< 2 Samuel 23 >

1 Or ce sont ici les dernières paroles de David. David, fils d'Isaï, l'homme qui a été élevé, qui a été l'oint du Dieu de Jacob, et le chantre aimé d'Israël, dit:
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi-Daudi mwana wa Yese, mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwandishi mzuri wa zaburi wa Israeli.
2 L'Esprit de l'Éternel a parlé par moi, et sa parole a été sur ma langue.
“Roho ya Yahwe alisema nami, na neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 Le Dieu d'Israël a dit, le rocher d'Israël a parlé de moi: Celui qui règne parmi les hommes avec justice, qui règne dans la crainte de Dieu,
Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli aliniambia, “Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu.
4 Est pareil à la lumière du matin, lorsque le soleil se lève, en un matin sans nuages; son éclat fait germer de la terre la verdure après la pluie.
Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua linapochomoza, asubuhi isiyo na mawingu, wakati mche mwororo unapochipua kutoka ardhini kupitia mwangaza wa mng'ao wa jua baada ya mvua.
5 N'en est-il pas ainsi de ma maison devant Dieu? Car il a fait avec moi une alliance éternelle, bien ordonnée, assurée. Tout mon salut, tout ce que j'aime, ne le fera-t-il pas fleurir?
Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu? Je hajafanya nami agano la milele, taratibu la uhakika kwa kila njia? Je yeye haongezi wokovu wangu na kutimiza kila hitaji langu?
6 Mais les méchants seront tous comme des épines qu'on jette au loin; car on ne les prend pas avec la main,
Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali, kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono.
7 Mais celui qui les veut manier, s'arme d'un fer ou du bois d'une lance, et on les brûle au feu sur la place même.
Ayagusaye ni lazima atumie chombo cha chuma au au fumo la mkuki. Ni lazima yachomwe mahali yalipo.
8 Ce sont ici les noms des hommes vaillants qu'avait David: Josheb-Bashébeth, Tachkémonite, était chef des meilleurs guerriers. C'est lui qui leva sa lance sur huit cents hommes qu'il tua en une seule occasion.
Haya ni majina ya askari wa Daudi: Yashobeamu Mhakmoni alikuwa kiongozi wa mashujaa. Aliua watu mia nne wakati mmoja.
9 Après lui était Éléazar, fils de Dodo, fils d'Achochi; l'un des trois vaillants hommes qui étaient avec David, lorsqu'ils défièrent les Philistins assemblés pour combattre, et que ceux d'Israël montèrent.
Baada yake alikuwa Elieza mwana wa Dodo, mwana wa mwahohi, mmoja wa mashujaa watatu wa Daudi. Alikuwepo walipowashinda Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kwa vita, na wakati watu wa Israeli walipokuwa wamekimbia.
10 Il se leva, et frappa les Philistins jusqu'à ce que sa main en fût lasse, et demeurât attachée à son épée. En ce jour-là l'Éternel accorda une grande délivrance, et le peuple revint après Éléazar, seulement pour prendre les dépouilles.
Elieza akasimama na kuwapiga Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka, mpaka mkono wake ukang'ang'ania mpini wa upanga wake. Siku hiyo Yahwe akatoa ushindi mkuu. Jeshi likarejea kwa ajili ya kuteka tu nyara za waliouawa na Elieza.
11 Après lui venait Shamma, fils d'Agué, Hararite. Les Philistins s'étaient rassemblés en troupe; et il y avait là une pièce de terre pleine de lentilles; or le peuple fuyait devant les Philistins;
Baada yake alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti wakajikusanya pamoja palipokuwa na shamba la dengu, na jeshi likawakimbia.
12 Mais il se tint au milieu du champ, le défendit, et frappa les Philistins. Ainsi l'Éternel accorda une grande délivrance.
Lakini Shama akasimama katikati ya shamba na kulitetea. Aliwauwa Wafilisti, na Yahwe akaleta ushindi mkuu.
13 Trois des trente chefs descendirent et vinrent, au temps de la moisson, vers David, dans la caverne d'Adullam, lorsqu'une troupe de Philistins était campée dans la vallée des Réphaïm (des géants).
Watatu kati ya askari thelathini walishuka kwa Daudi nyakati za mavuno, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Mrefai.
14 David était alors dans la forteresse, tandis qu'une garnison de Philistins était à Bethléhem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, wakati Wafilisti walikuwa wanaimilk Bethlehemu.
15 Et David fit un souhait, et dit: Qui me fera boire de l'eau du puits qui est à la porte de Bethléhem?
Daudi alitamani maji na akasema, “Kama ingekuwa mtu mmoja angenipa maji ya kunywa kutoka kisima kilichopo Bethlehemu, kisima kilichopo langoni!”
16 Alors ces trois hommes vaillants passèrent au travers du camp des Philistins, et puisèrent de l'eau du puits qui est à la porte de Bethléhem; et, l'ayant apportée, ils la présentèrent à David; mais il n'en voulut point boire, et il la répandit devant l'Éternel.
Hivyo mashujaa hawa watatu wakapita kati ya jeshi la Wafilisti na kuchota maji katika kisima cha Bethlehemu, kilichopo langoni. Wakachukua maji na kuyaleta kwa Daudi, lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake akayamwaga mbele za Yahwe.
17 Et il dit: Loin de moi, ô Éternel, de faire une telle chose! N'est-ce pas le sang de ces hommes, qui sont allés au péril de leur vie? Et il n'en voulut point boire. Voilà ce que firent ces trois vaillants hommes.
Kisha akasema, “Iwe mbali nami, Yahwe, kwamba niyanywe haya. Je ninywe damu ya watu waliohatarisha maisha yao?” Hivyo akakataa kuyanywa. Haya ni mambo yaliyofanywa na mashujaa watatu.
18 Abishaï, frère de Joab, fils de Tséruja, était le chef des trois. Ce fut lui qui brandit sa lance contre trois cents hommes, qu'il frappa à mort; et il s'acquit un nom parmi les trois.
Abishai, nduguye Yoabu na mwana wa Seruya, alikuwa akida wa watatu. Alipigana kwa mkuki wake na watu mia tatu na akawauwa wote mara. Mara kwa mara alitajwa kati ya mashujaa watatu.
19 Il était le plus considéré des trois, et il fut leur chef; cependant il n'égala point les trois premiers.
Hakuwa maarufu kuliko wale watatu? Alifanywa akida wao. Lakini, umaarufu wake haukulingana na umaarufu wa wale mashujaa watatu.
20 Puis Bénaja, fils de Jéhojada, fils d'un homme vaillant, grand par ses exploits, de Kabtséel; il tua deux des plus puissants hommes de Moab; il descendit aussi, et tua un lion au milieu d'une fosse, en un jour de neige.
Benaya kutoka Kabseeli mwana wa Yehoyada; alikuwa mtu hodari aliyefanya matendo makuu. Aliwauwa wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka shimoni na kuuwa simba wakati wa theruji.
21 Ce fut lui qui frappa un homme égyptien d'un aspect redoutable. Cet Égyptien avait en sa main une lance, et Bénaja descendit contre lui avec un bâton; il arracha la lance de la main de l'Égyptien, et le tua de sa propre lance.
Na alimwua Mmisri aliyekuwa mtu mnene sana. Mmisri alikuwa na mkuki mkononi, lakini Benaya alipigana naye kwa fimbo tu. Aliuchukua mkuki mkononi mwa Mmisri na kisha kumwua nao.
22 Voilà ce que fit Bénaja, fils de Jéhojada; et il eut un nom parmi ces trois hommes vaillants.
Benaya mwana wa Yehoyada alifanya matendo haya, naye alitajwa kati ya mashujaa watatu.
23 Il fut plus honoré que les trente; mais il n'égalait pas les trois premiers. Et David le mit en son conseil privé.
Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu. Hata hivyo Daudi alimweka kuwa mlinzi wake.
24 Asaël, frère de Joab, parmi les trente. Elchanan, fils de Dodo, de Bethléhem;
Wafuatao ni wale watu thelathini: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
25 Shamma, Harodite; Elika, Harodite;
Shama Mharodi, Elika Mharodi,
26 Hélets, Paltite; Ira, fils de Ikkèsh, Thékoïte;
Helesi Mpeloni, Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi,
27 Abiézer, Anathothite; Mébunnaï, Hushathite;
Abi Ezeri Mwanathothi, Mebunai Mhushathi,
28 Tsalmon, Achochite; Maharaï, Nétophathite;
Salmoni Mhahoi, Maharai Mnetofathi;
29 Héleb, fils de Baana, Nétophathite; Ittaï, fils de Ribaï de Guibea, des enfants de Benjamin;
Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi, Itai mwana wa Rabai kutoka Gibea ya Wabenjamini,
30 Bénaja, Pirathonite; Hiddaï, de Nachalé-Gaash;
Benaya Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya Gaashi.
31 Abi-Albon, Arbathite; Azmaveth, Barchumite;
Abieliboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi,
32 Eliachba, Shaalbonite; des enfants de Jashen, Jonathan;
Eliaba Mshalboni, wana wa Yasheni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
33 Shamma, Hararite; Achiam, fils de Sharar, Ararite;
Ahiamu mwana wa Sharari Mharari,
34 Éliphélet, fils d'Achasbaï, fils d'un Maacathite; Éliam, fils d'Achithophel, Guilonite;
Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni,
35 Hetsraï, Carmélite; Paaraï, Arbite;
Hezro Mkarmeli, Parai Mwarbi,
36 Jiguéal, fils de Nathan, de Tsoba; Bani, Gadite;
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, Bani kutoka kabila la Gadi,
37 Tsélek, Ammonite; Naharaï, Beérothite, qui portait les armes de Joab, fils de Tséruja;
Zeleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
38 Ira, Jithrite; Gareb, Jithrite;
Ira Mwithri, Garebu Mwithri,
39 Urie, Héthien; en tout trente-sept.
Uria Mhiti - jumla yao thelathini na wanane.

< 2 Samuel 23 >