< Daniel 10 >

1 La troisième année de Cyrus, roi de Perse, une parole fut révélée à Daniel, qu'on nommait Beltshatsar; et cette parole est véritable et annonce un grand combat. Et il comprit la parole, et il eut l'intelligence de la vision.
Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
2 En ce temps-là, moi Daniel, je fus dans le deuil pendant trois semaines.
Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
3 Je ne mangeai point de mets délicats; il n'entra dans ma bouche ni viande, ni vin, et je ne m'oignis point jusqu'à ce que les trois semaines fussent accomplies.
Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
4 Et le vingt-quatrième jour du premier mois, j'étais sur le bord du grand fleuve qui est l'Hiddékel.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
5 Et je levai les yeux et je regardai; et voici, je vis un homme vêtu de lin, et dont les reins étaient ceints d'une ceinture d'or fin d'Uphaz.
Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
6 Son corps était comme de chrysolithe, son visage brillait comme un éclair, ses yeux comme des lampes allumées, ses bras et ses pieds paraissaient comme de l'airain poli, et le bruit de ses paroles était comme le bruit d'une multitude.
Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
7 Et moi, Daniel, je vis seul la vision, et les hommes qui étaient avec moi ne la virent point; mais une grande frayeur tomba sur eux, et ils s'enfuirent pour se cacher.
Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
8 Je restai seul, et je vis cette grande vision, et il ne me resta plus de force. Mon visage changea de couleur et fut tout défait, et je ne conservai aucune force.
Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
9 Et j'entendis la voix de ses paroles, et quand je l'eus entendue, je tombai assoupi et la face contre terre.
Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
10 Et voici, une main me toucha et me fit mettre sur mes genoux et sur les paumes de mes mains.
Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
11 Puis il me dit: Daniel, homme bien-aimé, fais attention aux paroles que je te dis, et tiens-toi debout à la place où tu es, car je suis maintenant envoyé vers toi. Et quand il m'eut dit ces paroles, je me tins debout en tremblant.
Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
12 Et il me dit: Ne crains point, Daniel; car dès le jour où tu as pris à cœur de comprendre et de t'humilier devant ton Dieu, tes paroles ont été exaucées, et c'est à cause de tes paroles que je suis venu.
Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
13 Mais le chef du royaume de Perse m'a résisté vingt et un jours; et voici, Micaël, l'un des principaux chefs, est venu à mon aide, et je suis demeuré là auprès des rois de Perse.
Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
14 Et je viens maintenant pour te faire entendre ce qui doit arriver à ton peuple dans les derniers jours; car la vision s'étend jusqu'à ces jours-là.
Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
15 Pendant qu'il m'adressait ces paroles, je tenais mon visage contre terre, et je restais muet.
Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
16 Et voici, quelqu'un qui ressemblait aux fils de l'homme toucha mes lèvres. Alors j'ouvris la bouche, je parlai et je dis à celui qui se tenait devant moi: Mon seigneur, par la vision l'angoisse m'a saisi, et je n'ai conservé aucune force.
Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
17 Et comment le serviteur de mon seigneur pourrait-il parler avec mon seigneur? Maintenant il n'y a plus en moi aucune force, et il ne me reste plus de souffle!
Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
18 Alors celui qui avait l'apparence d'un homme me toucha de nouveau et me fortifia.
Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
19 Et il me dit: Ne crains point, homme bien-aimé; que la paix soit avec toi! Prends courage, prends courage! Et, comme il me parlait, je repris courage, et je dis: Que mon seigneur parle, car tu m'as fortifié.
Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
20 Et il me dit: Sais-tu pourquoi je suis venu vers toi? Et maintenant je m'en retourne pour combattre le chef de Perse; et quand je serai parti, voici, le chef de Javan viendra.
Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
21 Mais je t'annoncerai ce qui est écrit dans le livre de vérité. Et il n'y a personne qui me soutienne contre ceux-là, sinon Micaël, votre chef.
Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”

< Daniel 10 >