< Job 29 >
1 Job continua son discours sentencieux, et dit:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Oh! que ne suis-je comme aux mois d'autrefois, comme au jour où Dieu me gardait,
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Quand son flambeau luisait sur ma tête, quand je marchais à sa lumière dans les ténèbres;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Comme aux jours de mon automne, quand l'amitié de Dieu veillait sur ma tente;
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Quand le Tout-Puissant était encore avec moi, et que mes jeunes gens m'entouraient;
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Quand je lavais mes pieds dans le lait, et que le rocher se fondait près de moi en torrent d'huile!
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Quand je sortais pour me rendre à la porte de la ville, et que je me faisais préparer un siège dans la place publique,
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Les jeunes gens, me voyant, se retiraient; les vieillards se levaient et se tenaient debout.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Des princes s'arrêtaient de parler, et mettaient la main sur leur bouche.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 La voix des chefs s'éteignait, et leur langue s'attachait à leur palais.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Car l'oreille qui m'entendait me proclamait heureux, et l'œil qui me voyait me rendait témoignage.
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Car je délivrais l'affligé qui criait, et l'orphelin qui n'avait personne pour le secourir.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 La bénédiction de celui qui s'en allait périr venait sur moi, et je faisais chanter de joie le cœur de la veuve.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Je me revêtais de la justice, et elle se revêtait de moi. Mon équité était mon manteau et ma tiare.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 J'étais les yeux de l'aveugle, et les pieds du boiteux.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 J'étais le père des pauvres, et j'étudiais à fond la cause de l'inconnu.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Je brisais les mâchoires de l'injuste, et j'arrachais la proie d'entre ses dents.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Et je disais: Je mourrai avec mon nid, et je multiplierai mes jours comme le phénix.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Ma racine sera exposée à l'eau, et la rosée passera la nuit dans mes branches.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Ma gloire se renouvellera en moi, et mon arc se renforcera dans ma main.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 On m'écoutait, on attendait et on se taisait, jusqu'à ce que j'eusse donné mon avis.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Après que j'avais parlé, on ne répliquait pas, et ma parole découlait goutte à goutte sur eux.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Ils m'attendaient comme la pluie, et ils ouvraient leur bouche comme pour une ondée tardive.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Je souriais quand ils étaient désespérés; et ils n'altéraient pas la sérénité de mon visage.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 J'aimais à aller avec eux, et je m'asseyais à leur tête; je siégeais comme un roi au milieu de ses gardes, comme un consolateur au milieu des affligés.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.