< Job 5 >

1 Crie maintenant! Y aura-t-il quelqu'un qui te réponde? Et vers lequel des saints te tourneras-tu?
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 La colère tue l'insensé, et le dépit fait mourir celui qui est destitué de sens;
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 J'ai vu l'insensé étendant ses racines, mais soudain j'ai maudit sa demeure.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 Ses fils sont loin de tout secours, ils sont écrasés à la porte, et personne ne les délivre;
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 L'affamé dévore sa moisson; il la lui prend à travers les épines de sa haie; l'homme altéré convoite ses biens.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 Car la souffrance ne sort pas de la poussière, et la peine ne germe pas du sol,
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 De sorte que l'homme soit né pour la peine, comme l'étincelle pour voler en haut.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 Mais moi, j'aurais recours à Dieu, et j'adresserais ma parole à Dieu,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 Qui fait de grandes choses qu'on ne peut sonder, de merveilleuses choses qu'on ne peut compter;
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 Qui répand la pluie sur la face de la terre, et qui envoie les eaux sur la face des champs;
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 Qui met en haut ceux qui sont abaissés, et ceux qui sont en deuil au faîte du bonheur;
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 Qui dissipe les projets des hommes rusés, et leurs mains ne viennent à bout de rien;
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 Qui prend les sages dans leurs propres ruses, et le dessein des pervers est renversé.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 De jour, ils rencontrent les ténèbres, et, comme dans la nuit, ils tâtonnent en plein midi;
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 Et il délivre le pauvre de l'épée de leur bouche, et de la main des puissants.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 Et il y a une espérance pour les malheureux, et la méchanceté a la bouche fermée.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 Voici, heureux l'homme que Dieu châtie! Ne méprise donc pas la correction du Tout-Puissant.
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 Car c'est lui qui fait la plaie et la bande; il blesse et ses mains guérissent.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 Dans six détresses, il te délivrera; et dans sept, le mal ne te touchera point.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 En temps de famine, il te garantira de la mort, et en temps de guerre, du tranchant de l'épée.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 Tu seras à couvert du fléau de la langue, et tu n'auras point peur de la désolation, quand elle arrivera.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 Tu riras de la dévastation et de la famine, et tu n'auras pas peur des bêtes de la terre;
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 Car tu auras un pacte avec les pierres des champs, et les bêtes des champs seront en paix avec toi.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 Et tu verras la prospérité dans ta tente: tu visiteras tes pâturages,
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 Et rien ne t'y manquera; et tu verras ta postérité croissante, et tes descendants pareils à l'herbe de la terre.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 Tu entreras mûr dans le tombeau, comme une gerbe qu'on emporte en son temps.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Voilà, nous avons examiné la chose; elle est ainsi, écoute cela, et fais-en ton profit.
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< Job 5 >