< Isaïe 29 >
1 Malheur à Ariel! Ariel, ville où campa David! Ajoutez année sur année, que les fêtes reviennent tour à tour, et je mettrai Ariel à l'étroit;
Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 Elle ne sera que plaintes et gémissements; mais elle sera pour moi comme un Ariel (Lion de Dieu).
Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 Je camperai contre toi tout à l'entour, je te cernerai avec des postes armés, je dresserai des forts contre toi.
Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
4 Tu seras abaissée; tu parleras comme de dessous terre, et ta parole sortira étouffée de la poussière; ta voix montera de la terre comme celle d'un évocateur d'esprits; ta parole sera comme un murmure sortant de la poussière.
Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
5 Mais la foule de tes ennemis sera comme la poussière menue, et la foule des hommes puissants comme la balle qui s'envole; et cela tout à coup, en un instant.
Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
6 Tu seras châtiée par l'Éternel des armées, avec des tonnerres, des tremblements de terre et un grand bruit, avec la tempête, le tourbillon et la flamme d'un feu dévorant.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 Et comme il arrive dans un songe, dans une vision de la nuit, ainsi en sera-t-il de la multitude de toutes les nations qui combattront contre Ariel, de tous ceux qui l'attaqueront, elle et sa forteresse, et qui la serreront de près.
Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 Comme un homme affamé songe qu'il mange, mais quand il s'éveille, son âme est vide; et comme un homme altéré songe qu'il boit, mais quand il s'éveille, le voici languissant et son âme est altérée; ainsi en sera-t-il de toute la multitude de nations qui combattront contre la montagne de Sion.
kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Soyez étonnés et stupéfaits! Soyez aveuglés et éblouis! Ils sont ivres, mais non pas de vin; ils chancellent, mais non par la boisson forte!
Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 Car l'Éternel a répandu sur vous un esprit d'assoupissement; il a fermé vos yeux, - les prophètes; il a voilé vos têtes, - les voyants.
Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
11 Aussi toutes les visions sont devenues pour vous comme la parole d'un livre scellé, qu'on donnerait à un homme sachant lire, en lui disant: Lis ceci! et qui répondrait: Je ne puis, car il est scellé;
Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
12 Ou qu'on donnerait à un homme ne sachant pas lire, en lui disant: Lis ceci! et qui répondrait: Je ne sais pas lire.
Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 Et le Seigneur dit: Puisque ce peuple s'approche de moi de sa bouche, et qu'ils m'honorent de leurs lèvres, mais leur cœur est éloigné de moi; puisque la crainte qu'ils ont de moi n'est qu'un commandement enseigné par des hommes;
Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 A cause de cela, voici je continuerai à user de prodiges à l'égard de ce peuple, de miracles et de prodiges; la sagesse de ses sages périra, et l'intelligence de ses intelligents disparaîtra.
Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Malheur à ceux qui cachent profondément leurs desseins, pour les dérober à l'Éternel, qui font leurs œuvres dans les ténèbres, et qui disent: Qui nous voit, et qui nous connaît?
Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Pervers que vous êtes, l'argile sera-t-elle estimée à l'égal du potier? tellement que l'ouvrage dise de celui qui l'a fait: Il ne m'a point fait; et que l'œuvre dise de l'ouvrier: Il n'y entend rien?
Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
17 Encore un peu de temps, le Liban ne sera-t-il pas changé en verger, et le verger regardé comme une forêt?
Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 En ce jour-là les sourds entendront les paroles du livre; et les yeux des aveugles, délivrés de l'obscurité et des ténèbres, verront.
Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 Les débonnaires auront en l'Éternel joie sur joie, et les pauvres d'entre les hommes s'égaieront dans le Saint d'Israël.
Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 Car l'oppresseur ne sera plus; le moqueur sera détruit, et ceux qui veillent pour commettre l'iniquité seront retranchés,
Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 Ceux qui font condamner un homme par leur parole, qui tendent des pièges à l'homme qui plaide devant les portes, qui perdent le juste par leurs fraudes.
wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 C'est pourquoi l'Éternel qui a racheté Abraham, a dit ainsi à la maison de Jacob: Jacob ne sera plus dans la honte, et sa face ne pâlira plus.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 Car, lorsqu'il verra au milieu de lui ses fils, l'œuvre de mes mains, il sanctifiera mon nom; il sanctifiera le Saint de Jacob, il révérera le Dieu d'Israël.
Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 Et ceux qui avaient l'esprit égaré deviendront entendus, et ceux qui murmuraient apprendront la sagesse.
Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”