< Jérémie 27 >

1 Au commencement du règne de Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole fut adressée par l'Éternel à Jérémie, en ces termes:
Mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 L'Éternel me dit ainsi: Fais-toi des liens et des jougs, et mets-les sur ton cou;
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Tengeneza nira, ujivike shingoni mwako, uifunge kwa kamba za ngozi.
3 Et envoie-les au roi d'Édom, au roi de Moab, au roi des enfants d'Ammon, au roi de Tyr, et au roi de Sidon, par les mains des ambassadeurs qui viennent à Jérusalem, vers Sédécias, roi de Juda.
Kisha utume ujumbe kwa wafalme wa Edomu, Moabu, Amoni, Tiro na Sidoni kupitia wajumbe ambao wamekuja Yerusalemu kwa Sedekia mfalme wa Yuda.
4 Et donne-leur mes ordres pour leurs maîtres, en disant: Ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël: Vous direz ainsi à vos maîtres:
Wape ujumbe kwa ajili ya mabwana zao na uwaambie: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Waambieni hivi mabwana zenu:
5 J'ai fait la terre, les hommes et les bêtes qui sont sur la terre, par ma grande force et par mon bras étendu; et je les donne à qui bon me semble.
Kwa uwezo wangu mkuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa nimeumba dunia na watu wake na wanyama walioko ndani yake, nami humpa yeyote inipendezavyo.
6 Et maintenant, j'ai livré tous ces pays entre les mains de Nébucadnetsar, roi de Babylone, mon serviteur; et même je lui ai donné les bêtes des champs, pour qu'elles lui soient assujetties.
Sasa nitazitia nchi zenu zote mkononi mwa mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, na nitawafanya hata wanyama wa mwituni wamtumikie.
7 Et toutes les nations lui seront assujetties, à lui et à son fils, et au fils de son fils, jusqu'à ce que le temps de son pays lui-même vienne aussi, et que plusieurs nations et de grands rois l'asservissent.
Mataifa yote yatamtumikia yeye, pamoja na mwanawe na mwana wa mwanawe, hadi wakati wa nchi yake utakapowadia, kisha mataifa mengi na wafalme wenye nguvu nyingi watamshinda.
8 Et il arrivera que la nation ou le royaume qui ne se soumettra pas à lui, à Nébucadnetsar, roi de Babylone, et qui ne soumettra pas son cou au joug du roi de Babylone, je punirai cette nation-là, dit l'Éternel, par l'épée, par la famine et par la peste, jusqu'à ce que je les aie consumés par sa main.
“‘“Lakini kama kukiwa na taifa lolote au ufalme ambao hautamtumikia Nebukadneza mfalme wa Babeli, ama kuinamisha shingo yake chini ya nira yake, nitaliadhibu taifa hilo kwa upanga, njaa na tauni, asema Bwana, mpaka nitakapoliangamiza taifa hilo kwa mkono wake.
9 Vous donc, n'écoutez pas vos prophètes, ni vos devins, ni vos songeurs, ni vos augures, ni vos magiciens qui vous parlent, disant: Vous ne serez point assujettis au roi de Babylone.
Kwa hiyo msiwasikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota ndoto wenu, watabiri na wachawi wanaowaambia ninyi: Hamtamtumikia mfalme wa Babeli.
10 Car ils vous prophétisent le mensonge, pour que vous alliez loin de votre pays, afin que je vous en chasse et que vous périssiez.
Wanawatabiria uongo ambao utawafanya ninyi mhamishwe mbali kutoka nchi yenu. Nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia.
11 Mais la nation qui soumettra son cou au joug du roi de Babylone et le servira, je la laisserai dans son pays, dit l'Éternel, afin qu'elle le cultive et y demeure.
Lakini ikiwa taifa lolote litainama na kuweka shingo lake katika nira ya mfalme wa Babeli na kumtumikia, nitaliacha taifa hilo katika nchi yake yenyewe ili wailime na kuishi humo, asema Bwana.”’”
12 Puis je parlai à Sédécias, roi de Juda, conformément à toutes ces paroles, en disant: Soumettez-vous au joug du roi de Babylone, et servez-le, lui et son peuple, et vous vivrez.
Nilitoa ujumbe huo huo kwa Sedekia mfalme wa Yuda. Nilisema, “Ingiza shingo yako katika nira ya mfalme wa Babeli, umtumikie yeye na watu wake, nawe utaishi.
13 Pourquoi mourriez-vous, toi et ton peuple, par l'épée, par la famine et par la peste, selon que l'Éternel l'a dit de la nation qui ne se soumettrait pas au roi de Babylone?
Kwa nini wewe na watu wako mfe kwa upanga, njaa na tauni, ambazo Bwana ameonya juu ya taifa lolote ambalo halitamtumikia mfalme wa Babeli?
14 N'écoutez donc pas les paroles des prophètes qui vous parlent en disant: Vous ne serez point assujettis au roi de Babylone! Car ils vous prophétisent le mensonge.
Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia kwamba, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babeli,’ kwa sababu wanawatabiria uongo.
15 Je ne les ai pas envoyés, dit l'Éternel, et ils prophétisent faussement en mon nom, afin que je vous chasse et que vous périssiez, vous et les prophètes qui vous prophétisent.
‘Sikuwatuma hao,’ asema Bwana. ‘Wanatabiri uongo kwa jina langu. Kwa hiyo, nitawafukuzia mbali, nanyi mtaangamia, ninyi pamoja na manabii wanaowatabiria.’”
16 Je parlai aussi aux sacrificateurs et à tout ce peuple, et je leur dis: Ainsi a dit l'Éternel: N'écoutez pas les paroles de vos prophètes, qui vous prophétisent, en disant: Voici, les vases de la maison de l'Éternel seront bientôt rapportés de Babylone! Car ils vous prophétisent le mensonge.
Kisha nikawaambia makuhani na watu hawa wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: Msiwasikilize manabii wanaosema, ‘Hivi karibuni sana vyombo vya nyumba ya Bwana vitarudishwa kutoka Babeli.’ Wanawatabiria ninyi uongo.
17 Ne les écoutez pas. Soumettez-vous au roi de Babylone et vous vivrez. Pourquoi cette ville deviendrait-elle une ruine?
Msiwasikilize. Mtumikieni mfalme wa Babeli, nanyi mtaishi. Kwa nini mji huu uwe magofu?
18 Et s'ils sont prophètes et si la parole de l'Éternel est avec eux, qu'ils intercèdent donc auprès de l'Éternel des armées pour que les ustensiles restant dans la maison de l'Éternel et dans la maison du roi de Juda et à Jérusalem, n'aillent point à Babylone.
Kama wao ni manabii na wanalo neno la Bwana, basi na wamsihi Bwana Mwenye Nguvu Zote ili vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Bwana na katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda na katika Yerusalemu visipelekwe Babeli.
19 Car ainsi a dit l'Éternel des armées, touchant les colonnes, et la mer, et les socles, et les autres ustensiles qui sont restés dans cette ville,
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote kuhusu zile nguzo, ile Bahari, vile vishikizo viwezavyo kuhamishika, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika mji huu,
20 Que Nébucadnetsar, roi de Babylone, n'a pas emportés quand il a transporté de Jérusalem à Babylone Jéchonias, fils de Jéhojakim, roi de Juda, avec tous les grands de Juda et de Jérusalem;
ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli hakuvichukua wakati alipomchukua Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda kwenda uhamishoni huko Babeli kutoka Yerusalemu, pamoja na wakuu wote wa Yuda na Yerusalemu.
21 Ainsi a dit l'Éternel des armées, le Dieu d'Israël, au sujet des ustensiles qui restent dans la maison de l'Éternel, et dans la maison du roi de Juda, et à Jérusalem:
Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu vitu ambavyo vimebaki ndani ya nyumba ya Bwana, na ndani ya jumba la kifalme la mfalme wa Yuda, na katika Yerusalemu:
22 Ils seront emportés à Babylone, et ils y resteront jusqu'au jour où je les chercherai, dit l'Éternel, où je les ferai remonter, et revenir en ce lieu.
‘Vitachukuliwa kupelekwa Babeli, nako huko vitabaki mpaka siku nitakayovijilia,’ asema Bwana. ‘Kisha nitavirudisha na kuvirejesha mahali hapa.’”

< Jérémie 27 >