< Exode 10 >

1 Et l'Éternel dit à Moïse: Va vers Pharaon, car j'ai appesanti son cœur et le cœur de ses serviteurs, afin de mettre au milieu d'eux mes prodiges,
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili kwamba nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao
2 Et afin que tu racontes à ton fils et au fils de ton fils, les exploits que j'aurai accomplis sur les Égyptiens et les prodiges que j'aurai faits au milieu d'eux, et que vous sachiez que je suis l'Éternel.
ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
3 Moïse et Aaron vinrent donc vers Pharaon, et lui dirent: Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu des Hébreux: Jusqu'à quand refuseras-tu de t'humilier devant moi? Laisse aller mon peuple, afin qu'il me serve.
Kwa hiyo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
4 Car si tu refuses de laisser aller mon peuple, voici, je ferai venir demain des sauterelles dans ton territoire.
Kama ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
5 Et elles couvriront la face de la terre, et l'on ne pourra plus voir la terre; et elles dévoreront le reste de ce qui est échappé, ce que la grêle vous a laissé; et elles dévoreront tous les arbres qui poussent dans vos champs;
Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
6 Et elles rempliront tes maisons, et les maisons de tous tes serviteurs, et les maisons de tous les Égyptiens; ce que tes pères n'ont point vu, ni les pères de tes pères, depuis le jour qu'ils ont été sur la terre, jusqu'à ce jour. Puis il se tourna et sortit de chez Pharaon.
Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii mpaka leo hii.’” Ndipo Mose akageuka na kumwacha Farao.
7 Et les serviteurs de Pharaon lui dirent: Jusqu'à quand celui-ci nous sera-t-il en piège? Laisse aller ces gens, et qu'ils servent l'Éternel leur Dieu. Ne vois-tu pas encore que l'Égypte est perdue?
Maafisa wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Bwana Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
8 Alors on fit revenir Moïse et Aaron vers Pharaon, et il leur dit: Allez, servez l'Éternel votre Dieu. Quels sont tous ceux qui iront?
Ndipo Mose na Aroni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Bwana Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaokwenda?”
9 Et Moïse répondit: Nous irons avec nos jeunes gens et nos vieillards, avec nos fils et nos filles; nous irons avec nos brebis et nos bœufs; car c'est pour nous une fête de l'Éternel.
Mose akajibu, “Tutakwenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na kondoo zetu, ngʼombe, mbuzi, farasi na punda kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Bwana.”
10 Alors il leur dit: Que l'Éternel soit avec vous, comme je vous laisserai aller, vous et vos petits enfants! Prenez garde, car le mal est devant vous!
Farao akasema, “Bwana awe pamoja nanyi, kama nikiwaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
11 Il n'en sera pas ainsi; allez, vous les hommes, et servez l'Éternel; car c'est ce que vous demandiez. Et on les chassa de devant Pharaon.
La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Bwana, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Mose na Aroni wakaondolewa mbele ya Farao.
12 Alors l'Éternel dit à Moïse: Étends ta main sur le pays d'Égypte, pour faire venir les sauterelles, et qu'elles montent sur le pays d'Égypte, et dévorent toute l'herbe de la terre, tout ce que la grêle a laissé.
Basi Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri ili kundi la nzige liweze kuingia juu ya nchi na kutafuna kila kitu kiotacho katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
13 Moïse étendit donc sa verge sur le pays d'Égypte; et l'Éternel amena sur le pays, tout ce jour-là et toute la nuit, un vent d'Orient; le matin vint, et le vent d'Orient avait apporté les sauterelles.
Kwa hiyo Mose akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Bwana akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
14 Et les sauterelles montèrent sur tout le pays d'Égypte, et s'abattirent dans tout le territoire de l'Égypte, en très grand nombre. Il n'y en avait point eu avant elles de semblables, et il n'y en aura point de semblables après elles.
Wakaivamia Misri yote na kukaa kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe hapajapata kuwepo pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwepo tena.
15 Elles couvrirent la face de tout le pays, et le pays en fut obscurci; et elles dévorèrent toute l'herbe de la terre, et tout le fruit des arbres, que la grêle avait laissé; et il ne resta aucune verdure aux arbres, ni aux herbes des champs, dans tout le pays d'Égypte.
Wakafunika ardhi yote mpaka ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kile chote kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe, kila kitu kiotacho mashambani pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
16 Alors Pharaon se hâta d'appeler Moïse et Aaron, et dit: J'ai péché contre l'Éternel votre Dieu, et contre vous.
Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu na dhidi yenu pia.
17 Mais, maintenant, pardonne, je te prie, mon péché, pour cette fois seulement; et intercédez auprès de l'Éternel votre Dieu, pour qu'il éloigne de moi seulement cette mort.
Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Bwana Mungu wako aondoe pigo hili baya kwangu.”
18 Il sortit donc de chez Pharaon, et intercéda auprès de l'Éternel.
Kisha Mose akaondoka kwa Farao akamwomba Bwana.
19 Et l'Éternel ramena un vent d'Occident très fort, qui emporta les sauterelles, et les précipita dans la mer Rouge. Il ne resta pas une seule sauterelle dans tout le territoire de l'Égypte.
Naye Bwana akaugeuza upepo ukavuma kutoka magharibi, wenye nguvu nyingi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
20 Mais l'Éternel endurcit le cœur de Pharaon, et il ne laissa point aller les enfants d'Israël.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
21 Alors l'Éternel dit à Moïse: Étends ta main vers les cieux, et qu'il y ait des ténèbres sur le pays d'Égypte, telles qu'on puisse les toucher.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
22 Moïse étendit donc sa main vers les cieux, et il y eut d'épaisses ténèbres dans tout le pays d'Égypte, pendant trois jours;
Kwa hiyo Mose akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
23 On ne se voyait pas l'un l'autre, et nul ne se leva de sa place, pendant trois jours. Mais pour tous les enfants d'Israël il y eut de la lumière dans le lieu de leurs demeures.
Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi.
24 Alors Pharaon appela Moïse et dit: Allez, servez l'Éternel; que vos brebis et vos bœufs seuls demeurent; vos petits enfants iront aussi avec vous.
Ndipo Farao akamwita Mose na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Bwana. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ngʼombe wenu waacheni.”
25 Mais Moïse répondit: Tu mettras toi-même entre nos mains de quoi faire des sacrifices et des holocaustes, que nous offrirons à l'Éternel notre Dieu.
Lakini Mose akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Bwana Mungu wetu.
26 Et nos troupeaux iront aussi avec nous; il n'en restera pas un ongle. Car nous en prendrons pour servir l'Éternel notre Dieu; et nous ne saurons avec quoi nous devrons servir l'Éternel, que nous ne soyons arrivés là.
Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Bwana Mungu wetu, kwa kuwa mpaka tutakapofika huko hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Bwana.”
27 Mais l'Éternel endurcit le cœur de Pharaon, et il ne voulut point les laisser aller.
Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
28 Et Pharaon lui dit: Va-t'en de devant moi! Garde-toi de revoir ma face, car le jour où tu verras ma face, tu mourras.
Farao akamwambia Mose, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
29 Alors Moïse répondit: Tu as bien dit; je ne reverrai plus ta face.
Mose akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”

< Exode 10 >