< Ézéchiel 25 >

1 La parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Fils de l'homme, tourne ta face vers les enfants d'Ammon, et prophétise contre eux.
“Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
3 Dis aux enfants d'Ammon: Écoutez la parole du Seigneur, l'Éternel. Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce que tu as dit: ah! ah! à propos de mon sanctuaire, quand il fut profané, et du pays d'Israël, quand il fut dévasté, et de la maison de Juda, lorsqu'elle se rendit en captivité,
Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
4 Voici, je te livre aux enfants de l'Orient. Ils établiront au milieu de toi leurs parcs, et ils y placeront leurs demeures; ils mangeront tes fruits, et ils boiront ton lait.
kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
5 De Rabba, je ferai un pâturage pour les chameaux, et du pays des enfants d'Ammon, un bercail pour les moutons, et vous saurez que je suis l'Éternel.
Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
6 Car ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce que tu as battu des mains et frappé du pied, que tu t'es réjoui avec dédain en ton âme, au sujet du pays d'Israël,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
7 Voici, j'étends ma main sur toi et je te livre en proie aux nations; je te retranche d'entre les peuples, je te fais disparaître d'entre les pays, je t'extermine, et tu sauras que je suis l'Éternel.
Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
8 Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce que Moab et Séïr ont dit: voici, il en est de la maison de Juda comme de toutes les nations;
Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
9 A cause de cela, voici, j'ouvre le flanc de Moab, du côté de ses villes, ses villes frontières, l'ornement du pays, Beth-Jéshimoth, Baal-Méon et Kirjathaïm;
Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
10 Je l'ouvre aux enfants de l'Orient, qui marchent contre les enfants d'Ammon, et je le leur donne en possession, afin que les enfants d'Ammon ne soient plus rangés au nombre des nations.
kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
11 J'exercerai mes jugements contre Moab et ils sauront que je suis l'Éternel.
Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
12 Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce qu'Édom s'est livré à la vengeance à l'égard de la maison de Juda, et s'est rendu coupable en se vengeant d'elle,
Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
13 Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: J'étends ma main sur Édom; j'en extermine hommes et bêtes; je le réduis en désert; de Théman à Dédan ils tomberont par l'épée.
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
14 J'exercerai ma vengeance sur Édom par la main de mon peuple d'Israël, et ils traiteront Édom selon ma colère et selon ma fureur; ils sauront ce qu'est ma vengeance, dit le Seigneur, l'Éternel.
Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
15 Ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Parce que les Philistins ont agi par vengeance, et qu'ils se sont vengés inhumainement, avec mépris, et selon leur désir, jusqu'à tout détruire dans une haine éternelle,
Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
16 A cause de cela, ainsi a dit le Seigneur, l'Éternel: Voici, j'étends ma main sur les Philistins, et j'extermine les Kéréthiens, et je fais périr ce qui reste sur la côte de la mer.
Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
17 J'exercerai sur eux de grandes vengeances par des châtiments pleins de fureur, et ils sauront que je suis l'Éternel, quand j'exécuterai contre eux ma vengeance.
Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'

< Ézéchiel 25 >