< 2 Samuel 11 >
1 L'an d'après, au temps où les rois se mettaient en campagne, David envoya Joab, et avec lui ses serviteurs et tout Israël; et ils ravagèrent le pays des enfants d'Ammon et assiégèrent Rabba. Mais David demeura à Jérusalem.
Ikawa wakati wa majira ya kipupwe, wakati ambapo kwa kawaida wafalme huenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu, mtumishi wake, na jeshi lote la Israeli. Wakaliaribu jeshi la Amoni na kuuhusuru Raba. Lakini Daudi akakaa Yerusalemu.
2 Et il arriva, sur le soir, que David se leva de dessus son lit; et comme il se promenait sur la plate-forme du palais royal, il vit de cette plate-forme une femme qui se baignait, et cette femme était fort belle à voir.
Hivyo ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi akaamka kutoka kitandani na akatembea katika dari la kasri. Akiwa pale akamwona mwanamke aliyekuwa akioga, mwanamke yule alikuwa mzuri sana kwa mwonekano.
3 Et David envoya demander qui était cette femme, et on lui dit: N'est-ce pas Bath-Shéba, fille d'Éliam, femme d'Urie, le Héthien?
Hivyo Daudi akatuma na kuuliza watu waliomfahamu yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, “Je huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, naye si mke wa Uria mhiti?
4 Et David envoya des messagers, et l'enleva. Elle vint vers lui, et il coucha avec elle; or elle était nettoyée de sa souillure; puis elle s'en retourna dans sa maison.
Daudi akatuma wajumbe nao wakamchukua; akaja kwake, na akalala naye(kwani ndo alikuwa amejitakasa kutoka siku zake). Kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Or cette femme conçut, et elle envoya l'annoncer à David, en lui disant: Je suis enceinte.
Mwanamke akawa mjamzito, naye akatuma na kumwambia Daudi; akasema, “mimi ni mjamzito.”
6 Alors David fit dire à Joab: Envoie-moi Urie, le Héthien. Joab envoya donc Urie vers David.
Kisha Daudi akatuma watu kwa Yoabu kusema, “Umtume kwangu Uria mhiti.” Hivyo Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
7 Et Urie vint à lui, et David l'interrogea sur l'état de Joab et du peuple, et sur l'état de la guerre.
Uria alipofika, Daudi akamuuliza hali ya Yoabu. Jinsi jeshi lilivyokuwa likiendelea, na jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
8 Puis David dit à Urie: Descends dans ta maison et te lave les pieds. Urie sortit donc de la maison du roi, et il fut suivi d'un présent royal.
Daudi akamwambia Uria, “Shuka nyumbani kwako, unawe miguu yako. “Hivyo Uria akaondoka katika kasri la mfalme, mfalme akamtumia zawadi kwa Uria.
9 Mais Urie dormit à la porte de la maison du roi, avec tous les serviteurs de son seigneur, et ne descendit point dans sa maison.
Lakini Uria akalala pamoja na watumishi wa bwana wake katika lango la kasri, wala hakushuka nyumbani kwake.
10 Et on le rapporta à David, et on lui dit: Urie n'est pas descendu dans sa maison. Et David dit à Urie: Ne viens-tu pas de voyage? Pourquoi n'es-tu pas descendu dans ta maison?
Daudi alipoambiwa, “Uria hakushuka nyumbani kwake,” akamwambia Uria, Je haukutoka safarini? Kwa nini haukushuka nyumbani kwako?”
11 Et Urie répondit à David: L'arche, et Israël et Juda logent sous des tentes; mon seigneur Joab aussi et les serviteurs de mon seigneur campent aux champs; et moi j'entrerais dans ma maison pour manger et boire, et pour coucher avec ma femme? Tu es vivant, et ton âme vit, que je ne saurais faire une telle chose!
Uria akamjibu Daudi, “Sanduku, na Israeli na Yuda wamo kwenye mahema, na Yoabu na watumishi wa bwana wangu wamepiga hema uwandani. Jinsi gani basi mimi naweza kwenda nyumbani kwangu kula kunywa na kulala na mke wangu? kwa hakika kama uishivyo, sitafanya hivyo.
12 Et David dit à Urie: Demeure encore ici aujourd'hui, et demain je te renverrai. Urie resta donc à Jérusalem ce jour-là et le lendemain.
Hivyo Daudi akamwambia Uria, “Ukae leo pia, kesho nitakuacha uende.” Kwa hiyo uria akakaa Yerusalemu siku hiyo na iliyofuata.
13 Puis David l'appela, et il mangea et but devant lui, et David l'enivra; mais le soir il sortit pour coucher dans son lit, avec les serviteurs de son maître, et ne descendit point dans sa maison.
Daudi alipomwita, alikula na kunywa pamoja naye, Daudi akamfanya alewe. Wakati wa jioni Uria akaenda kulala kitandani pake pamoja na watumish wa bwana wake; hakushuka nyumbani kwake.
14 Alors, le lendemain matin, David écrivit une lettre à Joab et l'envoya par les mains d'Urie.
Hivyo asubuhi Daudi akamwandikia Yoabu barua, naye akaituma kwa mkono wa Uria.
15 Or il écrivit en ces termes: Placez Urie à l'endroit où sera le plus fort de la bataille, et retirez-vous d'auprès de lui, afin qu'il soit frappé et qu'il meure.
Ndani ya barua Daudi aliandika hivi, “Mweke Uria mbele ya vita vikali sana, na kisha, mmwache, ili apigwe na afe.
16 Joab, ayant donc considéré la ville, plaça Urie à l'endroit où il savait que seraient les plus vaillants hommes.
Hivyo Yoabu alipoona mji ukizingirwa, alimweka Uria katika sehemu aliyojua askari adui wenye nguvu wangekuwa wakipigana.
17 Et ceux de la ville sortirent et combattirent contre Joab, et plusieurs tombèrent parmi le peuple, d'entre les serviteurs de David. Urie, le Héthien, mourut aussi.
Wakati watu wa mji walipotoka na kupigana dhidi ya jeshi la Yoabu, baadhi ya askari wa Daudi wakaanguka, na Uria Mhiti pia akauwawa.
18 Puis Joab envoya vers David, pour lui faire savoir tout ce qui était arrivé dans le combat.
Wakati Yoabu alipotuma neno kwa mfalme kuhusu hali ya vita,
19 Et il donna cet ordre au messager, et lui dit: Quand tu auras achevé de parler au roi de tout ce qui est arrivé dans le combat,
alimwagiza mjumbe, kusema, “Utakapomaliza kumwambia mfalme kuhusu hali ya vita,
20 S'il arrive que le roi se mette en colère et qu'il te dise: Pourquoi vous êtes-vous approchés de la ville pour combattre? Ne savez-vous pas bien qu'on tire de dessus la muraille?
yawezekana mfalme akakasirika, naye akakwambia, 'Kwa nini mlipigana na mji kwa karibu hivyo, hamkujua kwamba wangeweza kushambulia kutokea ukutani?
21 Qui tua Abimélec, fils de Jérubbésheth? N'est-ce pas une femme qui jeta sur lui un morceau de meule de moulin, du haut de la muraille, et il mourut à Thébets? Pourquoi vous êtes-vous approchés de la muraille? Alors tu lui diras: Ton serviteur Urie, le Héthien, est mort aussi.
Ni nani aliyemwua Abimeleki mwana wa Yerubeshethi? Siye mwanamke aliyerusha jiwe la kusagia juu yake kutoka ukutani, hata akafa huko Thebesi? Kwanini basi mliukaribia ukuta jinsi hiyo? Nawe umjibu, 'Uria mtumishi wako amekufa pia.”
22 Ainsi le messager partit, et, étant arrivé, il fit savoir à David toutes les choses pour lesquelles Joab l'avait envoyé.
Hivyo mjumbe akaondoka na kwenda kwa Daudi akamwambia kila jambo ambalo Yoabu alimtuma kusema.
23 Le messager dit donc à David: Ces gens se sont montrés plus forts que nous, et sont sortis contre nous dans la campagne; mais nous les avons repoussés jusqu'à l'entrée de la porte.
Na mjumbe akamwambia Daudi, “Mwanzoni adui walikuwa na nguvu kuliko sisi; walitukabili uwandani, lakini tukawarudisha nyuma kwenye maingilio ya lango.
24 Et les archers ont tiré contre tes serviteurs, du haut de la muraille, et quelques-uns des serviteurs du roi sont morts; ton serviteur Urie, le Héthien, est mort aussi.
Na wapiga mishale wao wakawarushia watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watumishi wa mfalme wameuawa, na mtumishi wako Uria mhiti pia ameuawa.”
25 Et David dit au messager: Tu diras ainsi à Joab: Que cela ne te peine point; car l'épée dévore tantôt l'un, tantôt l'autre; redouble le combat contre la ville, et détruis-la. Et toi, encourage-le!
Kisha Daudi akamwambia mjumbe, “Mwambie hivi Yoabu, 'Usiruhusu jamba hili likuhuzunishe, kwa maana upanga huangamiza huyu kama uangamizavyo na mwingine. Vifanye vita vyako kuwa vyenye nguvu zaidi dhidi ya mji, na uuteke.' Mtie moyo Yoabu.”
26 Or la femme d'Urie apprit qu'Urie, son mari, était mort, et elle prit le deuil pour son mari.
Hivyo mke Uria aliposikia kwamba mme wake amekufa, akaomboleza sana kwa ajili yake.
27 Quand le deuil fut passé, David envoya, et la recueillit dans sa maison, et elle fut sa femme, et elle lui enfanta un fils. Mais l'action que David avait faite, déplut à l'Éternel.
Huzuni yake ilipoisha, Daudi akatuma na kumchukua kwake katika kasri lake, naye akawa mkewe na akamzalia mwana. Lakini alichokifanya Daudi hakikumpendeza Yahwe.