< Jérémie 22 >

1 Ainsi a dit l'Éternel: Descends dans la maison du roi de Juda, et prononces-y cette parole.
Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
2 Dis: Écoute la parole de l'Éternel, roi de Juda, qui es assis sur le trône de David, toi, et tes serviteurs, et ton peuple, qui entrez par ces portes.
Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
3 Ainsi a dit l'Éternel: Faites droit et justice; délivrez l'opprimé de la main de l'oppresseur; n'opprimez pas, ne violentez pas l'étranger, ni l'orphelin ni la veuve, et ne répandez point le sang innocent dans ce lieu.
Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
4 Car si vous agissez suivant cette parole, les rois assis sur le trône de David entreront par les portes de cette maison, montés sur des chars et sur des chevaux, eux, leurs serviteurs et leur peuple.
Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
5 Mais si vous n'écoutez pas ces paroles, j'ai juré par moi-même, dit l'Éternel, que cette maison sera réduite en ruines.
Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
6 Car ainsi a dit l'Éternel touchant la maison du roi de Juda: Tu es pour moi comme un Galaad, comme le sommet du Liban; mais certainement, je ferai de toi un désert, des villes sans habitants.
Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
7 Je prépare contre toi des destructeurs, chacun avec ses armes, qui couperont et jetteront au feu l'élite de tes cèdres.
Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
8 Et plusieurs nations passeront près de cette ville, et chacun dira à son compagnon: Pourquoi l'Éternel a-t-il fait ainsi à cette grande ville?
Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
9 Et on répondra: Parce qu'ils ont abandonné l'alliance de l'Éternel leur Dieu, et qu'ils se sont prosternés devant d'autres dieux, et les ont servis.
Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
10 Ne pleurez point celui qui est mort; ne faites point sur lui de condoléance. Mais pleurez, pleurez celui qui s'en va; car il ne reviendra plus, il ne reverra plus le pays de sa naissance!
Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
11 Car ainsi a dit l'Éternel, sur Shallum, fils de Josias, roi de Juda, qui régnait à la place de Josias, son père, et qui est sorti de ce lieu:
Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
12 Il n'y reviendra plus; mais il mourra dans le lieu où on l'a transporté, et il ne verra plus ce pays.
Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
13 Malheur à celui qui bâtit sa maison par l'injustice, et ses étages par l'iniquité; qui se sert de son prochain sans le payer, et ne lui donne pas le salaire de son travail;
Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
14 Qui dit: Je me bâtirai une vaste maison, et des étages bien aérés; qui s'y fait percer des fenêtres, la lambrisse de cèdre, et qui la peint de vermillon!
Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
15 Crois-tu que tu règnes, parce que tu te piques d'employer le cèdre? Ton père n'a-t-il pas mangé et bu? Il fit droit et justice; alors il prospéra.
Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
16 Il jugea la cause de l'affligé et du pauvre; alors il prospéra. N'est-ce pas là me connaître? dit l'Éternel.
Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
17 Mais tu n'as des yeux et un cœur que pour ta cupidité, pour répandre le sang innocent, et pour exercer l'oppression et la violence.
Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
18 C'est pourquoi, ainsi a dit l'Éternel touchant Jéhojakim, fils de Josias, roi de Juda: On ne le pleurera point, en disant: hélas, mon frère; hélas, ma sœur! On ne le plaindra point, en disant: hélas, seigneur! hélas, sa majesté!
Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
19 Il sera enseveli de la sépulture d'un âne; il sera traîné et jeté hors des portes de Jérusalem.
Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
20 Monte au Liban, et crie; élève ta voix sur le Bassan; et crie du mont Abarim! Car tous ceux qui t'aimaient sont détruits.
Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
21 Je t'ai parlé dans tes prospérités; tu as dit: Je n'écouterai pas! Tel est ton train dès ta jeunesse: tu n'as pas écouté ma voix.
Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
22 Le vent se repaîtra de tous ceux qui te paissent, et ceux qui t'aiment iront en captivité. Certainement alors tu seras honteuse et dans l'ignominie, à cause de toute ta malice.
Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
23 Toi qui habites le Liban et qui fais ton nid dans les cèdres, que tu seras à plaindre quand te surviendront les douleurs et l'angoisse, comme à la femme en travail!
Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
24 Je suis vivant! dit l'Éternel; quand Chonia, fils de Jéhojakim, roi de Juda, serait un cachet à ma main droite, je t'arracherais de là!
“Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
25 Je te livrerai entre les mains de ceux qui cherchent ta vie, entre les mains de ceux dont la présence te fait peur, et entre les mains de Nébucadnetsar, roi de Babylone, et entre les mains des Caldéens.
Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
26 Je te jetterai, toi et ta mère qui t'a enfanté, dans cet autre pays où vous n'êtes point nés, et c'est là que vous mourrez.
Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
27 Et quant au pays où leur âme aspire à retourner, ils n'y retourneront point.
Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
28 Est-il donc, ce Chonia, un vase de rebut, mis en pièces? un ustensile qui ne fait plus de plaisir? Pourquoi sont-ils jetés, lui et sa postérité, lancés dans un pays qu'ils ne connaissent pas?
Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
29 O terre, terre, terre! écoute la parole de l'Éternel.
Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
30 Ainsi a dit l'Éternel: Inscrivez cet homme comme n'ayant point d'enfants, comme un homme qui ne prospérera point dans ses jours; car de sa postérité personne ne réussira à siéger sur le trône de David, ni à dominer encore en Juda.
Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”

< Jérémie 22 >