< 2 Rois 16 >
1 La dix-septième année de Pékach, fils de Rémalia, Achaz, fils de Jotham, roi de Juda, commença à régner.
Katika mwaka wa kumi na saba wa Peka mwana wa Pemalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda, akaanza kutawala.
2 Achaz était âgé de vingt ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem. Il ne fit point ce qui est droit aux yeux de l'Éternel, son Dieu, comme David, son père;
Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala, na alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Alifanya yasiyo haki usoni mwa Yahwe Mungu wake, kama Daudi babu yake.
3 Mais il suivit la voie des rois d'Israël; et même il fit passer son fils par le feu, selon les abominations des nations que l'Éternel avait chassées devant les enfants d'Israël.
Badala yake, akatembea katika njia ya wafalme wa Israeli; hasa, akamuweka mwanaye kwenye moto kama sadaka ya kuteketeza, kufuatana na machukizo ya mataifa, ambayo Yahwe aliwafukuza wana wa Israeli.
4 Il sacrifiait aussi et faisait des encensements dans les hauts lieux, sur les coteaux et sous tout arbre vert.
Akatoa sadaka na kuchoma ubani mahali pa juu, juu ya milima, na chini ya kila mti mbichi.
5 Alors Retsin, roi de Syrie, et Pékach, fils de Rémalia, roi d'Israël, montèrent contre Jérusalem pour combattre, et ils assiégèrent Achaz; mais ils ne purent point en venir à bout par les armes.
Kisha Riseni, mfalme wa Shamu na Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, wakaja mpaka Yerusalemu kuteka. Wakamzunguka Ahazi, lakini hawakuweza kumshinda.
6 En ce temps-là, Retsin, roi de Syrie, remit Élath en la puissance des Syriens, car il déposséda les Juifs d'Élath, et les Syriens vinrent à Élath, où ils ont demeuré jusqu'à ce jour.
Katika kipindi hicho, Resini mfalme wa Shamu akamponya Elathi kwa Shamu na kuwapeleka watu wa Yuda nje ya Elathi. Kisha Washami wakaja kwa Elathi ambapo waliishi hadi leo.
7 Or Achaz avait envoyé des députés à Tiglath-Piléser, roi des Assyriens, pour lui dire: Je suis ton serviteur et ton fils; monte et délivre-moi de la main du roi de Syrie et de la main du roi d'Israël, qui s'élèvent contre moi.
Hivyo Ahazi akatuma wajumbe kwenda kwa Tiglath Pileseri mfalme wa Ashuru, akisema, “Mimi ni mtumishi wako na mwanao. Panda juu na uniokoe kutoka kwenye mikononi ya mfalme wa Shamu na kutoka kwenye mkono wa mfalme wa Israeli, ambao wameniteka.”
8 Et Achaz prit l'argent et l'or qui se trouva dans la maison de l'Éternel et dans les trésors de la maison royale, et il l'envoya en don au roi d'Assyrie.
Hivyo Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa imepatikana katika nyumba ya Yahwe na mingoni mwa waweka hazina wa nyumba ya mfalme na kuituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru.
9 Le roi d'Assyrie fit ce qu'il souhaitait; il monta contre Damas, la prit, en transporta le peuple à Kir, et fit mourir Retsin.
Kisha mfalme wa Ashuru akamsikiliza, na mfalme wa Ashuru akaenda juu dhidi ya Damaski, akaishinda na kuwabeba watu wake kama wafungwa hadi Kiri. Akamuua Resini pia yule mfalme wa Shamu.
10 Alors le roi Achaz s'en alla à Damas au-devant de Tiglath-Piléser, roi d'Assyrie. Or le roi Achaz, ayant vu l'autel qui était à Damas, envoya à Urie, le sacrificateur, le dessin et le modèle de cet autel, selon toute sa construction.
Mfalme Ahazi akaenda Dameski kuonana na Tiglath Pileseri mfalme wa Ashuru. akaiona mdhabahu huko Damski. Akampelekea Uria kuhani mfano wa ile madhabahu na mpangilio wake na mchoro kwa ustadi wote ulikuwa umehitajika.
11 Et Urie, le sacrificateur, bâtit un autel suivant tout ce que le roi Achaz avait mandé de Damas. Urie, le sacrificateur, le fit avant que le roi fût revenu de Damas.
Hivyo Uria yule kuhani akajenga madhabahu kuwa kama mipango ambayo Mfalme Ahazi atakaporudi kutoka Damaski. Akaimaliza kabla mfalme Ahazi hajarudi kutoka Dameski.
12 Et quand le roi Achaz fut revenu de Damas et qu'il eut vu l'autel, il s'en approcha et y monta.
Kisha mfalme akaja kuto Dameski akaiona ile madhabahu; mfalme akaikaribia ile madhabahu na kutoa sadaka juu yake.
13 Il fit fumer sur cet autel son holocauste et son oblation, y versa ses libations et y répandit le sang de ses sacrifices de prospérités.
Akatengeneza sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka, na kunyunyiza damu ya washirika wake sadaka juu ya madhabahu.
14 Quant à l'autel d'airain qui était devant l'Éternel, il le transporta de devant la maison, en sorte qu'il ne fût point entre son autel et la maison de l'Éternel; et il le mit à côté de cet autel-là, vers le nord.
Madhabahu ya shaba ambayo ilikuwa mbele ya Yahwe-akaileta kutoka mbele ya hekalu, kutoka kati ya madhabahu yake na hekalu la Yahwe na kuiweka upande wa kaskazini wa madhabahu yake.
15 Puis le roi Achaz donna ce commandement à Urie, le sacrificateur: Tu feras fumer sur le grand autel l'holocauste du matin et l'oblation du soir, l'holocauste du roi et son oblation, l'holocauste de tout le peuple du pays et leurs oblations; tu y répandras leurs libations, tout le sang des holocaustes, et tout le sang des sacrifices. Mais, quant à l'autel d'airain, ce sera à moi d'examiner.
Kisha mfalme Ahazi akamwiamuru Uria kuhani, akisema, “Juu ya madhabahu kubwa teketeza sadaka ya kutekezwa ya asubuhi na sadaka ya kuteketezwa ya nafaka ya jioni, pamoja na sadaka ya watu wote wa nchi, na matoleo ya sadaka ya mazao na sadaka zao za kinywaji. Nyunyiza juu ya hiyo damu yote ya sadaka ya kuteketeza, na damu yote ya kuteketeza. Lakini ile madhabahu ya shaba itakuwa kwa ajili yangu ili niulize ushauri.”
16 Or Urie, le sacrificateur, fit tout ce que le roi Achaz lui avait commandé.
Uria kuhani akafanya kile ambacho Ahazi aliamuru.
17 De plus le roi Achaz mit en morceaux les panneaux des socles et en ôta les cuves qui étaient dessus; il descendit la mer de dessus les bœufs d'airain qui étaient dessous, et la mit sur un pavé de pierre.
Kisha mfalme Ahazi akaondoa jopo na mabeseni vitako vinavyobebeka; pia akachukua bahari kutoka juu ya ng'ombe wa shaba ambayo ilikuwa chini ya hiyo na kuiweka juu ya sakafu ya mawe.
18 Il ôta aussi de la maison de l'Éternel, à cause du roi d'Assyrie, le portique couvert du sabbat, qu'on avait bâti au temple, et l'entrée du roi, qui était en dehors.
Aliondoa njia iliyokuwa kwa ajili ya kuingia kwenye Sabato ambayo walikuwa wamejenga kwenye hekalu, wote pamoja na mahali pa kuingilia mfalme kwenye hekalu la Yahwe, kwasababu ya mfalme wa Ashuru.
19 Le reste des actions d'Achaz, et ce qu'il fit, n'est-il pas écrit au livre des Chroniques des rois de Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Ahazi na yale aliyoyafanya, je yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
20 Puis Achaz s'endormit avec ses pères et fut enseveli avec eux dans la cité de David, et Ézéchias, son fils, régna à sa place.
Ahazi alilala pamoja na babu zake na kuzikwa pamoja babu zake katika mji wa Daudi. Hezekia mtoto wake akawa mfalme katika mahala pake.