< Josué 15 >

1 La part échue par le sort à la tribu des enfants de Juda, selon leurs familles, fut à la frontière d'Édom, au désert de Tsin, vers le midi, à l'extrémité méridionale.
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
2 Leur frontière méridionale partait de l'extrémité de la mer Salée, depuis le bras qui regarde vers le midi;
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
3 Et elle sortait au midi de la montée d'Akrabbim, passait vers Tsin, montait au midi de Kadès-Barnéa, passait à Hetsron, montait vers Addar, tournait vers Karkaa,
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
4 Passait vers Atsmon, sortait au torrent d'Égypte; et la frontière aboutissait à la mer. Ce sera là, dit Josué, votre frontière du côté du midi.
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
5 Et la frontière vers l'orient était la mer Salée, jusqu'à l'embouchure du Jourdain; et la frontière de la région du nord partait du bras de mer qui est à l'embouchure du Jourdain.
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
6 Et la frontière montait à Beth-Hogla, et passait au nord de Beth-Araba. Et la frontière montait à la pierre de Bohan, fils de Ruben.
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
7 Puis la frontière montait vers Débir, du côté de la vallée d'Acor, et vers le nord, se dirigeant vers Guilgal, qui est vis-à-vis de la montée d'Adummim, au midi du torrent; la frontière passait ensuite près des eaux d'En-Shémèsh et aboutissait à En-Roguel.
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
8 De là la frontière montait par la vallée du fils de Hinnom, vers le côté méridional de Jébus, qui est Jérusalem. Ensuite la frontière s'élevait au sommet de la montagne qui est en face de la vallée de Hinnom, vers l'occident, et à l'extrémité de la vallée des Réphaïm, au nord.
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
9 Cette frontière s'étendait du sommet de la montagne vers la source des eaux de Nephthoach, et sortait vers les villes de la montagne d'Éphron; puis la frontière s'étendait à Baala, qui est Kirjath-Jéarim.
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
10 La frontière tournait ensuite de Baala à l'occident vers la montagne de Séir, et passait, vers le nord, à côté de la montagne de Jéarim qui est Késalon; puis elle descendait à Beth-Shémesh, et passait à Thimna.
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
11 De là la frontière sortait du côté septentrional d'Ékron. Puis cette frontière s'étendait vers Shikron, passait par la montagne de Baala, et sortait à Jabnéel; et la frontière aboutissait à la mer.
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
12 Or, la frontière de l'occident était la grande mer et la côte. Telle fut, de tous les côtés, la frontière des enfants de Juda, selon leurs familles.
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
13 On donna à Caleb, fils de Jephunné, une portion au milieu des enfants de Juda, selon le commandement de l'Éternel à Josué: savoir la cité d'Arba, père d'Anak. C'est Hébron.
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
14 Et Caleb en déposséda les trois fils d'Anak: Shéshaï, Ahiman et Thalmaï, enfants d'Anak.
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
15 De là il monta vers les habitants de Débir; et le nom de Débir était autrefois Kirjath-Sépher.
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
16 Et Caleb dit: Je donnerai ma fille Acsa pour femme à celui qui battra Kirjath-Sépher, et la prendra.
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
17 Alors Othniel, fils de Kénaz, frère de Caleb, la prit; et il lui donna pour femme sa fille Acsa.
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
18 Or il arriva qu'à son entrée chez Othniel, elle l'incita à demander un champ à son père. Et elle se jeta de dessus son âne, et Caleb lui dit: Qu'as-tu?
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
19 Et elle répondit: Donne-moi un présent; puisque tu m'as donné une terre du midi, donne-moi aussi des sources d'eaux. Et il lui donna les sources supérieures et les sources inférieures.
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
20 Tel fut l'héritage de la tribu des enfants de Juda, selon leurs familles.
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
21 Les villes à l'extrémité de la tribu des enfants de Juda, vers la frontière d'Édom, au midi, furent Kabtséel, Éder, Jagur,
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
22 Kina, Dimona, Adéada,
Kina, Dimona, Adada,
23 Kédès, Hatsor, Jithnan,
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
24 Ziph, Télem, Béaloth,
Zifu, Telemu, Bealothi.
25 Hatsor-Hadattha, Kérijoth-Hetsron, qui est Hatsor,
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
26 Amam, Shéma, Molada,
Amamu, shema, Molada,
27 Hatsar-gadda, Heshmon, Beth-Palet,
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
28 Hatsar-Shual, Béer-Shéba, Bizjothja,
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
29 Baala, Ijjim, Atsem,
Baala, Limu, Ezemu,
30 Eltholad, Késil, Horma,
Eltoladi, Kesili, Horma,
31 Tsiklag, Madmanna, Sansanna,
Ziklagi, Madimana, Sansana,
32 Lébaoth, Shilhim, Aïn, et Rimmon; en tout vingt-neuf villes et leurs villages.
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
33 Dans la plaine, Eshthaol, Tsoréa, Ashna,
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
34 Zanoach, En-Gannim, Thappuach, Énam,
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
35 Jarmuth, Adullam, Soco, Azéka,
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
36 Shaaraïm, Adithaïm, Guédéra, et Guédérothaïm, quatorze villes et leurs villages;
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
37 Tsénan, Hadasha, Migdal-Gad,
Zena, Hadasha, Migidagadi,
38 Dilan, Mitspé, Jokthéel,
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
39 Lakis, Botskath, Églon,
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
40 Cabbon, Lachmas, Kithlish,
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
41 Guédéroth, Beth-Dagon, Naama, et Makkéda; seize villes et leurs villages;
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
42 Libna, Éther, Ashan,
Libna, Etheri, Ashani,
43 Jiphtach, Ashna, Netsib,
Ifuta, Ashina, Nezibu,
44 Keïla, Aczib et Marésha; neuf villes et leurs villages;
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
45 Ékron, les villes de son ressort, et ses villages;
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
46 Depuis Ékron, et à l'occident, toutes celles qui sont dans le voisinage d'Asdod, et leurs villages;
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Asdod, les villes de son ressort, et ses villages; Gaza, les villes de son ressort, et ses villages, jusqu'au torrent d'Égypte, et à la grande mer et son rivage.
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
48 Et dans la montagne, Shamir, Jatthir, Soco,
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
49 Danna, Kirjath-Sanna, qui est Débir,
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
50 Anab, Eshthemo, Anim,
Anabu, Eshitemo, Animu,
51 Gossen, Holon, et Guilo; onze villes et leurs villages;
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
52 Arab, Duma, Eshéan,
Arabu, Duma, Ehani,
53 Janum, Beth-Thappuach, Aphéka,
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
54 Humta, Kirjath-Arba, qui est Hébron, et Tsior; neuf villes et leurs villages;
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
55 Maon, Carmel, Ziph, Juta,
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
56 Jizréel, Jokdéam, Zanoach,
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
57 Kaïn, Guibéa, et Thimna; dix villes et leurs villages;
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
58 Halhul, Beth-Tsur, Guédor,
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
59 Maarath, Beth-Anoth, et Elthekon; six villes et leurs villages;
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Kirjath-Baal, qui est Kirjath-Jéarim, et Rabba; deux villes et leurs villages;
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
61 Dans le désert, Beth-Araba, Middin, Secaca,
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
62 Nibshan, et Ir-Hammélach (la ville du sel), et En-Guédi; six villes et leurs villages.
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
63 Or les enfants de Juda ne purent déposséder les Jébusiens qui habitaient à Jérusalem, et les Jébusiens ont habité avec les enfants de Juda à Jérusalem jusqu'à ce jour.
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.

< Josué 15 >