< Daniel 11 >

1 Et moi, dans la première année de Darius le Mède, je me tenais auprès de lui pour l'aider et le fortifier.
Katika mwaka wa kwanza wa Dario Mmedi, mimi mwenyewe nilikuja kumwezesha na kumlinda Mikaeli.
2 Maintenant je t'annoncerai la vérité: Voici, il y aura encore trois rois en Perse; puis le quatrième possédera de plus grandes richesses que tous les autres; et quand il sera devenu fort par ses richesses, il soulèvera tout contre le royaume de Javan.
Na sasa nitakufunulia ukweli. Wafalme watatu watainuka katika Uajemi, na mfalme wa nne atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Na wakati atakapopata nguvu kupitia utajiri wake, atamwamsha kila mtu kinyume na ufalme wa Ugiriki.
3 Mais il s'élèvera un roi vaillant, qui dominera avec une grande puissance, et fera ce qu'il voudra.
Mfalme wenye nguvu atainuka ambaye atatawala ufalme mkubwa, na ataenenda kufuatana na matakwa yake mwenyewe.
4 Et dès qu'il se sera élevé, son royaume se brisera et sera divisé vers les quatre vents des cieux, mais il ne passera point à sa postérité, et n'aura pas la même puissance qu'il a exercée; car son royaume sera déchiré et donné à d'autres qu'à ceux-là.
Na atakapokuwa ameinuka, ufalme wake utavunjika na utagawanyika katika pepo nne za mbinguni, lakini hawatakuwa wazao wake mwenyewe, na si kwa nguvu zake kwa wakati alipokuwa akitawala. Kwa kuwa ufalme wake utang'olewa kwa ajili ya wengine tofauti na wazawa wake.
5 Et le roi du midi deviendra fort, mais l'un de ses chefs deviendra plus fort que lui et dominera, et sa domination sera une grande domination.
Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja kati ya maamiri jeshi wake atakuwa mwenye nguvu kuliko yeye na atautawala ufalme wake kwa nguvu kubwa.
6 Et au bout de quelques années ils s'allieront, et la fille du roi du midi viendra vers le roi du nord pour rétablir l'accord. Mais elle ne conservera pas la force du bras, et son bras ne subsistera point; et elle sera livrée, elle et ceux qui l'auront amenée, avec son père et celui qui l'aura soutenue dans ces temps-là.
Baada ya miaka michache, wakati muda utakapokuwa sawa, watafanya mwungano. Binti wa mfalme wa Kusini atakuja kwa mfalme wa Kaskazini kuyathibitisha makubaliano yao. Lakini hataweza kuzitunza nguvu za mkono wake, wala mfalme hatasimama wala mkono wake. Ataachwa na wale waliomleta, na baba yake, na yeye aliyemwunga mkono katika nyakati hizo.
7 Mais un rejeton de ses racines s'élèvera pour le remplacer. Il viendra à l'armée, il entrera dans les forteresses du roi du nord, il agira contre eux, et il sera puissant.
Lakini tawi kutoka katika mizizi yake litachipuka katika nafasi yake. Atalishambulia jeshi na kuingia ngome ya mfalme wa Kaskazini. Atapigana nao, na atawashinda.
8 Et même il transportera en Égypte leurs dieux, avec leurs images de fonte et avec leurs vases précieux d'or et d'argent; puis il se tiendra pendant quelques années éloigné du roi du nord.
Ataichukua miungu yao mpaka Misri pamoa na sanamu zao za chuma na vyombo vyao vya fedha na vya dhahabu vyenye thamani. Kwa miaka mingi atakaa mbali na mfalme wa Kaskazini.
9 Celui-ci marchera contre le royaume du midi, et il retournera dans son pays.
Kisha mfalme wa Kaskazini atauvamia ufalme wa mfalme wa Kusini, lakini atajitoa na kwenda katika nchi yake mwenyewe.
10 Mais ses fils entreront en guerre et rassembleront une grande multitude de troupes; l'un d'eux s'avancera et se répandra comme un torrent; il passera et reviendra, et il portera la guerre jusqu'à la forteresse du roi du midi.
Wana wake watajiweka tayari na kuunganisha jeshi kubwa. Litaendelea kukua na litagharikisha kila kitu, litapita katikati hadi kwenye ngome yake.
11 Et le roi du midi sera irrité; il sortira et combattra contre lui, contre le roi du nord. Et celui-ci mettra sur pied une grande multitude, mais la multitude sera livrée en sa main.
Ndipo mfalme wa Kusini atakasirika, na ataenda na kupigana naye, mfalme wa Kaskazini. Mfalme wa Kaskazini atainua jeshi kubwa, bali jeshi litatiwa katika mkono wake.
12 Cette multitude s'enorgueillira, et le cœur du roi s'élèvera; il fera tomber des milliers, mais il n'en sera pas fortifié.
Jeshi litachukuliwa, na moyo wa mfalme wa Kusini utainuliwa juu, na atawafanya makumi maelfu kuanguka, lakini hataweza kuwa mshindi.
13 Car le roi du nord reviendra et rassemblera une multitude plus nombreuse; et au bout de quelque temps, de quelques années, il viendra avec une grande armée et un grand appareil.
Kisha mfalme wa Kaskazini atainua jeshi jingine, kubwa kuliko la kwanza. Baada ya miaka kadhaa, mfalme wa Kaskazini atakuja na jeshi kubwa likiwa na vifaa vingi.
14 En ce temps-là, plusieurs s'élèveront contre le roi du midi, et des hommes violents de ton peuple s'élèveront, afin d'accomplir la vision, mais ils succomberont.
Katika siku hizo wengi watainuka kinyume na mfalmea wa Kusini. Wana wa vurugu miongoni mwa watu wake watasimama wao wenyewe ili kuyatimiliza maono, lakini watajikwaa.
15 Et le roi du nord viendra, il élèvera des terrasses et prendra les villes fortes; et les bras du midi, ni son peuple d'élite ne pourront résister. Il n'y aura point de force pour résister.
Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima, na kuuteka mji wenye ngome. Majeshi ya Kusini hayataweza kusimama, hata wanajeshi wake bora. Hawatakuwa na nguvu za kusimama.
16 Et celui qui sera venu contre lui fera tout ce qu'il voudra, et il n'y aura personne qui lui résiste; et il s'arrêtera dans le pays de gloire, ayant la destruction dans sa main.
Badala yake, yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake; hakuna yeyote atakayesimama katika njia yake. Atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi wake.
17 Et il concevra le dessein de venir avec la force de tout son royaume, et fera un accord avec le roi du midi, et il lui donnera sa fille pour la perdre; mais cela ne lui réussira pas et ne sera pas pour lui.
Mfalme wa Kaskazini atauelekeza uso wake ili kuja kwa nguvu za ufalme wake wote, na kutakuwa na makubaliano atakayoyafanya na mfalme wa Kusini. Atampatia katika ndoa binti wa wanawake ili kuuharibu ufalme wa Kusini. Lakini mpango huo hautafanikiwa wala kumsaidia.
18 Puis il tournera sa face vers les îles et en prendra plusieurs. Mais un capitaine mettra fin à l'opprobre qu'il lui attirait; il fera retomber sur lui son opprobre.
Baada ya hayo, mfalme atafuatilia nchi za pwani na ataziteka nchi nyingi. Lakini amiri jeshi atakikomesha kiburi chake na atakisababisha kiburi chake kiishe.
19 Et il tournera sa face vers les forteresses de son pays, mais il chancellera, il tombera, et on ne le trouvera plus.
Kisha atafuatilia miji yenye ngome katika nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka; na hatapatikana tena.
20 Et un autre sera établi à sa place, qui fera passer l'exacteur dans l'ornement du royaume; et en peu de jours il sera brisé, et ce ne sera ni par la colère, ni dans la bataille.
Kisha mtu mwingine atainuka katika nafasi ambaye atamfanya mtoza ushuru apite kwa ajili ya ufahari wa ufalme. Lakini katika siku zijazo atakatiliwa mbali, lakini si kwa hasira wala si katika vita.
21 A sa place il s'élèvera un homme méprisé, auquel on ne donnera pas l'honneur de la royauté; mais il viendra inopinément, et il s'emparera de la royauté par des flatteries.
Katika nafasi atainuka mtu wa kudharauliwa ambaye watu hawatampa heshima ya nguvu ya kifalme; atakuja bila kukusudiwa na atautwaa ufalme kwa ulaghai.
22 Et les forces qui submergent seront submergées devant lui et seront brisées, aussi bien que le prince son allié.
Mbele yake, kila jeshi litafutiliwa mbali kama gharika. Jeshi na kiongozi wa agano wataangamizwa wote kwa pamoja.
23 Et après l'accord fait avec lui, il usera de tromperie, et il montera, et il aura le dessus avec peu de gens.
Tangu katika kipindi kile ambacho makubaliano yalifanywa pamoja naye, ataenenda kwa kwa hila; atakuwa mwenye nguvu akiwa na watu wachache tu.
24 Il viendra à l'improviste dans les lieux les plus fertiles de la province, et il fera ce que n'avaient pas fait ses pères, ni les pères de ses pères; il leur distribuera le butin, les dépouilles et les richesses; et il formera des desseins contre les forteresses, et cela pour un temps.
Kwa ghafla ataingia katika sehemu tajiri sana za jimbo, na atafanya kile ambacho si baba yake wala baba wa baba yake alishakifanya. Atagawanya mateka, nyara, na mali zake miongoni mwa wafuasi wake. Atapanga mpango wa kuiangusha ngome, lakini ni kwa muda tu.
25 Puis il réveillera sa force et son courage contre le roi du midi, avec une grande armée. Et le roi du midi s'engagera dans la guerre avec une grande et très forte armée, mais il ne subsistera pas, parce qu'on formera contre lui des complots.
Ataamsha nguvu zake na moyo wake kinyume na mfalme wa Kusini kwa jeshi kubwa. Mfalme wa Kusini atapigana vita akiwa na jeshi kubwa lenye nguvu, lakini hataweza kusimama kwa kuwa wengine watafanya njama dhidi yake.
26 Et ceux qui mangent les mets de sa table le briseront; son armée s'écoulera comme un torrent, et beaucoup d'hommes tomberont blessés à mort.
Hata wale wanaokula chakula chake kizuri watajaribu kumwangamiza. Jeshi lake litakatiliwa mbali kama gharika, na wengi wao watauawa.
27 Et les deux rois chercheront dans leur cœur à se nuire; et à la même table ils parleront avec fausseté. Mais cela ne réussira pas, car la fin ne viendra qu'au temps marqué.
Wafalme wote hawa wawili, wakiwa na mioyo yao imejawa na uovu kinyume na mwenzake, watakaa katika meza moja na kudanganyana, lakini haitakuwa na maana yoyote. Kwa kuwa mwisho utatokea katika kipindi ambacho kimeshapangwa.
28 Il retournera dans son pays avec de grandes richesses; son cœur se déclarera contre l'alliance sainte, et il agira contre elle, puis il retournera dans son pays.
Kisha mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake akiwa na utajiri mkubwa, na moyo wake ukipinga vikali agano takatifu. Atatenda na kisha atarudi katika nchi yake mwenyewe.
29 Au temps marqué, il reviendra et marchera contre le midi; mais cette dernière fois ne sera pas comme la précédente.
Katika muda uloamriwa atarudi na kuushambulia ufalme wa Kusini. Lakini katika kipindi hiki hakitakuwa kama awali.
30 Des navires de Kittim viendront contre lui, et il perdra courage; il s'en retournera, et il sera irrité contre l'alliance sainte et il agira contre elle, il retournera et s'entendra avec ceux qui abandonnent l'alliance sainte.
Kwa kuwa meli kutoka Kitimu zitamshambulia, naye ataogopa na kurudi nyuma. Atakuwa mwenye hasira dhidi ya agano takatifu, na atawaonyesha mema wale watakaoliacha agano takatifu.
31 Et des forces se lèveront de sa part, elles profaneront le sanctuaire, la forteresse, et feront cesser le sacrifice continuel, et mettront l'abomination qui cause la désolation.
Majeshi yake yatainuka na kukufuru sehemu takatifu katika ngome. Wataziondoa sadaka za kawaida za kuteketezwa, na watasimamisha chukizo la uharibifu litakalosababisha ukiwa.
32 Il séduira par des flatteries les prévaricateurs de l'alliance; mais le peuple de ceux qui connaissent leur Dieu prendra courage et agira.
Na kwa wale walioenenda kwa ouvu kinyume na agano, atawadanganya na kuwatia uovu. Bali watu wale wanaomjua Mungu wao watakuwa jasiri na watachukua hatua.
33 Et ceux du peuple qui seront intelligents en instruiront plusieurs; mais il y en aura qui tomberont par l'épée et par la flamme, par la captivité et par le pillage, pendant un certain temps.
Watu wenye hekima miongobi mwa watu watawafanya watu waelewe. Lakini watajikwaa kwa upanga na kwa miali ya moto; watatiwa mateka na kunyang'anywa kwa siku.
34 Et lorsqu'ils seront renversés, ils seront un peu secourus; et plusieurs se joindront à eux par hypocrisie.
Katika siku za kujikwaa kwao, watasaidiwa kwa msaada kidogo. Watu wengi watajiunga nao wenyewe katika unafiki.
35 Et parmi les intelligents, quelques-uns seront renversés, afin qu'il y en ait qui soient éprouvés, purifiés et blanchis, jusqu'au temps de la fin, car elle ne viendra qu'au temps marqué.
Baadhi ya watu wenye hekima watajikwaa ili kujisafisha kutokee kwao, na kujiosha, na kujitakasa, mpaka wakati wa mwisho. Kwa kuwa wakati ulioamriwa haujaja bado.
36 Le roi fera tout ce qu'il voudra; et il s'enorgueillira et s'élèvera au-dessus de tout dieu; il proférera des choses étranges contre le Dieu des dieux; et il prospérera jusqu'à ce que la colère soit consommée, car ce qui est décrété sera exécuté.
Mfalme atafanya kutokana na matakwa yake. Atajiinua mwenyewe na kujifanya mkubwa kuliko kila mungu. Kinyume cha Mungu wa miungu, atasema vitu vibaya, kwa kuwa atafanikiwa mpaka pale ghadhabu itakapokuwa imekamilika. Kwa ajili kile kilichoamriwa kitakapokuwa kimefanyika.
37 Il n'aura égard ni aux dieux de ses pères, ni à l'amour des femmes; il n'aura égard à aucun dieu; car il s'élèvera au-dessus de tout.
Hatazijali miungu ya baba zake wala mungu anayependwa na wanawake. Wala hatamjali mungu mwingine yeyote. Kwa kuwa zaidi ya mtu yeyote atajifanya mwenyewe kuwa mkuu.
38 Mais, à la place, il honorera le dieu des forteresses. Il honorera avec de l'or, de l'argent, des pierres précieuses et avec les choses les plus désirables, un dieu que n'ont pas connu ses pères.
Atamheshimu mungu wa ngome badala ya haya. Ni mungu ambaye baba zake hawakumkubali ambaye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa mawe ya thamani na zawadi zenye kuthaminiwa.
39 Et il agira ainsi dans les remparts des forteresses avec un dieu étranger: à ceux qui le reconnaîtront, il multipliera la gloire; il les fera dominer sur plusieurs et leur partagera le pays en récompense.
Atazishambulia ngome imara sana kwa msaada wa mungu mgeni. Atampa heshima kubwa yeyote anayemkubali. Atawafanya kuwa watawala juu ya watu wengi, na ataigawanya nchi kama thawabu.
40 Et au temps de la fin, le roi du midi se heurtera contre lui; et le roi du nord fondra sur lui comme une tempête, avec des chars et des cavaliers et beaucoup de navires.
Kwa wakati wa mwisho mfalme wa Kusini atamshambulia. Mfalme wa Kaskazini atamvamia kwa ukali wa magari na wapanda farasi, na meli nyingi. Naye ataenda kinyume cha nchi, kuwagharikisha, na kupita katikati.
41 Il entrera dans les terres, se répandra comme un torrent et passera. Il entrera dans le pays de gloire; et plusieurs pays succomberont, mais ceux-ci échapperont de sa main: Édom et Moab et les principaux des enfants d'Ammon.
Naye ataingia katika nchi ya uzuri, makumi elfu ya Waisraeli wataanguka. Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika mkono wake: Waedomu, Wamoabu, na mabaki ya watu wa Amoni.
42 Il étendra sa main sur les pays, et le pays d'Égypte n'échappera point.
Naye ataunyosha mkono katika nchi; nchi ya Misri haitaokolewa.
43 Il se rendra maître des trésors d'or et d'argent et de toutes les choses précieuses de l'Égypte. Les Libyens et les Éthiopiens seront à sa suite.
Atakuwa na mamlaka juu ya hazina za dhahabu na za fedha, na juu ya utajiri wote wa Misri; watu wa Libya na Ethiopia watakuwa chini katika nyayo za miguu yake.
44 Mais des nouvelles de l'orient et du nord viendront le troubler; et il sortira avec une grande fureur pour détruire et exterminer beaucoup de gens.
Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamwogopesha, naye atatoka akiwa mwenye hasira nyingi kuwa ili kuwaharibu kabisa na kuwahifadhi kwa ajli ya uharibifu.
45 Il dressera les tentes de son palais entre les mers, vers la montagne glorieuse et sainte. Puis il viendra à sa fin, et personne ne lui donnera de secours.
Naye ataisimamisha hema ya makao yake ya kifalme kati ya bahari na milima ya uzuri wa utakatifu. Ataufikia mwisho wake, na hapatakuwa na msaidizi wa kumsadia.

< Daniel 11 >