< Isaïe 15 >

1 Oracle sur Moab. La nuit même où on la ravage, Ar-Moab périt! La nuit même où on la ravage, Kir-Moab périt!
Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
2 On monte à la maison des dieux et à Dibon, sur les hauts lieux, pour pleurer. Moab se lamente sur Nébo et sur Médéba; toutes les têtes sont rasées, toutes les barbes sont coupées.
Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
3 On est ceint de sacs dans ses rues; sur ses toits et dans ses places, chacun gémit et fond en larmes.
Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
4 Hesbon et Élealé se lamentent, leur voix est entendue jusqu'à Jahats; aussi les guerriers de Moab jettent des cris; son âme est tremblante.
Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
5 Mon cœur gémit sur Moab, dont les fugitifs courent jusqu'à Tsoar, jusqu'à Églath-Shélishija. Car on monte en pleurant la montée de Luchith; car on fait retentir le cri de la ruine au chemin de Horonajim.
Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
6 Même les eaux de Nimrim ne sont que désolation; le gazon est desséché, l'herbe a disparu, il n'y a plus de verdure.
Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
7 Aussi l'épargne qu'ils avaient faite, ce qu'ils avaient mis en réserve, ils l'emportent au torrent des saules.
Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
8 Et les cris font le tour des frontières de Moab; ses gémissements vont jusqu'à Églaïm; ses gémissements vont jusqu'à Béer-Élim.
Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
9 Et les eaux de Dimon sont pleines de sang; et j'enverrai sur Dimon un surcroît de maux: les lions contre les réchappés de Moab, et contre ce qui reste du pays.
Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

< Isaïe 15 >