< Job 6 >

1 Et Job prit la parole, et dit:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oh! si l'on pesait ma douleur, et si l'on mettait en même temps mes calamités dans la balance!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 Elles seraient plus pesantes que le sable des mers! Voilà pourquoi mes paroles sont outrées.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Car les flèches du Tout-Puissant sont sur moi: mon âme en boit le venin. Les terreurs de Dieu se rangent en bataille contre moi.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 L'onagre brait-il auprès de l'herbe? Et le bœuf mugit-il auprès de son fourrage?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Mange-t-on sans sel ce qui est fade? Trouve-t-on du goût dans un blanc d'œuf?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 Ce que mon âme refusait de toucher, est comme devenu ma dégoûtante nourriture.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 Oh! puisse mon vœu s'accomplir et Dieu me donner ce que j'attends!
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 Qu'il plaise à Dieu de me réduire en poussière, qu'il laisse aller sa main pour m'achever!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Et j'aurai une consolation, et j'aurai des transports de joie au milieu des tourments qu'il ne m'épargne pas: c'est que je n'ai pas renié les paroles du Saint.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 Quelle est ma force pour que j'espère, et quelle est ma fin pour que je prenne patience?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Ma force est-elle la force des pierres? Ma chair est-elle d'airain?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 Ne suis-je pas sans secours, et toute ressource ne m'est-elle pas ôtée?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 Le malheureux a droit à la pitié de son ami, eût-il abandonné la crainte du Tout-Puissant.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 Mes amis m'ont trompé comme un torrent, comme le lit des torrents qui passent;
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 Ils sont troublés par les glaçons, la neige s'y engloutit;
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 Mais, au temps de la sécheresse, ils tarissent, et, dans les chaleurs, ils disparaissent de leur place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 Les caravanes se détournent de leur route; elles montent dans le désert et se perdent.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 Les caravanes de Théma y comptaient; les voyageurs de Shéba s'y attendaient.
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 Ils sont honteux d'avoir eu cette confiance: ils arrivent sur les lieux, et restent confondus.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 C'est ainsi que vous me manquez à présent; vous voyez une chose terrible, et vous en avez horreur!
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Mais vous ai-je dit: “Donnez-moi quelque chose, et, de vos biens, faites des présents en ma faveur;
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 Délivrez-moi de la main de l'ennemi, et rachetez-moi de la main des violents? “
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Instruisez-moi, et je me tairai. Faites-moi comprendre en quoi j'ai erré.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 Oh! que les paroles droites ont de force! Mais que veut censurer votre censure?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Sont-ce des mots que vous voulez censurer? Mais il faut laisser au vent les paroles d'un homme au désespoir.
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Vraiment, vous joueriez au sort un orphelin, et vous vendriez votre ami!
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Mais, à présent, veuillez jeter les yeux sur moi, et voyez si je vous mens en face!
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Revenez donc, et soyez sans injustice! Revenez, et que mon bon droit paraisse!
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Y a-t-il de l'injustice dans ma langue? Et mon palais ne sait-il pas discerner le mal?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

< Job 6 >