< Isaïe 27 >
1 En ce jour-là, l'Éternel frappera, de sa dure, grande et forte épée, le Léviathan, le serpent agile, le Léviathan, le serpent tortueux, et il tuera le monstre marin.
Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
2 En ce temps-là, on chantera ainsi sur la vigne excellente:
Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
3 C'est moi, l'Éternel, qui la garde; je l'arroserai en tout temps; je la garderai nuit et jour, de peur qu'on ne lui fasse du mal.
Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
4 Il n'y a point en moi de colère. Qu'on me donne des ronces, des épines à combattre! Je marcherai sur elles, je les brûlerai toutes ensemble.
Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
5 Ou bien qu'il me prenne pour refuge! Qu'il fasse la paix avec moi, qu'il fasse la paix avec moi!
Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
6 Un jour, Jacob poussera des racines; Israël fleurira et s'épanouira; ils couvriront de fruits la face de la terre.
Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
7 Dieu a-t-il frappé son peuple, comme l'ont été ceux qui le frappaient? Israël a-t-il été tué, comme le furent ceux qui le tuaient?
Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
8 C'est avec mesure que tu l'as châtié en le rejetant, lorsqu'il fut emporté par ton souffle impétueux, au jour du vent d'orient.
Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
9 Aussi l'iniquité de Jacob est ainsi expiée; et voici le fruit du pardon de son péché: c'est qu'il a mis en poussière toutes les pierres des autels, comme des pierres à chaux; les emblèmes d'Ashéra ni les colonnes solaires ne se relèveront plus.
Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
10 Car la ville forte est changée en solitude; c'est une demeure abandonnée, délaissée comme un désert. Là vient paître le veau; il s'y couche, et broute les branches qui s'y trouvent.
Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
11 Quand le branchage en est sec, on le brise, et les femmes y viennent pour allumer du feu. Car ce peuple n'a point d'intelligence; c'est pourquoi son créateur n'a pas pitié de lui; celui qui l'a formé ne lui fait pas grâce.
Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
12 En ce jour-là, l'Éternel abattra les fruits depuis le cours du Fleuve jusqu'au torrent d'Égypte; et vous serez ramassés un par un, ô enfants d'Israël!
Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
13 En ce jour-là, on sonnera de la grande trompette; et ceux qui étaient perdus au pays d'Assur, et ceux qui étaient chassés au pays d'Égypte, viendront se prosterner devant l'Éternel, en la sainte montagne, à Jérusalem.
Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.