< Osée 4 >

1 Écoutez la parole de l'Éternel, enfants d'Israël! Car l'Éternel a un procès avec les habitants du pays, parce qu'il n'y a ni vérité, ni bonté, ni connaissance de Dieu, dans le pays.
Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
2 Il n'y a que parjures et mensonges; meurtres, vols et adultères; on use de violence, et un meurtre touche l'autre.
Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
3 C'est pourquoi le pays sera dans le deuil, et tous ses habitants dans la langueur, avec les bêtes des champs et les oiseaux des cieux; même les poissons de la mer périront.
Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
4 Mais que nul ne conteste, et que nul ne reprenne! Car ton peuple est comme ceux qui disputent avec le sacrificateur.
Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
5 Tu tomberas de jour; le prophète aussi tombera avec toi de nuit; et je détruirai ta mère.
Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
6 Mon peuple est détruit, faute de connaissance. Puisque toi tu as rejeté la connaissance, je te rejetterai, afin que tu n'exerces plus devant moi le sacerdoce; puisque tu as oublié la loi de ton Dieu, moi aussi j'oublierai tes enfants.
Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
7 Plus ils se sont multipliés, plus ils ont péché contre moi: je changerai leur gloire en ignominie!
Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
8 Ils se nourrissent des péchés de mon peuple; ils sont avides de ses iniquités.
Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
9 Aussi il en sera du sacrificateur comme du peuple; je le punirai selon ses voies et lui rendrai selon ses œuvres.
Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
10 Ils mangeront, et ne seront pas rassasiés; ils se prostitueront, et ne multiplieront pas. Car ils ont abandonné l'Éternel, pour ne pas observer sa loi.
Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
11 La fornication, le vin et le moût ôtent l'entendement.
Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
12 Mon peuple consulte son bois, et son bâton lui prophétise; car l'esprit de fornication égare, et ils se prostituent en abandonnant leur Dieu.
Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
13 Ils sacrifient sur le sommet des montagnes; sur les coteaux, ils font fumer le parfum; sous le chêne, le peuplier, le térébinthe, dont l'ombre est agréable. C'est pourquoi vos filles se prostituent, et vos belles-filles commettent adultère.
Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
14 Je ne punirai point vos filles parce qu'elles se prostituent, ni vos belles-filles parce qu'elles commettent adultère. Car eux-mêmes se retirent avec des prostituées, et sacrifient avec les femmes consacrées à l'impudicité; et le peuple sans intelligence court à sa ruine.
Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
15 Si tu te prostitues, Israël, que Juda ne se rende pas coupable! N'entrez pas à Guilgal! Et ne montez point à Beth-Aven! Et ne jurez point: “L'Éternel est vivant! “
Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
16 Parce qu'Israël a été rebelle comme une génisse indomptée, maintenant l'Éternel les fera paître comme un agneau dans des lieux spacieux.
Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
17 Éphraïm s'est associé aux idoles: abandonne-le!
Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
18 Ont-ils fini de boire, les voilà à la fornication. Les chefs d'Israël n'aiment que l'ignominie.
Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
19 Le vent les attachera à ses ailes, et ils auront honte de leurs sacrifices.
Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.

< Osée 4 >