< Jérémie 30 >

1 La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de l'Éternel, en ces termes:
Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
2 Ainsi a parlé l'Éternel, le Dieu d'Israël: Écris dans un livre toutes les paroles que je t'ai dites.
“Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
3 Car voici, les jours viennent, dit l'Éternel, où je ramènerai les captifs de mon peuple d'Israël et de Juda, a dit l'Éternel; je les ramènerai dans le pays que j'ai donné à leurs pères, et ils le posséderont.
Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
4 Et ce sont ici les paroles que l'Éternel a prononcées pour Israël et Juda;
Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
5 Car ainsi a dit l'Éternel: Nous entendons des cris d'effroi; c'est l'épouvante; et il n'y a point de paix!
“Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
6 Informez-vous, et voyez si un mâle enfante. Pourquoi vois-je tout homme les mains sur les reins, comme une femme en travail? Et pourquoi tous les visages sont-ils devenus livides?
Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
7 Hélas! c'est que cette journée est grande, et qu'il n'y en a point eu de semblable. C'est un temps de détresse pour Jacob! Pourtant il en sera délivré.
Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
8 Et en ce jour-là, dit l'Éternel des armées, je briserai son joug de dessus ton cou, et je romprai tes liens; et les étrangers ne t'asserviront plus.
Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
9 Ils serviront l'Éternel leur Dieu et David leur roi, que je leur susciterai.
Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
10 Toi donc, mon serviteur Jacob, ne crains point, dit l'Éternel; ne t'épouvante pas, Israël! car voici, je te délivrerai de la terre lointaine, et ta postérité du pays de leur captivité. Alors Jacob reviendra, et il sera tranquille et à l'aise, et il n'y aura personne qui le trouble.
Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
11 Car je suis avec toi, dit l'Éternel, pour te délivrer. Je détruirai entière-ment toutes les nations parmi lesquelles je t'ai dispersé; mais toi, je ne te détruirai point entièrement; je te châtierai avec mesure; cependant je ne te tiendrai pas pour innocent.
Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
12 Car ainsi a dit l'Éternel: Ta blessure est incurable; ta plaie est sans espoir.
Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
13 Nul ne prend ton parti, pour bander ta plaie; il n'y a pour toi nul remède, nul moyen de guérison.
Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
14 Tous ceux qui t'aiment t'ont oubliée; ils ne s'inquiètent plus de toi; car je t'ai frappée comme frappe un ennemi, comme châtie un homme cruel, à cause de la multitude de tes iniquités, parce que tes péchés se sont accrus.
Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
15 Pourquoi cries-tu pour ta blessure? Ta douleur est incurable. C'est pour la grandeur de ton iniquité, parce que tes péchés se sont accrus, que je t'ai fait ces choses.
Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
16 Cependant tous ceux qui te dévorent seront dévorés, et tous tes oppresseurs, tous, s'en iront en captivité; ceux qui te dépouillent seront dépouillés, et je livrerai au pillage tous ceux qui te pillent.
Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
17 Mais je consoliderai tes plaies et je te guérirai, dit l'Éternel; car ils t'ont appelée la répudiée: c'est Sion, dont nul ne s'enquiert!
Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
18 Ainsi a dit l'Éternel: Voici je ramène les captifs des tentes de Jacob, et j'ai compassion de ses demeures; la ville sera rebâtie sur sa hauteur, et le palais habité selon l'usage.
Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
19 Et il en sortira des chants de louange et des cris de réjouissance. Je les multiplierai, et ils ne diminueront pas; je les honorerai, et ils ne seront pas avilis.
Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
20 Ses fils seront comme autrefois, son assemblée sera affermie devant moi, et je punirai tous ceux qui l'oppriment.
Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
21 Et son chef sera pris de lui, et son dominateur sera issu de son sein. Je le ferai approcher, et il viendra vers moi; car qui est celui qui exposerait son cœur à s'approcher de moi? dit l'Éternel.
Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
22 Et vous serez mon peuple, et je serai votre Dieu.
Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
23 Voici, la tempête de l'Éternel, la fureur éclate, et l'orage prêt à fondre tombera sur la tête des méchants.
Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
24 L'ardeur de la colère de l'Éternel ne se détournera pas, jusqu'à ce qu'il ait exécuté et accompli les desseins de son cœur. Vous entendrez ceci dans les derniers jours.
Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”

< Jérémie 30 >