< 2 Samuel 13 >

1 Après cela il arriva qu'Absalom, fils de David, ayant une sœur qui était belle et qui se nommait Tamar, Amnon, fils de David, l'aima.
Ikawa baada ya hayo kwamba Amnoni mwana wa Daudi, akamtamani sana Tamari dada yake wa kambo aliyekuwa mzuri, alikuwa tumbo moja na Absalome, mwana wingine wa Daudi.
2 Et Amnon était tourmenté jusqu'à se rendre malade, à cause de Tamar, sa sœur; car elle était vierge, et il semblait trop difficile à Amnon de rien obtenir d'elle.
Amnoni akasononeka sana kiasi cha kuugua kwa ajili ya Tamari dada yake. Tamari alikuwa bikra, na hivyo ilionekana haiwezekani Amnoni kufanya neno lolote kwake.
3 Or Amnon avait un ami nommé Jonadab, fils de Shimea, frère de David; et Jonadab était un homme fort adroit.
Lakini Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi.
4 Et il lui dit: Fils du roi, pourquoi dépéris-tu ainsi de jour en jour? Ne me le déclareras-tu pas? Amnon lui dit: J'aime Tamar, la sœur de mon frère Absalom.
Yehonadabu alikuwa mtu mwelevu sana. Akamwambia Amnoni, “Kwa nini, mwana wa mfalme, unadhoofika kila siku? Kwa nini uniambii? Ndipo Amnoni akamjibu, “Nampenda Tamari, dada yake Absalome ndugu yangu.”
5 Et Jonadab lui dit: Couche-toi sur ton lit, et fais le malade; et quand ton père viendra te voir, tu lui diras: Je te prie, que ma sœur Tamar vienne, et qu'elle me donne à manger; qu'elle apprête devant moi quelque mets, afin que je le voie, et que je le mange de sa main.
Ndipo Yehonadabu akamwambia, “Lala kitandani mwako na ujifanye kuwa mgonjwa. Wakati baba yako atakapo kuja kukuona, mwambie, Tafadhari mtume dada yangu Tamari aandaye chakula mbele yangu, ili kwamba nikione na kula kutoka mkononi mwake?”
6 Amnon se coucha donc et fit le malade; et le roi vint le voir, et Amnon dit au roi: Je te prie, que ma sœur Tamar vienne et fasse deux gâteaux devant moi, et que je les mange de sa main.
Hivyo Amnoni akalala na kujifanya kuwa mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia mfalme, “Tafadhari mtume Tamari dada yangu aandaye chakula kwa ajili ya ugonjwa wangu mbele yangu ili kwamba nikile kutoka mkononi mwake.
7 Et David envoya dire à Tamar dans la maison: Va dans la maison de ton frère Amnon, et apprête-lui quelque chose à manger.
Ndipo Daudi katika kasri lake akatuma neno kwa Tamari, kusema, “Nenda katika nyumba ya nduguyo Amnoni na umwandalie chakula. Hivyo
8 Et Tamar s'en alla dans la maison d'Amnon, son frère, qui était couché. Et elle prit de la pâte, et la pétrit, et elle en fit devant lui des gâteaux, et les fit cuire.
Tamari akaenda katika nyumba ya Amnoni nduguye alipokuwa amelala. Akachukua donge na kulifinyanga na kuandaa mkate mbele zake, kisha akauoka.
9 Puis elle prit la poêle et les versa devant lui; mais Amnon refusa d'en manger, et il dit: Faites retirer tous ceux qui sont auprès de moi. Et chacun se retira.
Akachukua kikaangio na kumpa mkate, lakini akakataa kula. Kisha Amnoni akawambia waliokuwepo, “Kila mtu na aondoke.” Hivyo kila mmoja akaondoka.
10 Alors Amnon dit à Tamar: Apporte-moi dans la chambre ce que tu m'as apprêté, et que j'en mange de ta main. Et Tamar prit les gâteaux qu'elle avait faits, et les apporta à Amnon, son frère, dans la chambre.
Amnoni akamwambia Tamari, “Lete chakula chumbani kwangu nikile katika mkono wako.” Tamari akachukua mkate aliokuwa ameuandaa, na kuuleta katika chumba cha Amnoni kaka yake.
11 Et elle les lui présenta afin qu'il en mangeât; mais il se saisit d'elle et lui dit: Viens, couche avec moi, ma sœur.
Alipoleta chakula kwake, Amnoni akamshikilia na kumwambia, “Njoo, ulale nami, dada yangu.”
12 Et elle lui répondit: Non, mon frère, ne me fais pas violence, car cela ne se fait point en Israël; ne commets pas cette infamie.
Yeye akamjibu, “Hapana, kaka yangu, usinilazimishe, kwani hakuna jambo kama hili linapaswa kufanyika katika Israeli. Usifanye jambo la aibu kiasi hiki!
13 Et moi, où irais-je porter mon opprobre? Et toi, tu serais comme l'un des infâmes, en Israël. Maintenant donc, parles-en, je te prie, au roi, et il n'empêchera point que tu ne m'aies pour femme.
Nitakwenda wapi ili nijiepushe na aibu ambayo jambo hili litaileta juu ya maisha yangu? Na tendo hili litakuonesha kuwa mpumbavu usiye na aibu katika Israeli yote. Tafadhari, ninakuomba uongee na mfalme. Yeye atakuruhusu unioe.”
14 Mais il ne voulut point l'écouter, et il fut plus fort qu'elle; il lui fit violence et coucha avec elle.
Lakini Amnoni hakuweza kumsikiliza. Kwa kuwa alikuwa zaidi akamkamata na akalala naye.
15 Puis Amnon eut pour elle une très grande haine; et la haine qu'il lui porta fut plus grande que l'amour qu'il avait eu pour elle. Ainsi Amnon lui dit: Lève-toi, va-t'en!
Kisha Amnoni akamchukia Tamari kwa chuki kuu. Akamchukia zaidi ya jinsi alivyokuwa amemtamani. Amnoni akamwambia, “Inuka na uondoke.”
16 Et elle lui dit: Ne me fais pas ce mal-là, plus grand que l'autre que tu m'as fait, de me chasser! Mais il ne voulut pas l'écouter;
Lakini yeye akamjibu, “Hapana! kwa maana uovu wa kunifanya ni uondoke ni mbaya zaidi ya kile ulichonitenda!” Lakini Amnoni hakumsikiliza.
17 Et, appelant le valet qui le servait, il dit: Qu'on chasse cette femme loin de moi, qu'on la mette dehors, et ferme la porte après elle!
Badala yake, akamwita mtumishi wake na akasema, “Mwondoe mwanamke huyu mbele yangu, na uufunge mlango nyuma yake.”
18 Or elle était vêtue d'une robe bigarrée, car les filles vierges du roi étaient ainsi habillées. Celui qui servait Amnon la fit donc sortir, et ferma la porte après elle.
Hivyo mtumishi wake akamtoa na kufunga mlango. Tamari alikuwa amevaa vazi lilinakishiwa kwani ndivyo binti za wafalme waliobikra valivyokuwa wakivaa.
19 Alors Tamar prit de la cendre sur sa tête, et déchira la robe bigarrée qu'elle avait sur elle; elle mit la main sur sa tête, et elle s'en allait en criant.
Tamari akaweka majivu juu ya kichwa chake na akalirarua vazi lake
20 Et son frère Absalom lui dit: Amnon, ton frère, a été avec toi? Maintenant, ma sœur, tais-toi, c'est ton frère; ne prends point ceci à cœur. Ainsi Tamar demeura désolée dans la maison d'Absalom, son frère.
Absalome, kaka yake, akamwambia, “Amnoni, kaka yako, amekuwa nawe? Lakini sasa nyamaza, dada yangu. Yeye ni kaka yako. Usiliweke hili moyoni.” Hivyo Tamari akakaa peke yake katika nyumba ya Absalomu kaka yake.
21 Le roi David apprit toutes ces choses, et il en fut fort irrité.
Mfalme Daudi aliposikia haya yote, alikasirika sana.
22 Or Absalom ne parlait ni en bien ni en mal à Amnon; car Absalom haïssait Amnon, parce qu'il avait outragé Tamar, sa sœur.
Absalome hakusema chochote kwa Amnoni, kwa maana Absalome alimchukia kwa kile alichokifanya, kumdhalilisha Tamari, dada yake.
23 Et il arriva, deux ans après, qu'Absalom ayant les tondeurs à Baal-Hatsor, qui est près d'Éphraïm, il invita tous les fils du roi.
Ikawa baada ya miaka miwili mizima Absalomu akawa na wakatao kondoo manyoya wakifanya kazi huko Baali Hazori, ulioko karibu na Efraim, naye Absalomu akawaarika wana wote wa mfalme kufika huko.
24 Et Absalom vint vers le roi, et dit: Voici, ton serviteur a les tondeurs; je te prie donc, que le roi et ses serviteurs viennent chez ton serviteur.
Absalomu akamwendea mfalme na kusema, “Tazama sasa, mtumishi wako anao wakatao kondoo manyoya. Tafadhari, naomba mfalme na watumishi wake waende nami, mtumishi wako.”
25 Mais le roi dit à Absalom: Non, mon fils, non; nous n'irons pas tous, de peur que nous ne te soyons à charge; et bien qu'Absalom le pressât fort, il n'y voulut point aller; et il le bénit.
Mfalme akamjibu Absalomu, “hapana mwanangu, tusiende sisi yote kwani tutakuwa mzigo kwako.” Absalomu akamhakikishia mfalme, lakini yeye asikubali kwenda, ila alimbariki Absalomu.
26 Alors Absalom dit: Si tu ne viens pas, je te prie, que mon frère Amnon vienne avec nous. Et le roi lui répondit: Pourquoi irait-il avec toi?
Kisha Absalomu akasema, “kama sivyo, basi tafadhari mwache ndugu yangu Amnoni aende nasi.” Mfalme akamuliza, “Kwa nini Amnoni aende nanyi?”
27 Mais Absalom le pressa tant qu'il laissa aller Amnon, et tous les fils du roi avec lui.
Absalomu akamsihi Daudi, hivyo akamruhusu Amnoni na wana wengine wa mfalme kwenda naye.
28 Or, Absalom donna ordre à ses serviteurs, et leur dit: Prenez garde, quand le cœur d'Amnon sera égayé par le vin, et que je vous dirai: Frappez Amnon! alors tuez-le, ne craignez point; n'est-ce pas moi qui vous le commande? Fortifiez-vous et soyez vaillants.
Absalomu akawaamuru watumishi wake kusema, “Sikilizeni kwa makini. Amnoni atakapokuwa amelewa mvinyo, na nitakapowambia, 'Mpigeni Amnoni,' msiogope mwueni. Je siyo mimi niliyewamru? Mwe jasiri na hodari.”
29 Et les serviteurs d'Absalom firent à Amnon comme Absalom l'avait commandé; alors tous les fils du roi se levèrent, et montèrent chacun sur sa mule, et s'enfuirent.
Hivyo watumishi wa Absalome wakamtendea Amnoni kama walivyoamriwa. Kisha wana wote wa mfalme wakainuka na kila mmoja akapanda nyumbu wake akakimbia.
30 Or, comme ils étaient en chemin, le bruit parvint jusqu'à David qu'Absalom avait tué tous les fils du roi, et qu'il n'en était pas resté un seul.
Hata ikawa wakati wakiwa njiani habari zikafika kwa Daudi kusema, “Absalomu ameua wana wote wa mfalme na hakuna hata mmoja aliyesalia.”
31 Alors le roi se leva et déchira ses vêtements, et se coucha par terre; tous ses serviteurs aussi se tenaient là avec leurs vêtements déchirés.
Kisha mfalme akainuka na kurarua mavazi yake na kujilaza juu ya sakafu; watumishi wake wote wakasimama karibu naye mavazi yao yameraruriwa.
32 Et Jonadab, fils de Shimea, frère de David, prit la parole et dit: Que mon seigneur ne dise point qu'on a tué tous les jeunes gens, fils du roi; car Amnon seul est mort; et c'était là le dessein d'Absalom depuis le jour où Amnon outragea Tamar sa sœur.
Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi, akajibu na kusema, “Bwana wangu asidhani kuwa vijana wote ambao ni wana wa mfalme wameuawa, kwa maana ni Amnoni pekee ndiye aliyeuawa. Absalomu alilipanga jambo hili tangu siku ile Amnoni alivyomwaribu Tamari, dada yake.
33 Maintenant donc, que le roi mon seigneur ne prenne point la chose à cœur, en disant: Tous les fils du roi sont morts; car Amnon seul est mort.
Kwa hiyo basi, bwana wangu mfalme asiiweke taarifa hii moyoni, kudhani kwamba wana wote wa mfalme wameuawa, kwani aliyeuawa ni Amnoni peke yake.”
34 Or Absalom s'était enfui. Et le jeune homme qui était en sentinelle, leva les yeux et regarda; et voici que par la route opposée une grande troupe s'avançait sur le flanc de la montagne.
Absalomu akakimbia. Mtumishi aliyekuwa akiangalia akainua macho yake na kuona watu wengi wakija njiani kando ya kilima upande wake wa magharibi.
35 Et Jonadab dit au roi: Voici les fils du roi qui viennent; la chose est arrivée comme ton serviteur a dit.
Kisha Yehonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wanakuja. kama mtumishi wako alivyosema.”
36 Et comme il achevait de parler, on vit arriver les fils du roi, et ils élevèrent la voix et pleurèrent. Le roi aussi et tous ses serviteurs pleurèrent abondamment.
Ikawa mara alipomaliza kusema wana wa mfalme wakafika, wakainua sauti zao na kulia. Na mfalme pamoja na watumishi wake wote pia wakalia kwa uchungu.
37 Mais Absalom s'enfuit, et se retira chez Thalmaï, fils d'Ammihud, roi de Gueshur. Et David pleurait tous les jours sur son fils.
Lakini Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Mfalme akaomboleza kila siku kwa ajili ya mwanaye.
38 Or Absalom, s'étant enfui, alla à Gueshur, et y resta trois ans;
Hivyo Absalomu akakimbia na kwenda Geshuri na akakaa huko kwa miaka mitatu.
39 Et le roi David cessa de poursuivre Absalom, parce qu'il était consolé de la mort d'Amnon.
Moyo wa mfalme Daudi ukatamani kwenda kumwona Absalomu, kwa maana alikuwa amefarijika kwa habari ya kifo cha Amnoni.

< 2 Samuel 13 >