< Genèse 21 >

1 Et l'Éternel visita Sara, comme il l'avait dit; et l'Éternel fit à Sara comme il en avait parlé.
Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
2 Et Sara conçut, et enfanta un fils à Abraham dans sa vieillesse, à l'époque que Dieu lui avait dite.
Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
3 Et Abraham appela son fils, qui lui était né, et que Sara lui avait enfanté, Isaac.
Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
4 Et Abraham circoncit Isaac son fils à l'âge de huit jours, comme Dieu le lui avait commandé.
Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
5 Or, Abrabam était âgé de cent ans, quand Isaac, son fils, lui naquit.
Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
6 Et Sara dit: Dieu m'a fait une chose qui fera rire; tous ceux qui l'apprendront, riront à mon sujet.
Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
7 Puis elle dit: Qui eût dit à Abraham que Sara allaiterait des enfants? car je lui ai enfanté un fils dans sa vieillesse.
Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
8 Et l'enfant grandit, et fut sevré. Et Abraham fit un grand festin le jour où Isaac fut sevré.
Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
9 Et Sara vit le fils d'Agar l'Égyptienne qu'elle avait enfanté à Abraham, qui riait.
Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
10 Et elle dit à Abraham: Chasse cette servante et son fils, car le fils de cette servante n'héritera point avec mon fils, avec Isaac.
Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
11 Et cette parole déplut fort à Abraham, à cause de son fils.
Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
12 Mais Dieu dit à Abraham: Que cela ne te déplaise pas à cause de l'enfant et de ta servante. Quoi que te dise Sara, obéis à sa voix: car c'est en Isaac que ta postérité sera appelée de ton nom.
Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
13 Mais je ferai aussi du fils de la servante une nation, parce qu'il est ta race.
Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
14 Et Abraham se leva de bon matin, prit du pain et une outre d'eau, et les donna à Agar; il les mit sur son épaule; il lui donna aussi l'enfant et la renvoya. Et elle s'en alla et erra dans le désert de Béer-Shéba.
Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
15 Quand l'eau de l'outre fut épuisée, elle laissa l'enfant sous un des arbrisseaux.
Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
16 Et elle s'en alla, et s'assit vis-à-vis, environ à la distance d'une portée d'arc; car elle dit: Que je ne voie pas mourir l'enfant. Et elle s'assit vis-à-vis, éleva la voix, et pleura.
Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
17 Et Dieu entendit la voix du jeune garçon, et l'ange de Dieu appela des cieux Agar, et lui dit: Qu'as-tu, Agar? Ne crains point, car Dieu a entendu la voix du jeune garçon, là où il est.
Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
18 Lève-toi, prends le jeune garçon, et tiens-le par la main; car je ferai de lui une grande nation.
Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19 Et Dieu lui ouvrit les yeux, et elle vit un puits d'eau, et elle alla et remplit l'outre d'eau, et donna à boire au jeune garçon.
Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
20 Et Dieu fut avec le jeune garçon, qui devint grand, et habita dans le désert; et il fut tireur d'arc.
Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
21 Et il habita dans le désert de Paran. Et sa mère lui prit une femme du pays d'Égypte.
Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
22 Et il arriva qu'en ce temps-là Abimélec, accompagné de Picol, chef de son armée, parla à Abraham, en disant: Dieu est avec toi dans tout ce que tu fais.
Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
23 Maintenant donc, jure-moi ici par le nom de Dieu, que tu ne tromperas ni moi, ni mes enfants, ni ma race. Tu agiras envers moi et envers le pays où tu as séjourné, avec la même bonté avec laquelle j'ai agi envers toi.
Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
24 Et Abraham répondit: Je le jurerai.
Abraham akasema, “Nina apa.”
25 Mais Abraham se plaignit à Abimélec à cause d'un puits d'eau, dont les serviteurs d'Abimélec s'étaient emparés.
Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
26 Et Abimélec dit: Je ne sais qui a fait cela; toi-même tu ne m'en as point averti, et moi je n'en ai entendu parler qu'aujourd'hui.
Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
27 Alors Abraham prit des brebis et des bœufs, et les donna à Abimélec, et ils firent alliance ensemble.
Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
28 Et Abraham mit à part sept jeunes brebis du troupeau.
Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
29 Et Abimélec dit à Abraham: Qu'est-ce que ces sept jeunes brebis que tu as mises à part?
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
30 Et il répondit: C'est que tu accepteras ces sept jeunes brebis de ma main, afin que ce me soit un témoignage que j'ai creusé ce puits.
Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
31 C'est pourquoi on appela ce lieu-là Béer-Shéba (puits du serment); car ils y jurèrent tous deux.
Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
32 Ils traitèrent donc alliance à Béer-Shéba. Puis Abimélec se leva avec Picol, chef de son armée, et ils retournèrent au pays des Philistins.
Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33 Et Abraham planta un tamarin à Béer-Shéba, et il invoqua là le nom de l'Éternel, le Dieu d'éternité.
Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
34 Et Abraham séjourna longtemps au pays des Philistins.
Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.

< Genèse 21 >