< Job 42 >

1 Alors Job répondit à l'Éternel, et dit:
Kisha Ayubu akamjibu Yahweh na kusema,
2 Je sais que tu peux tout, et qu'on ne saurait t'empêcher d'accomplir un dessein.
“Ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote, ya kuwa hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa.
3 “Qui obscurcit mes plans sans science? “J'ai parlé et je ne comprenais pas; ce sont des choses trop merveilleuses pour moi, et je ne les connais point.
Ni nani huyo ambaye pasipo maarifa huificha mipango? Kwa kweli nilisema mambo ambayo sikuyaelewa, mambo magumu kwangu kuyafahamu, ambayo juu yake sikujua chochote.
4 “Écoute donc et je parlerai; je t'interrogerai et tu m'instruiras. “
Uliniambia, 'Sikiliza sasa, nami nitasema; nitakuuliza mambo, nawe utaniambia.'
5 Mes oreilles avaient entendu parler de toi; mais, maintenant, mon œil t'a vu.
Nimekuwa nikikusikia kwa usikivu wa sikio langu, lakini sasa jicho langu linakuona wewe.
6 C'est pourquoi je me condamne et je me repens, sur la poussière et sur la cendre.
Basi ninajidharau mwenyewe; ninatubu kwa mavumbi na majivu.”
7 Or, après que l'Éternel eut ainsi parlé à Job, il dit à Éliphaz, de Théman: Ma colère est enflammée contre toi et contre tes deux amis, parce que vous n'avez pas parlé avec droiture devant moi, comme Job, mon serviteur.
Ilitokea baada ya kuwa amekwisha kusema maneno hata kwa Ayubu, Yahweh alimwambia Elifazi Mtemani, “Ghadhabu yangu imewaka dhidi yako na dhidi ya marafiki zako wawili kwa kuwa hamkusema maneno ya haki juu yangu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.
8 Maintenant, prenez sept taureaux et sept béliers, et allez vers mon serviteur Job, offrez un holocauste pour vous, et Job, mon serviteur, priera pour vous; et par égard pour lui, je ne vous traiterai pas selon votre folie, car vous n'avez pas parlé avec droiture devant moi, comme mon serviteur Job.
Sasa basi, jitwalieni mafahari saba na mabeberu saba, kisha mmwendee mtumishi wangu Ayubu na mtoe sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Ndipo Mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi, nami nitayapokea maombi yake, ili kwamba nisiwashughulikie sawasawa na upumbavu wenu. Maana hamkusema mambo ya haki juu yangu, kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”
9 Et Éliphaz, de Théman, Bildad, de Shuach, et Tsophar, de Naama, allèrent et firent comme leur avait dit l'Éternel, et l'Éternel eut égard à Job.
Basi Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi na Zofari Mnaamathi walienda na kufanya kama vile Yahweh alivyowaamuru, na Mungu alimtakabali Ayubu.
10 Et l'Éternel rétablit Job dans ses biens, quand il eut prié pour ses amis; et il lui rendit au double tout ce qu'il avait eu.
Na wakati Ayubu alimpowaombea rafiki zake, Yahweh alirejeza bahati yake. Yahweh alimjalia mara mbili ya kile alichokimiliki hapo awali.
11 Tous ses frères, et toutes ses sœurs, tous ceux qui l'avaient connu auparavant vinrent vers lui, et mangèrent avec lui dans sa maison. Ils lui firent leurs condoléances, et le consolèrent au sujet de tout le mal que l'Éternel avait fait venir sur lui, et chacun lui donna une késita et un anneau d'or.
Ndipo ndugu zake na Ayubu, na wale jamaa zake wote walikuwa wanajuana naye hapo mwanzo, walikuja hapo kwake na kula chakula pamoja naye katika nyumba yake. Waliomboleza pamoja naye na walimfariji kwa ajili majanga yote ambayo Yahweh alikuwa ameyaleta juu yake. Kila mtu alimpa Ayubu kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 Ainsi l'Éternel bénit le dernier état de Job plus que le premier; il eut quatorze mille brebis, six mille chameaux, et mille couples de bœufs, et mille ânesses.
Yahweh aliubarikiwa mwisho wa maisha ya Ayubu kuliko mwanzo wake; alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, ngamia elfu sita, jozi elfu moja, na punda jike elfu moja.
13 Il eut sept fils et trois filles.
Pia alikuwa na wana saba na mabinti watatu.
14 Il donna à la première le nom de Jémima (colombe), à la seconde celui de Ketsia (parfum), à la troisième celui de Kéren-Happuc (flacon de fard).
Binti wa kwanza alimwita Yemima, na wa pili Kezia, na wa tatu Kerenihapuki.
15 Et il ne se trouvait pas de femmes aussi belles que les filles de Job dans tout le pays; et leur père leur donna un héritage avec leurs frères.
Katika nchi yote hawakupatikana wanawake wazuri kama mabinti wa Ayubu. Baba yao aliwapa urithi miongoni mwa kaka zao.
16 Job vécut, après ces choses, cent quarante ans, et vit ses fils et les fils de ses fils jusqu'à la quatrième génération.
Baada ya haya, Ayubu aliishi miaka 140; aliwaona wana wake na wana wa wanawe, hata kizazi cha nne.
17 Et il mourut âgé et rassasié de jours.
Basi Ayubu alifariki, akiwa mzee na akijawa na siku nyingi.

< Job 42 >