< Job 19 >

1 Alors Job prit la parole, et dit:
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 Jusques à quand affligerez-vous mon âme, et m'accablerez-vous de paroles?
lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?
3 Voilà déjà dix fois que vous m'outragez: vous n'avez pas honte de me maltraiter?
Mara kumi hivi mmenishutumu mimi; ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.
4 Vraiment si j'ai failli, ma faute demeure avec moi.
Kama ni dhahiri kweli mimi nimekosa, makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.
5 Si vraiment vous vous élevez contre moi, si vous me reprochez l'opprobre où je me trouve,
Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi,
6 Sachez donc que c'est Dieu qui m'a fait tort, et qui a tendu ses filets autour de moi.
kisha ninyi mnapaswa kutambua kwamba Mungu amefanya mabaya kwangu mimi na amenikamata mimi katika mtego wake yeye.
7 Voici, je crie à la violence, et on ne me répond pas; je crie au secours, et il n'y a point de justice!
Tazama, Mimi ninalia kwa sauti, “dhuluma!” lakini sipati jibu. Mimi ninaita kwa ajili ya msaada, lakini hakuna haki.
8 Il a fermé mon chemin, et je ne puis passer; il a mis des ténèbres sur mes sentiers.
Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu.
9 Il m'a dépouillé de ma gloire; il a ôté la couronne de ma tête.
Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu, na ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi.
10 Il m'a détruit de tous côtés, et je m'en vais; il a arraché, comme un arbre, mon espérance.
Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande, na Mimi nimetoweka; yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.
11 Il a allumé sa colère contre moi, et il m'a tenu pour l'un de ses ennemis.
Yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi; yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.
12 Ses troupes sont venues en-semble; elles ont dressé contre moi leurs chaussées, et se sont campées autour de ma tente.
Majeshi yake huja juu pamoja; wao wananikosesha tumaini kwa kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi wakizunguka hema yangu.
13 Il a éloigné de moi mes frères, et ceux qui me connaissaient se sont écartés comme des étrangers;
Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi; watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi.
14 Mes proches m'ont abandonné, et mes connaissances m'ont oublié.
Vizazi vyangu vimeniangusha mimi; rafiki zangu wa karibu wamenisahamu mimi.
15 Les hôtes de ma maison et mes servantes m'ont traité comme un étranger; je suis devenu un inconnu pour eux.
Wale ambao mwanzoni walikaa kama wageni ndani ya nyumba yangu na watumishi wangu wa kike, hunihesabu mimi kama mgeni. Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao.
16 J'ai appelé mon serviteur, il ne m'a pas répondu; de ma propre bouche, j'ai dû le supplier.
Mimi ninamwita mtumishi wangu, lakini yeye hanipi jibu japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.
17 Mon haleine est insupportable à ma femme, et ma prière aux fils de ma mère.
Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu; Hata mimi ninachukiwa na wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.
18 Les petits enfants eux-mêmes me méprisent: si je veux me lever, ils parlent contre moi.
Hata watoto wachanga wananichukia mimi; ikiwa Mimi nitainuka kuzungumza, wao huzungumza dhidi yangu mimi.
19 Tous mes intimes m'ont en abomination, et ceux que j'aimais se sont tournés contre moi.
Rafiki zangu wote ninaowazoea wananichukia sana mimi; wale ambao Mimi ninawapenda wamegeuka kinyume na mimi.
20 Mes os se sont attachés à ma peau et à ma chair, et je me suis échappé avec la peau de mes dents.
Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu; Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.
21 Ayez pitié de moi, ayez pitié de moi, vous, mes amis! Car la main de Dieu m'a frappé.
Iweni na huruma juu yangu mimi, muwe na huruma juu yangu mimi, rafiki zangu, kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mimi.
22 Pourquoi me persécutez-vous comme Dieu, et ne pouvez-vous vous rassasier de ma chair?
Kwa nini mnanitesa mimi kama ninyi mlikuwa Mungu? kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?
23 Oh! je voudrais que mes paroles fussent écrites quelque part! Je voudrais qu'elles fussent inscrites dans un livre;
Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini! Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
24 Qu'avec un burin de fer et avec du plomb, elles fussent gravées sur le roc, pour toujours!
Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!
25 Pour moi, je sais que mon Rédempteur est vivant, qu'à la fin il se lèvera sur la terre,
Lakini kama ilivyo kwangu mimi, Mimi ninafahamu kwamba mkombozi wangu anaishi, na kwamba hata mwisho atasimama katika nchi;
26 Et qu'après cette peau qui se détruit, et hors de ma chair, je verrai Dieu;
baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa, ndipo katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.
27 Moi, je le verrai, à moi propice; mes yeux le verront, et non un autre. Mes reins se consument en mon sein!
Mimi nitamwona yeye kwa macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine. Moyo wangu hushindwa ndani yangu mimi.
28 Si vous dites: Comment le poursuivrons-nous, et trouverons-nous en lui la cause de son malheur?
Kama mnatasema, 'Kwa jinsi gani tutamtesa yeye? Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;
29 Craignez l'épée pour vous-mêmes, car la fureur est un crime digne de l'épée, afin que vous sachiez qu'il y a un jugement.
ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga, kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga, hivyo kwamba wewe uweze kutambua kuna hukumu.”

< Job 19 >