< 2 Samuel 8 >

1 Après cela David battit les Philistins et les abaissa; et David enleva Méthegamma des mains des Philistins.
ikawa baada ya haya Daudi aliwashambulia Wafilisti na kuwashinda. Hivyo Daudi akaichukua Gathi na vijiji vyake kutoka katika mamlaka ya wafilisti.
2 Il battit aussi les Moabites, et les mesura au cordeau, en les faisant coucher par terre; il en mesura deux cordeaux pour les faire mourir, et un plein cordeau pour leur laisser la vie; et les Moabites furent soumis à David et ses tributaires.
Kisha akaishinda Moabu na akawapima watu wake kwa mstari kwa kuwafanya walale chini juu ya ardhi. Alipima mistari miwili ya kuua, na mstari mmoja kamili kuwahifadhi hai. Hivyo Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakaanza kumlipa kodi.
3 David battit aussi Hadadézer, fils de Réhob, roi de Tsoba, comme il allait rétablir sa domination sur le fleuve de l'Euphrate.
Kisha Daudi akamshinda Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, Hadadezeri aliposafiri kuurudisha ufalme wake katika mto Frati.
4 Et David lui prit dix-sept cents cavaliers, et vingt mille hommes de pied; et il coupa les jarrets aux chevaux de tous les chars, mais il en réserva cent chars.
Daudi aliteka magari 1, 700 ya farasi na askari ishirini elfu waendao kwa miguu. Daudi akawakata miguu farasi wa magari, lakini akahifadhi wakutosha magari mia moja.
5 Or les Syriens de Damas vinrent au secours de Hadadézer, roi de Tsoba; et David battit vingt-deux mille Syriens.
Wakati Washami wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadeziri mfalme wa Soba, Daudi akaua katika Washami watu ishirini na mbili elfu.
6 Puis David mit des garnisons dans la Syrie de Damas, et les Syriens furent soumis à David et ses tributaires. Et l'Éternel gardait David partout où il allait.
Daudi akaweka ngome huko Shamu ya Dameski, na Washami wakawa watumishi wake na wakaleta kodi. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alikokwenda.
7 Et David prit les boucliers d'or qu'avaient les serviteurs de Hadadézer, et les apporta à Jérusalem.
Daudi akachukua ngao za dhahabu walizokuwa nazo watumishi wa Hadadezeri naye akazileta Yerusalemu.
8 Le roi David emporta aussi une très grande quantité d'airain de Bétach et de Bérothaï, villes de Hadadézer.
Mfalme Daudi akachukua shaba nyingi kutoka Beta na Berosai, miji ya Hadadezeri.
9 Or Thoï, roi de Hamath, apprit que David avait défait toutes les forces de Hadadézer.
Wakati Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 Et il envoya Joram, son fils, vers le roi David, pour le saluer, et pour le bénir de ce qu'il avait fait la guerre contre Hadadézer et de ce qu'il l'avait défait. Car Hadadézer était continuellement en guerre avec Thoï. Et Joram apporta des vases d'argent, des vases d'or et des vases d'airain,
Tou akamtuma Hadoramu mwanawe kwa mfalme Daudi kumpa salamu na kumbariki, kwa kuwa Daudi alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda, maana Hadadezeri alikuwa amepiga vita dhidi ya Tou. Hadoramu akaja pamoja na vitu vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 Que David consacra à l'Éternel, avec l'argent et l'or qu'il avait déjà consacrés, du butin de toutes les nations qu'il s'était assujetties,
Mfalme Daudi akaviweka wakfu vitu hivi kwa ajili ya Yahwe, pamoja na fedha na dhahabu kutoka katika mataifa yote aliyokuwa ameyashinda-
12 De la Syrie, de Moab, des enfants d'Ammon, des Philistins, d'Amalek, et du butin de Hadadézer, fils de Réhob, roi de Tsoba.
kutoka Shamu, Moabu, Waamoni, Wafilist, Waamaleki, pamoja na nyara zote alizoziteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 David s'acquit encore du renom, à son retour de la défaite des Syriens, en battant, dans la vallée du Sel, dix-huit mille Iduméens,
Jina la Daudi likajulikana sana alipowashinda washami katika bonde la Chumvi, pamoja na watu wao wapatao elfu kumi na nane.
14 Et il mit des garnisons dans l'Idumée; il mit des garnisons dans toute l'Idumée, et l'Idumée entière fut soumise à David. Et l'Éternel gardait David partout où il allait.
Akaweka ngome katika Edomu yote, na Waedomu wote wakawa watumishi wake. Yahwe akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 Ainsi David régna sur tout Israël, faisant droit et justice à tout son peuple.
Daudi akatawala juu ya Israeli yote, naye akatenda kwa haki na usawa kwa watu wote.
16 Et Joab, fils de Tséruja, commandait l'armée; et Josaphat, fils d'Achilud, était archiviste;
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwenye kuandika taarifa.
17 Et Tsadok, fils d'Achitub, et Achimélec, fils d'Abiathar, étaient sacrificateurs, et Séraja, secrétaire;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi.
18 Et Bénaja, fils de Jéhojada, était sur les Kéréthiens et les Péléthiens, et les fils de David étaient ses principaux officiers.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >