< Amos 7 >
1 Le Seigneur, l'Éternel, m'a fait voir ceci: Voici, il formait des sauterelles, au temps où le regain commençait à croître; et voici, le regain poussait après les fenaisons du roi.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua.
2 Et quand elles eurent achevé de dévorer l'herbe de la terre, je dis: Seigneur Éternel pardonne, je te prie! Comment Jacob subsistera-t-il? Car il est petit.
Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
3 L'Éternel se repentit de cela. Cela n'arrivera point, dit l'Éternel.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”
4 Puis le Seigneur, l'Éternel, me fit voir ceci: voici, le Seigneur, l'Éternel, proclamait le jugement par le feu. Et le feu dévorait le grand abîme, et il dévorait les champs.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi.
5 Et je dis: Seigneur Éternel, cesse, je te prie! Comment Jacob subsistera-t-il? Car il est petit.
Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”
6 L'Éternel se repentit de cela. Cela non plus n'arrivera point, dit le Seigneur, l'Éternel.
Kwa hiyo Bwana akaghairi. Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”
7 Puis il me fit voir ceci: voici, le Seigneur se tenait debout sur un mur fait au niveau, et dans sa main était un niveau.
Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake.
8 Et l'Éternel me dit: Que vois-tu, Amos? Et je dis: Un niveau. Et le Seigneur dit: Je mettrai le niveau au milieu de mon peuple d'Israël; je ne lui pardonnerai plus.
Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?” Nikamjibu, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.
9 Les hauts lieux d'Isaac seront ravagés, et les sanctuaires d'Israël seront détruits, et je me lèverai contre la maison de Jéroboam avec l'épée.
“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa, na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa; kwa upanga wangu nitainuka dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”
10 Alors Amatsia, sacrificateur de Béthel, fit dire à Jéroboam, roi d'Israël: Amos conspire contre toi, au milieu de la maison d'Israël; le pays ne saurait souffrir tous ses discours.
Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote.
11 Car voici ce que dit Amos: Jéroboam mourra par l'épée, et Israël sera transporté hors de son pays.
Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema: “‘Yeroboamu atakufa kwa upanga, na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”
12 Et Amatsia dit à Amos: Voyant, va, enfuis-toi au pays de Juda, et manges-y ton pain, et là tu prophétiseras.
Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako.
13 Mais ne continue plus de prophétiser à Béthel, car c'est le sanctuaire du roi, et c'est la maison royale.
Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”
14 Et Amos répondit, et dit à Amatsia: Je n'étais ni prophète, ni fils de prophète; j'étais un berger, et je recueillais des figues sauvages.
Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu.
15 Or l'Éternel m'a pris derrière le troupeau, et l'Éternel m'a dit: Va, prophétise à mon peuple d'Israël.
Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’
16 Et maintenant écoute la parole de l'Éternel. Tu dis: Ne prophétise pas contre Israël, et ne parle pas contre la maison d'Isaac.
Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema, “‘Usitabiri dhidi ya Israeli, na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’
17 C'est pourquoi ainsi a dit l'Éternel: Ta femme se prostituera dans la ville; tes fils et tes filles tomberont par l'épée; ton champ sera partagé au cordeau; et toi, tu mourras sur une terre souillée, et Israël sera transporté hors de son pays.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “‘Mke wako atakuwa kahaba mjini, nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga. Shamba lako litapimwa na kugawanywa, na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani. Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni, mbali na nchi yao.’”