< Job 36 >

1 Élihu continua, et dit:
Elihu akaendelea kusema:
2 Attends un peu et je t'instruirai, car il y a encore des raisons pour la cause de Dieu.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Je prendrai de loin ma science, et je donnerai droit à mon créateur.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Car, certainement, mes discours ne sont point mensongers, et c'est un homme qui te parle d'une science parfaite.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Voici, Dieu est puissant, et il ne dédaigne personne; il est puissant par la force de son intelligence.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Il ne laisse point vivre le méchant, et il fait droit aux affligés.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Il ne détourne pas ses yeux des justes, il place ces justes avec les rois sur le trône; et il les y fait asseoir pour toujours, et ils sont élevés.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 S'ils sont liés de chaînes, s'ils sont pris dans les liens de l'affliction,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Il leur fait connaître ce qu'ils ont fait, leurs péchés et leur orgueil.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Alors il ouvre leur oreille à la réprimande; il leur dit de se détourner de l'iniquité.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 S'ils l'écoutent, et s'ils le servent, ils achèvent leurs jours dans le bonheur, et leurs années dans la joie;
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Mais s'ils ne l'écoutent pas, ils passent par l'épée, et ils expirent dans leur aveuglement.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Les cœurs impies se mettent en colère; ils ne crient point à lui quand il les a liés.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Leur âme meurt en sa jeunesse, et leur vie s'éteint comme celle des débauchés.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Il sauve l'affligé par son affliction, et il l'instruit par sa douleur.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Et toi-même, il te mettra hors de ta détresse, au large, loin de toute angoisse, et ta table sera dressée, couverte de graisse.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Mais si tu es plein de la cause du méchant, cette cause et la condamnation se suivront de près.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Prends garde que la colère ne te pousse au blasphème, et ne te laisse pas égarer par la pensée d'une abondante expiation.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Ferait-il cas de ta richesse? Il n'estimera ni l'or ni les moyens de l'opulence.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Ne souhaite point la nuit, en laquelle les peuples sont enlevés sur place.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Garde-toi de te tourner vers l'iniquité; car tu la préfères à l'affliction.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Voici, Dieu est élevé en sa puissance; qui pourrait enseigner comme lui?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Qui lui a prescrit sa voie? Et qui lui dira: Tu as fait une injustice?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Souviens-toi de célébrer ses ouvrages, que tous les hommes chantent.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Tout homme les admire, chacun les contemple de loin.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Voici, Dieu est élevé, et nous ne le connaissons pas; le nombre de ses années, nul ne peut le sonder!
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Il attire les gouttes d'eau, elles se fondent en pluie, au milieu du brouillard;
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Les nuées la font couler, et tomber goutte à goutte sur la foule des hommes.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Et qui pourrait comprendre le déploiement des nuées, et le fracas de sa tente?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Voici, il étend sur lui-même la lumière, et il couvre le profond des mers.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 C'est ainsi qu'il juge les peuples, et qu'il donne la nourriture en abondance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Il tient cachée dans sa main la lumière, et il lui prescrit de frapper.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Son tonnerre l'annonce, et les troupeaux font connaître qu'il s'approche.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >