchi yao?
24 N'aurais-tu pas la possession de ce que ton dieu Kémosh t'aurait donné à posséder? Ainsi nous posséderons le pays de tous ceux que l'Éternel notre Dieu aura chassés devant nous.
Je, huwezi kuchukua nchi ambayo Kemoshi, mungu wako, anakupa? Kwa hiyo nchi yoyote Bwana, Mungu wetu, ametupa, tutachukua.
25 Au reste, vaux-tu mieux que Balak, fils de Tsippor, roi de Moab? A-t-il contesté et combattu contre Israël?
Sasa wewe ni bora zaidi kuliko Balaki, mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu? Je, alidai kuwa na hoja na Israeli? Je, yeye amewahi kupigana vita dhidi yao?
26 Voilà trois cents ans qu'Israël habite Hesbon et les villes de son ressort, et Aroër et les villes de son ressort, et toutes les villes qui sont le long de l'Arnon; pourquoi ne les lui avez-vous pas enlevées pendant ce temps-là?
Wakati Israeli walipoishia miaka mia tatu huko Heshboni na vijiji vyake, na Aroeri na vijiji vyake, na katika miji yote iliyo karibu na Arnoni, kwa nini hamkuwachukua tena wakati huo?
27 Je ne t'ai point offensé, mais tu agis mal avec moi, en me faisant la guerre. Que l'Éternel, le juge, soit aujourd'hui juge entre les enfants d'Israël et les enfants d'Ammon!
Sijawafanyia vibaya, lakini mnanifanyia vibaya kwa kunishambulia. Bwana, mwamuzi, ataamua leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni.
28 Mais le roi des enfants d'Ammon ne voulut point écouter les paroles que Jephthé lui avait fait dire.
Lakini mfalme wa wana wa Amoni akakataa onyo alilotumiwa na Yeftha.
29 Alors l'Esprit de l'Éternel fut sur Jephthé, qui traversa Galaad et Manassé; il passa jusqu'à Mitspa de Galaad, et de Mitspa de Galaad il marcha contre les enfants d'Ammon.
Basi, Roho wa Bwana akamjia Yeftha, akapita Gileadi na Manase, akapitia Mizpa ya Gileadi, na kutoka Mispa ya Gileadi akapita kwa wana wa Amoni.
30 Et Jephthé fit un vœu à l'Éternel, et dit: Si tu livres les enfants d'Ammon entre mes mains,
Yeftha akaahidi kwa Bwana, akasema, “Ikiwa utanipa ushindi juu ya wana wa Amoni,
31 Ce qui sortira au-devant de moi des portes de ma maison, quand je retournerai en paix de chez les enfants d'Ammon, sera à l'Éternel, et je l'offrirai en holocauste.
chochote kinachotoka mlangoni mwa nyumba yangu kunijia mimi nitakaporudi kwa amani kutoka kwa wana wa Amoni kitakuwa cha Bwana; Nami nitatoa hiyo sadaka ya kuteketezwa.”
32 Puis Jephthé marcha contre les enfants d'Ammon, pour leur faire la guerre, et l'Éternel les livra entre ses mains.
Basi Yeftha akapita kwa wana wa Amoni ili kupigana nao, naye Bwana akampa ushindi.
33 Et il les battit depuis Aroër jusqu'à Minnith, espace qui renfermait vingt villes, et jusqu'à Abel-Keramim (la plaine des vignes); et les enfants d'Ammon furent abaissés devant les enfants d'Israël.
Akawashinda na kusababisha mauaji makubwa kutoka Aroeri hadi miji ishirini na miwili-na Abeli ​​Keramimu. Basi wana wa Amoni waliwekwa chini ya uangalizi wa watu wa Israeli.
34 Et comme Jephthé venait à Mitspa, en sa maison, voici, sa fille sortit au-devant de lui avec des tambourins et des danses. Elle était son seul et unique enfant, sans qu'il eût d'autre fils, ni fille.
Yeftha alifika nyumbani kwake huko Mizpa, na binti yake akatoka kumlaki na ngoma na kucheza. Alikuwa mtoto wake pekee, na badala yake hakuwa na mwana wa kiume wala binti.
35 Et sitôt qu'il l'eut aperçue, il déchira ses vêtements, et dit: Ah! ma fille! tu m'accables, tu m'accables! Et tu es du nombre de ceux qui me troublent! Car j'ai fait un vœu à l'Éternel, et je ne puis le révoquer.
Mara tu alipopomwona, alirarua nguo zake akasema, 'Loo! Binti yangu! Umenivunja kwa huzuni, na umekuwa mtu anayenisababishia maumivu yangu! Kwa maana nimeapa kwa Bwana, wala siwezi kurudisha ahadi yangu.
36 Et elle lui répondit: Mon père, as-tu fait un vœu à l'Éternel? Fais-moi selon ce qui est sorti de ta bouche, puisque l'Éternel t'a vengé de tes ennemis, les enfants d'Ammon.
Akamwambia, “Baba yangu, umeweka ahadi kwa Bwana, unifanyie kila kitu ulichoahidi; kwa kuwa Bwana amekulipia kisasi juu ya adui zako, wana wa Amoni.”
37 Puis elle dit à son père: Accorde-moi ceci; laisse-moi pendant deux mois; je m'en irai, je descendrai par les montagnes, et je pleurerai ma virginité, moi et mes compagnes.
Akamwambia baba yake, “Hebu ahadi hii ihifadhiwe kwa ajili yangu. Niache kwa miezi miwili, nipate kuondoka na kwenda kwenye vilima na kuomboleza juu ya ubikira wangu, mimi na wenzangu.”
38 Et il dit: Va! Et il la laissa aller pour deux mois. Elle s'en alla donc avec ses compagnes, et pleura sa virginité sur les montagnes.
Akasema, “Nenda.” Alimtuma kwa muda wa miezi miwili. Akamwondoa, yeye na wenzake, nao wakauomboleza ubikira wake katika milimani.
39 Et, au bout de deux mois, elle revint vers son père, et il accomplit sur elle le vœu qu'il avait fait, et elle ne connut point d'homme.
Mwishoni mwa miezi miwili alirudi kwa baba yake, ambaye alifanya kulingana na ahadi ya aliyoifanya. Sasa alikuwa hajalala na mwanaume, na ikawa desturi katika Israeli
40 De là vint la coutume en Israël, qu'annuellement les filles d'Israël vont célébrer la fille de Jephthé, le Galaadite, pendant quatre jours chaque année.
kwamba binti za Israeli kila mwaka, kwa siku nne, waweze kurejea hadithi ya binti ya Yeftha Mgileadi.

< Juges 11 >