< 2 Chroniques 15 >
1 Alors l'Esprit de Dieu fut sur Azaria, fils d'Oded.
Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
2 Et il sortit au-devant d'Asa, et lui dit: Asa, et tout Juda et Benjamin, écoutez-moi! L'Éternel est avec vous quand vous êtes avec lui. Si vous le cherchez, vous le trouverez; mais si vous l'abandonnez, il vous abandonnera.
Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
3 Pendant longtemps Israël a été sans vrai Dieu, sans sacrificateur qui enseignât, et sans loi;
Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
4 Mais dans sa détresse il revint à l'Éternel, le Dieu d'Israël; ils le recherchèrent, et il se laissa trouver d'eux.
Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
5 Dans ces temps-là, il n'y avait point de sécurité pour ceux qui allaient et venaient, car il y avait de grands troubles parmi tous les habitants du pays.
Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
6 Une nation était heurtée par une autre, et une ville par une autre ville; car Dieu les agitait par toutes sortes d'angoisses.
Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
7 Mais vous, fortifiez-vous, et que vos mains ne soient point lâches; car il y a un salaire pour ce que vous ferez.
Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
8 Quand Asa eut entendu ces paroles et la prophétie d'Oded, le prophète, il se fortifia, et fit disparaître les abominations de tout le pays de Juda et de Benjamin, et des villes qu'il avait prises dans la montagne d'Éphraïm; et il rétablit l'autel de l'Éternel, qui était devant le portique de l'Éternel.
Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
9 Puis il rassembla tout Juda et Benjamin, et ceux d'Éphraïm, de Manassé et de Siméon, qui demeuraient avec eux; car un grand nombre de gens d'Israël passaient à lui, voyant que l'Éternel son Dieu était avec lui.
Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
10 Ils s'assemblèrent donc à Jérusalem, le troisième mois de la quinzième année du règne d'Asa;
Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11 Et ils sacrifièrent, ce jour-là, à l'Éternel, sept cents bœufs et sept mille brebis, du butin qu'ils avaient amené.
Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
12 Et ils rentrèrent dans l'alliance, pour chercher l'Éternel, le Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme;
Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
13 En sorte qu'on devait faire mourir tous ceux qui ne rechercheraient pas l'Éternel, le Dieu d'Israël, tant les petits que les grands, tant les hommes que les femmes.
Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
14 Et ils prêtèrent serment à l'Éternel, à haute voix, avec acclamation, et au son des trompettes et des cors;
Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
15 Et tout Juda se réjouit de ce serment, parce qu'ils avaient juré de tout leur cœur, et qu'ils avaient recherché l'Éternel de leur plein gré, et qu'ils l'avaient trouvé. Et l'Éternel leur donna du repos de tous côtés.
Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
16 Le roi Asa destitua même de son rang sa mère, Maaca, parce qu'elle avait fait une idole pour Ashéra. Asa abattit son idole, la mit en pièces, et la brûla au torrent de Cédron.
Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
17 Mais les hauts lieux ne furent point ôtés du milieu d'Israël; néanmoins le cœur d'Asa fut intègre tout le long de ses jours.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
18 Il remit dans la maison de Dieu les choses qui avaient été consacrées par son père, avec ce qu'il avait lui-même consacré, l'argent, l'or et les ustensiles.
Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
19 Et il n'y eut point de guerre jusqu'à la trente-cinquième année du règne d'Asa.
Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.