< Josué 4 >

1 Et quand toute la nation eut achevé de passer le Jourdain, l'Éternel parla à Josué, et lui dit:
Watu wote walipokwisha kuvuka Yordani, Yahweh akamwambia Yoshua,
2 Prenez parmi le peuple douze hommes, un homme par tribu,
“Chagueni wenyewe watu waume kumi na wawili, mmoja katika kila kabila.
3 Et commandez-leur en disant: Prenez d'ici, du milieu du Jourdain, du lieu où les sacrificateurs se sont arrêtés de pied ferme, douze pierres que vous emporterez avec vous et que vous poserez au lieu où vous passerez cette nuit.
Wape agizo hilo: 'Chukueni mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani mahali wanaposimama makuhani katika nchi kavu, na wayalete na kuyaweka chini katika sehemu ambapo mtalala usiku wa leo.
4 Josué appela donc les douze hommes qu'il avait choisis d'entre les enfants d'Israël, un homme par tribu,
Kisha Yoshua akawaita wanaume kumi na wawili ambao aliwachagua kutoka katika makabila ya Israeli, mmoja kutoka kila kabila.
5 Et Josué leur dit: Passez devant l'arche de l'Éternel votre Dieu, au milieu du Jourdain, et que chacun de vous prenne une pierre sur son épaule, selon le nombre des tribus des enfants d'Israël;
Yoshua akawaambia, “Nendeni mbele za sanduku la Yahweh Mungu wenu katikati ya Yordani. Kila mmoja wenu achukue jiwe moja mabegani mwake, kulingana na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli.
6 Afin que cela soit un signe au milieu de vous. Quand dans l'avenir vos enfants demanderont: Que veulent dire pour vous ces pierres?
Hii itakuwa ni ishara miongoni mwenu kwa ajili yenu wakati watoto wenu watakapowauliza katika siku zijazo, 'Nini maana ya mawe haya kwenu?'
7 Vous leur répondrez: C'est que les eaux du Jourdain furent coupées devant l'arche de l'alliance de l'Éternel, quand elle passa le Jourdain; les eaux du Jourdain furent coupées; et ces pierres sont pour les enfants d'Israël un mémorial à jamais.
Ndipo mtakapowaambia, 'Maji ya Yordani yalitengwa mbele ya sanduku la Yahweh. Lililpopitishwa katika Yordani, maji ya Yordani yalisimamishwa. Hivyo, mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.'”
8 Les enfants d'Israël firent donc ce que Josué avait commandé. Ils prirent douze pierres du milieu du Jourdain, comme l'Éternel l'avait dit à Josué, selon le nombre des tribus des enfants d'Israël, et les emportèrent avec eux au lieu où ils passèrent la nuit, et ils les y posèrent.
Watu waisraeli walifanya kama Yoshua alivyowaagiza, na walichukua mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani, kama Yahweh alivyomwambia Yoshua, walipangwa sawa sawa na hesabu ya makabila ya watu wa Israeli. Waliyachukua mawe mpaka mahali walipolala na wakayaweka chini huko.
9 Josué dressa aussi douze pierres au milieu du Jourdain, au lieu où s'étaient arrêtés les pieds des sacrificateurs qui portaient l'arche de l'alliance, et elles sont là jusqu'à ce jour.
Kisha Yoshua akayapanga mawe kumi na mbili katikati ya Yordani, katika sehemu ambapo ilisimama miguu ya makuhani waliolichukua sanduku la agano. Na kumbukumbu hiyo ipo hadi leo.
10 Et les sacrificateurs qui portaient l'arche se tinrent au milieu du Jourdain, jusqu'à ce que tout ce que l'Éternel avait commandé à Josué de dire au peuple fût achevé, selon tout ce que Moïse avait prescrit à Josué. Puis le peuple se hâta de passer.
Makuhani waliolichukua sanduku walisimama katikati ya Yordani mpaka pale kila kitu ambacho Yahweh alimwamuru Yoshua kuwaambia watu kilipokamilika, sawa sawa na yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua. Watu walifanya haraka na wakavuka.
11 Quand tout le peuple eut achevé de passer, l'arche de l'Éternel et les sacrificateurs passèrent devant le peuple.
Wakati watu wote walipokwisha kuvuka, sanduku la Yahweh pamoja na makuhani walivuka mbele za watu.
12 Alors les enfants de Ruben, les enfants de Gad, et la demi-tribu de Manassé passèrent en armes devant les enfants d'Israël, comme Moïse le leur avait dit;
Kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase walipita kama jeshi mbele ya watu wa Israeli, kama ambavyo Musa alivyowaambia.
13 Environ quarante mille hommes, équipés pour la guerre, passèrent devant l'Éternel pour combattre, dans les campagnes de Jérico.
Yapata watu watu elfu arobaini walioandaliwa kwa vita walipita mbele za Yahweh, kwa ajili ya vita katika uwanda wa Yeriko.
14 En ce jour-là, l'Éternel éleva Josué à la vue de tout Israël, et ils le craignirent comme ils avaient craint Moïse, tous les jours de sa vie.
Katika siku hiyo Yahweh alimfanya Yoshua kuwa mkuu katika macho ya watu wote wa Israeli. Walimheshimu - kama walivyomheshimu Musa - siku zake zote.
15 Or l'Éternel parla à Josué, en disant:
Kisha Yahweh akamwambia Yoshua,
16 Commande aux sacrificateurs qui portent l'arche du Témoignage, et qu'ils montent hors du Jourdain.
“Waamuru makuhani wanaolibeba sanduku la ushuhuda watoke katika Yordani.”
17 Et Josué commanda aux sacrificateurs, en disant: Montez hors du Jourdain.
Hivyo Yoshua akawaamuru makuhani, '' pandeni mtoke Yordani.”
18 Et lorsque les sacrificateurs qui portaient l'arche de l'alliance de l'Éternel furent montés du milieu du Jourdain, et que la plante des pieds des sacrificateurs se leva pour se poser sur le sec, les eaux du Jourdain retournèrent à leur place, et coulèrent comme auparavant par-dessus toutes ses rives.
Wakati makuhani wenye kulibeba sanduku la agano la Yahweh walitoka katikati ya Yordani, na nyayo za miguu yao ilikuwa imeinuliwa katika nchi kavu, kisha maji ya Yordani yalirudi katika sehemu zake na kujaa hadi katika kingo zake kama ilivyokuwa siku nne zilizopita.
19 Le peuple monta ainsi hors du Jourdain, le dixième jour du premier mois, et il campa à Guilgal, du côté de l'Orient de Jérico.
Katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, watu walikwea kutoka Yordani. Wakakaa huko Gilgali, mashariki mwa Yeriko.
20 Et Josué dressa à Guilgal les douze pierres qu'ils avaient prises du Jourdain.
Mawe kumi na mawili ambayo yalichukuliwa katika Yordani, Yoshuua aliyasimamisha hapo Gilgali.
21 Et il parla aux enfants d'Israël, en disant: Quand à l'avenir vos enfants interrogeront leurs pères, et diront: Que veulent dire ces pierres?
Aliwaambia watu wa Israeli, “wakati watoto wenu watakapowauliza baba zao katika wakai ujao, 'Mawe haya ni ya nini?'
22 Vous l'apprendrez à vos enfants, en disant: Israël a passé ce Jourdain à sec.
Waambieni watoto wenu, 'Hapa ndipo Waisraeli walivuka Yordani katika nchi kavu.
23 Car l'Éternel votre Dieu a mis à sec les eaux du Jourdain devant vous, jusqu'à ce que vous fussiez passés, comme l'Éternel votre Dieu avait fait à la mer Rouge qu'il mit à sec devant nous, jusqu'à ce que nous fussions passés;
Yahweh Mungu wenu aliyakausha maji ya Yordani, mpaka hapo Yahweh Mungu wako aliyoyafanya katika bahari ya mianzi, ambayo aliikausha kwa ajili yetu ili tupite juu yakes,
24 Afin que tous les peuples de la terre sachent que la main de l'Éternel est forte, et afin que vous craigniez toujours l'Éternel votre Dieu.
ili kwamba watu wote wa nchi wajue kwamba mkono wa Yahweh ni nguvu, na kwamba mtamweshimu Yahweh Mungu wenu milele.''

< Josué 4 >