< Genèse 8 >

1 Or, Dieu se souvint de Noé, et de tous les animaux et de tout le bétail qui étaient avec lui dans l'arche. Et Dieu fit passer un vent sur la terre, et les eaux s'arrêtèrent.
Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
2 Et les sources de l'abîme et les bondes des cieux se fermèrent; et la pluie fut retenue des cieux.
Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa, na mvua ikakoma kunyesha.
3 Et les eaux se retirèrent de dessus la terre; elles allèrent se retirant; et les eaux diminuèrent au bout de cent cinquante jours.
Maji ya gharika yakaanza kuzama kidogo kidogo katika nchi. na mwisho wa siku miamoja na hamsini maji yakawa yamezama chini.
4 Et au septième mois, au dix-septième jour du mois, l'arche s'arrêta sur les montagnes d'Ararat.
safina ikatulia katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, juu ya milima ya Ararati.
5 Et les eaux allèrent diminuant, jusqu'au dixième mois. Au dixième mois, au premier jour du mois, ap-parurent les sommets des montagnes.
Maji yakaendelea kuzama chini hadi mwezi wa kumi. Siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
6 Et il arriva qu'au bout de quarante jours Noé ouvrit la fenêtre qu'il avait faite à l'arche.
Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
7 Et il lâcha le corbeau, qui sortit, allant et revenant, jusqu'à ce que les eaux eussent séché de dessus la terre.
Akatuma kunguru na akaruka hadi maji yalipo kauka katika nchi.
8 Puis il lâcha la colombe d'avec lui, pour voir si les eaux avaient fort diminué à la surface de la terre.
Kisha akatuma njiwa kuona kama maji yamezama chini kutoka kwenye uso wa nchi,
9 Mais la colombe ne trouva pas où poser la plante de son pied, et elle retourna vers lui dans l'arche; car il y avait de l'eau à la surface de toute la terre. Et Noé avança sa main, la prit, et la ramena vers lui dans l'arche.
lakini njiwa hakuona sehemu ya kutua unyayo wake, na akarudi kwake ndani ya safina, kwa kuwa maji yalikuwa bado yamefunika nchi yote. Akanyoosha mkono wake, akamchukua na kumuweka ndani ya safina pamoja naye.
10 Et il attendit encore sept autres jours, puis il lâcha de nouveau la colombe hors de l'arche.
Akasubiri siku saba zingine akatuma tena njiwa kutoka kwenye safina.
11 Et la colombe revint à lui vers le soir; et voici, une feuille d'olivier fraîche était à son bec; et Noé comprit que les eaux avaient fort diminué sur la terre.
Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
12 Et il attendit encore sept autres jours; puis il lâcha la colombe; mais elle ne retourna plus à lui.
Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
13 Et il arriva en l'an six cent un de la vie de Noé, au premier mois, au premier jour du mois, que les eaux avaient séché sur la terre; et Noé ôta la couverture de l'arche, et regarda; et voici, la surface du sol avait séché.
Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
14 Au second mois, au vingt-septième jour du mois, la terre fut sèche.
Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa imekauka.
15 Alors Dieu parla à Noé, en disant:
Mungu akamwambia Nuhu,
16 Sors de l'arche, toi, ta femme, tes fils, et les femmes de tes fils avec toi.
“Toka nje ya safina, wewe, mke wako, wanao wa kiume, na wake wa wanao pamoja nawe.
17 Fais sortir avec toi tous les animaux qui sont avec toi, de toute chair, tant des oiseaux que des bêtes, et de tous les reptiles qui rampent sur la terre; et qu'ils peuplent en abondance la terre, et qu'ils croissent et multiplient sur la terre.
Wachukuwe utoke nje pamoja nao kila kiumbe hai chenye mwili ambacho kiko nawe - ndege, wanyama wa kufugwa, na kila kitambaacho ambacho hutambaa juu ya nchi - ili kwamba viweze kukua na kuwa na idadi kubwa zaidi ya viumbe hai katika nchi yote, kwa kuzaliana na kuongezeka juu ya nchi.”
18 Et Noé sortit, et ses fils, sa femme, et les femmes de ses fils avec lui.
Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
19 Tous les animaux, tous les reptiles et tous les oiseaux, tout ce qui rampe sur la terre, selon leurs familles, sortirent de l'arche.
Kila kiumbe hai, kila kitambaacho, na kila ndege, na kila kiendacho juu ya nchi, kwa kabila zao, wakaiacha safina.
20 Et Noé bâtit un autel à l'Éternel; et il prit de toute bête pure, et de tout oiseau pur, et il offrit des holocaustes sur l'autel.
Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 Et l'Éternel respira l'agréable odeur, et l'Éternel dit en son cœur: Je ne maudirai plus la terre, à cause de l'homme; car la nature du cœur de l'homme est mauvaise dès sa jeunesse; et je ne frapperai plus tout ce qui vit, comme je l'ai fait.
Yahwe akanusa harufu nzuri ya kuridhisha na akasema moyoni mwake, “Sita laani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, ingawa nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto. Wala sita haribu kilakitu chenye uhai, kama nilivyo fanya.
22 Tant que la terre durera, les semailles et la moisson, le froid et le chaud, l'été et l'hiver, et le jour et la nuit, ne cesseront point.
Wakati nchi isaliapo, majira ya kupanda mbegu na mavuno, baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi, mchana na usiku havitakoma.”

< Genèse 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark